Wednesday, March 9, 2016

Rais wa Vietnam awasili nchini kuanza ziara ya kwanza ya kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Mhe. Truong Tang San (kushoto) pamoja na mkewe Mama Mai Thi Hann wakipunga mkono mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere kwa ajili ya kuanza ziara ya kwanza ya kitaifa nchini.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akimpokea Rais wa Vietnam Mhe. Troung Tang San kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mara baada ya kuwasili nchini
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa (kulia) akimtambulisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga ( wa pili kushoto) kwa Rais wa Vietnam Mhe. Truong Tang San (mwenye tai ya Blue).
Rais Truong Tang San akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Autralasia katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki
Rais Troung Tang San pamoja na Mkewe Bi. Mai Thi Hahn (mwenye nguo ya bluu) wakitizama kikundi cha ngoma kilichokuwapo Uwanja wa Ndege.
Waziri wa Mambo ya Nje akizungumza na waandishi wa habari waliojitokeza kumlaki Rais Truong Tang San
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa akiagana na Rais Truong Tang San mara baada ya kuwasili hotelini kwake.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Paul Makonda akimweleza jambo Balozi Mbelwa wakati wa mapokezi ya Rais Truong wa Vietnam.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.