Thursday, March 17, 2016

Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini wafanya Ziara Kilosa

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. John Henjewele akitoa taarifa ya Wilaya na historia ya migogoro kwa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini ambao walitembelea jamii ya wafugaji na wakulima Wilayani humo kwa lengo la kuwashawishi kuwa wavumilivu kwa kila mmoja katika kutatua migogoro ya Ardhi na kuimaliza kabisa, sambamba na kutoa vifaa kwa watoto wa shule katika shule ya Sekondari Parakuyo na shule za msingi Mabwerebwere, Tindiga na Ulaya. Kauli mbiu ya Ziara hiyo ilikuwa "Tusipigane Tuzungumze Wakulima na Wafugaji Tushirikiane kudumisha Amani

Sehemu ya Maafisa walioshiriki Ziara wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikiwasilishwa na Mhe. Henjewele. 

Maafisa Habari kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakikabidhi fulana kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Parakuyo Wilayani Kilosa, kutoka kushoto Bi. Rose Mbilinyi, kutoka kulia Bw. Ally Kondo na Bw. Teodos Komba. Vilevile maafisa hao walikabidhi msaada wa Vitabu, Zana za Kufundishia na Madawati.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tindiga Wilayani Kilosa wakiwa wamekaa katika Madawati waliyokabidhiwa na Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini, ambapo shule hiyo ilipokea msaada wa Madawati 50.


========================================================================


Ziara hiyo ni miongoni mwa shughuli zilizofanyika wakati Kikao Kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kikiendelea, Kikao hicho kilifunguliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye tarehe 14 Machi na kinatarajiwa kumalizika tarehe 18 Machi,2016.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akifungua Kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini nchini hawapo pichani kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel ambapo alieleza lengo la kikao hicho ni kupeana na kushirikishana uzoefu ili kuboresha utendaji na kuleta ufanisi kwa maafisa hao, Pia aliwasisitiza ni vema kila Afisa akaonesha uwezo binafsi ili kuweza kukubalika na kuthaminiwa kwa nafasi yake katika Tasisi anayoiwakilisha.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Bi. Mindi Kasiga kati akiwa na baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini wakifuatilia kikao.
Mkufunzi kutoka Chuo cha Diplomasia Kurasini Dar es salaam Bw. Luke Chilambo ambaye alikuwa miongoni mwa wawezeshaji katika kikao kazi hicho akitoa mada kuhusiana na Diplomasia na Itifaki.
Bi Joy Nyabongo ambaye ni muwezeshaji na mtoa mada ya Huduma kwa Mteja akitoa Zawadi kwa mshindi wa pili Bi. Mindi Kasiga baada ya kushinda jaribio la uelewa wa mada hiyo.
Mhe. Waziri Nape na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa Habari na Mawasiliano kutoka Serikali kuu.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.