Wednesday, March 2, 2016

Ujumbe wa Vietnam wakutana na Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje.

Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhan Muombwa (kulia) akizungumza na Naibu Mkuu wa Itifaki wa Vietnam, Bw. Giang Son kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Vietnam.
Sehemu ya ujumbe kutoka Vietnam ukiongozwa na Balozi wa Vietnam hapa nchini, Mhe. Vo Thanh Nam (wa pili kulia), wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki,(wa kwanza kushoto) kwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara hiyo Bi. Mindi Kasiga  na Maafisa wa Wizara hiyo nao wakifuatilia mazungumzo hayo.
Kikao kikiendelea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.