Tuesday, January 23, 2024

MAKAMU WA RAIS WA CUBA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 23 - 25 Januari, 2024. 

Mara baada ya kuwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Mesa alipokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb.)

Akiwa nchini, Mhe. Mesa atakutana kwa mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete na pia atatembelea Taasisi ya Mwalimu Nyerere.

Mhe. Mesa pia atamtembelea Mjane wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mama Maria Nyerere pamoja na kutembelea kiwanda kinachozalisha dawa za viuadudu ya Biolarvicide cha Kibaha, Pwani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa akisalimiana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Humphrey Polepole baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.