Tuesday, March 8, 2016

Waziri Mahiga akutana na Waziri wa Uingereza wa masuala ya Afrika


Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. James Duddridge, mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara ambapo waliweza kufanya mazungumzo. 
Mhe. Waziri Mahiga akiendelea na Ukaribisho kwa Mhe. Balozi Diana Melrose ambaye aliambatana na Mhe. Waziri James Duddridge katika mazungumzo hayo.
Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na Mhe. Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika ambapo katika mazungumzo yao waliweza kujadili masuala ya maendeleo hususan katika sekta ya uwekezaji na biashara pamoja na kuangalia namna Serikali ya Uingereza inavyoweza kushirikiana na Tanzania katika kukuza uchumi na kuimarisha viwanda.
Mhe. Balozi Diana Melrose pamoja na afisa aliyeambatana naye wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Waziri Mahiga na Mhe. Waziri James Duddridge.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine wa kwanza kushoto, akiwa pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Mona Mahecha na Msaidizi wa Waziri Bw. Thobias Makoba kulia wakifuatilia mazungumzo pia.
Mhe. Waziri Mahiga akiagana na Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika mara baada ya kumaliza mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.