Wednesday, March 16, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje amuaga Mwendesha Mashitaka wa ICTR-MICT

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,  Mhe. Dkt.Suzan Kolimba (Mb.) akiwa katika picha ya pamoja na Mwendesha Mashtaka wa iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya  Rwanda (ICTR) na ile iliyoririthi shughuli za Mahakama hiyo MICT, Bw. Hassan Bubacar Jallow alipofika Wizarani kwa ajili ya kuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Jallow. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda (wa pili kulia), Dkt. Cheichk Bangoura (kushoto) ambaye ni Mwanasheria wa MICT na Bw. Elisha Suku (kulia), Afisa Mambo ya Nje.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.