Wednesday, February 17, 2016

Mkurugenzi wa Idara ya Asia azungumza na Balozi wa China nchini

Mhe. Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini, Dkt. Lu Youqing, alipotembelea Wizarani jana. Katika Mazungumzo yao Balozi huyo wa Jamhuri ya Watu wa China nchini alielezea taratibu zinazofanywa na mamlaka za nchi hiyo katika kutekeleza ahadi zake za miaka mitatu (2016-2018) zilizoahidiwa katika Mkutano wa Sita wa kilele cha Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika, ambapo alieleza miradi itakayotekelezwa ni ile ya kuendeleza Viwanda na Ujenzi wa Miundombinu.
Maafisa walioambatana na Mhe. Balozi Dkt. Lu Youquing wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya mabalozi hao.
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakifuatilia mazungumzo.
 Mabalozi wakiagana mara baada ya kumaliza mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.