Wednesday, January 24, 2024

NAIBU WAZIRI MKUU WA CHINA AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI

Naibu Waziri Mkuu wa China, Mhe. Liu Guozhong amehitimisha ziara yake ya kikazi nchini aliyoianza tarehe 22 Januari 2024. 

Baada ya kuhitimisha ziara hiyo Mhe. Guozhong ameagwa na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb.) ambaye aliambatana na viongozi wengine waandamizi wa Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) tarehe 24 Januari 2024 jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb.) (wa pili kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (katikati), Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, Khamis Omar wakimuaga Mhe. Gouzhong.

Wakiteta jambo wakati wa kumuaga Mhe. Gouzhong.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.