Wednesday, March 30, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Brazil nchini

Naibu Waziri wa Mambo za Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Brazil hapa nchini, Mhe. Carlos Alfonso Iglesias Puente, zoezi hilo lilifanyika tarehe 30 Machi, 2016 Wizarani Jijini Dar es Salaam. 
Balozi Mteule wa Brazil hapa nchini, Mhe. Carlos Alfonso Iglesias Puente, akizungumza jambo kwa Naibu Waziri Mhe. Susan Kolimba, muda mfupi baada ya kuwasilisha Nakala za Hati zake za Utambulisho.
 Naibu Waziri Mhe. Susan Kolimba, akimweleza jambo Balozi Mteule wa Brazil hapa nchini, Mhe. Carlos Alfonso Iglesias Puente.
 Mazungumzo yakiendelea huku Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana (kulia kwa Naibu Waziri),  Afisa Mambo ya Nje Bw. Lucas Mayenga, Msaidizi wa Naibu Waziri (wa mwisho kulia), pamoja na Msaidizi wa Balozi Mteule (wa kwanza kushoto) kwa pamoja wakifuatilia mazungumzo hayo.
 Naibu Waziri Dkt. Susan Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Brazil hapa nchini, Mhe. Carlos Alfonso Iglesias Puente.
Picha ya pamoja.
=========================
Picha na Reuben Mchome.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.