Friday, March 4, 2016

WAKUU WA NCHI WA EAC WAFANYA UZINDUZI UJENZI WA BARABARA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Arusha, viongozi na wawakilishi wa mataifa mbalimbali hawapo pichani ambao walihudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa ujenzi wa mradi wa barabara ya Arusha -Holili/Taveta -Voi km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha, tarehe 3 March,2016.

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Masharika, Kikanda na Kimataifa na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwasilisha taarifa ya Tanzania katika hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa mradi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km234.3.
Mhe. Rais Dkt. Magufuli na Mhe.  Rais Uhuru Kenyatta wakiongoza zoezi maalum la kukata utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Mradi wa barabara Arusha-Holili/Taveta-Voi, wakiwa pamoja na wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na viongozi mbalimbali walioshiriki hafla fupi ya Uzinduzi huo.
Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akiagana na Mhe. Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe tayari kwa kuanza safari ya kurudi nchini Uganda mara baada ya kukamilisha shughuli zilizoambatana na Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta akitoa neno la shukrani kwa waziri wa Nishati na Madini Mhe. Sospeter Muhungo kuishukuru Serikali ya Tanzania tayari kwa safari ya kurudi nchini Kenya mara baada ya kukamilisha ushiriki wa Mkutano na kuzindua mradi wa ujenzi wa barabara unayoiunganisha nchi ya Kenya na Tanzania.

Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ally Mohamed Shein akiondoka katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro kwa safari ya kuelekea visiwani Zanzibar mara baada ya kukamilisha zoezi la uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha -Holili/Taveta-Voi uliofanyika Tengeru nje kidogo ya Jiji la Arusha, tarehe 3 Machi,2016.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.