Tuesday, March 15, 2016

Mabalozi wa Afrika wampa pole Mhe. Dkt. Kikwete kwa kifo cha kaka yake

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimweleza jambo Kaimu Kiongozi wa Mabalozi kutoka nchi za Afrika wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Zimbabwe, Mhe. Edzai Chimonyo walipofika nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpa pole kufuatia kifo cha Kaka yake Marehemu Suleiman Kikwete kilichotokea hivi karibuni.
Sehemu ya Mablozi wakifuatilia mazungumzo na Mhe. Dkt. Kikwete (hayupo pichani). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo ambaye alifuatana na Mabalozi hao.
Sehemu nyingine ya Mabalozi wakifuatilia mazungumzo na Mhe. Dkt. Kikwete hayupo pichani.
Mhe. Dkt. Kikwete akiendelea na mazungumzo
Mabalozi wakimsikiliza Mhe. Dkt. Kikwete
Mabalozi wakifurahia jambo
Mhe. Dkt. Kikwete akiwaeleza jambo Mabalozi mara baada ya Mabalozi hao kutoa salamu zao za pole
Mhe. Dkt. Kikwete akiagana na Balozi Shelukindo
Mhe. Dkt. Kikwete katika picha ya pamoja na Mabalozi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.