Friday, March 11, 2016

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Norway

 Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway Bi. Tone Skogen kushoto aliyemtembelea leo katika ofisi za Wizara, ambapo katika mazungumzo yao walijadili mahusiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Norway ambapo Norway imekuwa ikisaidia katika sekta ya Nishati na  Elimu hasa katika taaluma ya Uhandisi, pia ni mdau katika kupigania haki za binadamu pamoja na masuala ya jinsia.
 Maafisa waliofuatana na Mhe. Tone Skogen wakifuatilia mazungumzo.
 Sehemu nyingine ya maafisa hao wakifuatilia mazungumzo.
 Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa Balozi Joseph Sokoine kushoto pamoja na afisa mambo ya nje wakifuatilia Mazungumzo.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.