Monday, February 22, 2016

Kituo maarufu cha Televisheni cha Marekani kuitangaza Ngorongoro moja kwa moja

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje , Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga akizungumza na Kaimu Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Bw. Julius Kibebe alipowasili Ofisini kwake kwa ajili ya  kuratibu  urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja na Kituo maarufu cha Televisheni cha Marekani ABC News kutokea Bonde la Ngorongoro yatakayofanyika tarehe 23 Februari, 2016. Matangazo hayo ambayo yatatazamwa na watu milioni tano wa Jijini New York na takribani watu milioni 52 nchini Marekani yanakusudia kutangaza Hifadhi hiyo ya kipekee duniani pamoja na kuelezea jitihada za Serikali ya Tanzania kwenye uhifadhi wa mazingira. Bi. Kasiga anaiwakilisha Wizara kwenye uratibu wa tukio hilo kwa kushirikiana na Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali.
Bi. Kasiga akifafanua jambo huku Bw. Kibebe (kulia) na Bw. Asante Melita (kushoto), Mhifadhi na Mratibu wa Tukio hilo wakimsikiliza



Bi. Kasiga akioneshwa namna matangazo hayo yatakavyorushwa na Fundi Mitambo Mkuu wa ABC News, Bw. John.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.