Friday, January 12, 2024

DKT. MWINYI AONGOZA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA MAPINDUZI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Maadhimisho hayo yamefanyika katika Uwanja wa New Amani Complex, Mkoa wa Mjini- Magharibi Unguja, ambapo pia imehudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Sherehe za mapinduzi zimehudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa mataifa jirani ambao ni Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Museveni, Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Rigathi Gachagua pamoja na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Doto Biteko.

Viongozi wengine ni pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Akson pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali zote mbili.

Akitoa salamu katika sherehe hizo, Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Museveni ameipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuadhimisha miaka 60 ya mapinduzi matukufu.

“Nawashukuru na kuwapongeza wazanzibar na watanzania kwa ujumla kwa kuulinda Muungano, nawasihi tuendelee kushikamana na kuwa wamoja kwani tumebaini kuwa Bara la Afrika haliwezi kuendelea bila kushikamana,” Alisema Mhe. Museveni

Naye Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame ameipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mapinduzi, na kusema kuwa kufanyika kwa Mapinduzi kumedhihirisha ushirikiano na umoja wa Wazanzibar na Watanzania kwa ujumla. 

Kadhalika, Naibu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe.Rigathi Gachagua ameipongeza Zanzibar na kuwasihi kuendelea kushikamana kama kaka na dada na kuhakikisha umoja wetu hautenganishwi na jambo lolote. “Nawapongeza Wazanzibar kwa kuadhimisha miaka 60 ya mapinduzi,” alisema.

Viongozi wengine walioshiriki sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ni Waziri Mkuu wa Burundi Mhe. Gervais Ndirakobuca na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Marais wastaafu walioshiriki ni pamoja na Rais Mustaafu wa awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, Rais wa awamu ya sita wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mhe. Aman Abeid Karume. Wengine ni Mawaziri Wakuu Wastaafu, Mhe. Fredrick Sumaye, Mhe. Peter Pinda pamoja na Mawaziri mbalimbali.

Mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika Januari 12 mwaka 1964 ambapo chama cha Afro Shirazi kwa kushirikiana na wanachama wa Chama cha Umma waliiondoa madarakani serikali ya mseto wa vyama vya Wazalendo wa Zanzibar, ZNP, na Chama cha Watu wa Zanzibar na Pemba, ZPPP na kutangaza Jamhuri ya Watu wa Zanzibar badala ya serikali ya Kisultani.

Tukio hilo lilichochea/waafrika wengi, kutanzua tatizo hilo, vyama viwili vya waafrika, Afro Shirazi Party (ASP) viliungana na Umma Party kuongeza nguvu, tarehe 12 Januari 1964, ASP ikiongozwa na John Okello, ilihamasisha wanamapinduzi wapatao 600 kuingia mji wa Zanzibar (Unguja) na kupindua Serikali ya Sultani.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia wananchi waliojitokeza kushiriki sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akikagua gwaride katika sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi (mgeni rasmi) pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akifuatilia sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Uganda Mheshimiwa Yoweri Museveni akiongea katika sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Rwanda Mheshimiwa Paul Kagame akiongea katika sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) pamoja na viongozi mbalimbali wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.