Friday, February 19, 2016

MHE.WAZIRI AREJEA KUTOKA ZIARA YA KIKAZI NCHINI RWANDA


WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA RAIS WA RWANDA

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amefanya ziara ya Kikazi Nchi Rwanda na kuonana na Rais wanchi hiyo Mhe. Paul Kagame. Waziri Mahiga alifanya ziara hiyo akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere mara baada ya kuwasili, amesema ziara hiyo ya kikazi nchini Rwanda ililenga kuonana na Rais wanchi hiyo Mhe. Paul Kagame kwakuwa ni jirani na ni mmoja wa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo pia walitumia fursa hiyo kujadili masuala mbambali kuhusu Jumuiya.

Aidha katika mazungumzo hayo walijadili suala la mgogoro wa kisiasa wa nchini Burundi na kwa pomoja kuangalia namna bora zaidi ya kurejesha amani ya kudumu katika nchi hiyo.
 Pia Mhe. Waziri alipata fursa ya kuzungumza na wafanyabishara wa Nchini Rwanda ambapo wamesifu utendaji wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli. Wafanyabiashara hao wamesifu utendaji wa Serikali kwa hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kuboresha utendaji wa taasisi zake ikiwamo Bandari. “Nimepewa salamu za pongezi na wafanyabiashara wa Rwanda nizilete kwa Serikali ya Tanzania kwa kazi nzuri iliyofanywa na Serikali na wameahidi kuongeza ushirikiano wa kibishara baina ya nchi hizi mbili” alisema Waziri Mahiga.
 
Vilevile Rais Mhe. Paul Kagame katika mazungumzo hayo amesisitiza ujenzi wa mradi wa reli ya ukanda wa kati ambayo itasaidia kukuza biashara zaidi baina ya nchi hizi mbili na kuongeza fursa za uwekezaji.
Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, akiwasili uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere akitokea Nchini Rwanda ambako alienda kumuwakilisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Mhe. Waziri akijadili jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga akimkaribisha Mhe. Waziri kuongea na waandishi wa habari juu ya lengo la safari ya kwenda nchini Rwanda na manufaa yake kwa Taifa, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Mhe. Balozi Samuel Shelukindo.
Sehemu ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano.
Mhe. Waziri akiongea na waandishi wa habari na kuwaeleza safari ilikuwa na lengo la kuonana na Mhe. Rais Paul Kagame kama jirani na mwanachama wa Jumuiya ya Afrika mashariki na kufanya mazungumzo naye juu ya hali ya kisiasa nchini Burundi pia aliweza kuzungumza na wafanyabiashara nchini Rwanda ambao walieleza kuridhishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano. 

Wakizungumza mara baada ya kumaliza Mkutano na vyombo vya habari.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.