Thursday, January 25, 2024

MAKAMU WA RAIS WA CUBA AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI


Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa amemaliza ziara ya kikazi ya siku tatu nchini aliyoifanya kuanzia tarehe 23 hadi 25 Januari, 2025.

 

Akiwa nchini, Mhe. Mesa alikutana kwa mazungumzo na Mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango.

 

Katika mazungumzo yao, Viongozi hao walikubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kihistoria baina ya Tanzania na Cuba hususan kwenye maeneo ya kimkakati ya kilimo, afya, teknolojia na elimu.

 

Vilevile viongozi hao walishuhudia utiaji saini wa Hati mbili za Makubaliano ya Ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Chuo Kikuu cha Artimesa Diaz Gonzalez cha Cuba. 

 

Hati ya pili ya Makubaliano iliyosainiwa ilihusu ushirikiano  kati ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania(TMDA) na Kituo cha Afya cha Taifa cha Udhibiti na Vifaa Tiba (CECMED) cha Serikali ya Cuba kwa lengo la kupanua wigo na kuongeza matumizi ya teknolojia katika masuala ya dawa na vifaa tiba.

 

Mhe. Mesa pia alitembelea Taasisi ya Mwalimu Nyerere ya jijini Dar es Salaam pamoja na kutembelea Kiwanda cha Viuadudu cha Biotech kilichopo Kibaha, Pwani.

 

Mhe. Mesa pia alipata nafasi ya kumtembelea Mjane wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere kwenye makazi yake jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumsalimia na kumjulia hali.

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa akiagana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024. Akiwa nchini, pamoja na mambo mengine Mhe. Mesa alikutana kwa mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango pamoja na kutembelea taasisi mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Mwalimu Nyerere. Katikati anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk
Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Humphrey Polepole mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024. Wengine wanaoshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa (wa kwanza kulia) akifuatiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme
Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa akiagana na Maafisa wa Ubalozi wa Cuba nchini  mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024.
Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa akiagana na wadau mbalimbali
Mhe. Kairuki akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk wakati wa hafla ya kumuaga Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa 
Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wakati wa hafla ya kumuaga Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024.
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu akiagana na Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa  mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024.
Mawaziri wakimpungia mkono wa kwaheri Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Mesa  mara baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu nchini aliyoianza tarehe 23 hadi 25 Januari, 2024.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.