Friday, February 19, 2016

Dkt. Kolimba akutana na Ujumbe wa Bunge la Sweden


Mhe. Naibu Waziri  wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb) akiukaribisha ujumbe wa wabunge wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Bunge la Sweden walipomtembelea leo ofisini kwake.Wabunge hao wapo nchini kwa madhumuni ya kutathmini na kukagua miradi inayofadhiliwa na Serikali ya Sweden kwa Tanzania ili kubaini utaratibu bora zaidi wa kusaidia Tanzania katika kipindi kijacho.
Mhe. Naibu Waziri (kulia) akizungumza na kiongozi wa ujumbe huo, Mhe. Kenneth G. Forslund ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Sweden. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kolimba alishukuru Serikali ya Sweden kwa misaada yake katika sekta ya elimu ya juu na Bajeti ya Maendeleo. Aidha, Mhe. Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Sweden hususan katika masuala ya kiuchumi na biashara.


Naafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo hayo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine, Bi. Tunsume Mwangolombe, Bw. Adam Issara na Bw. Ally Kondo.


Baadhi ya Waheshimiwa. Wabunge kutoka Sweden wakifuatilia mazungumzo hayo.

Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Wabunge kutoka Sweden.

Mhe. Naibu Waziri, Dkt. Kolimba wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na wabunge wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Bunge la Sweden.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.