Monday, January 22, 2024

NAIBU WAZIRI MKUU WA CHINA MHE. LIU ATEMBELEA JKCI

 

Naibu Waziri Mkuu wa China, Mhe. Liu Guozhong ametembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo tarehe 21 Januari 2024 na kupokelewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Mhe. Dkt. Godwin Mollel. 

Akiwa katika Taasisi hiyo, Mhe. Liu alipokea taarifa ya utendaji kazi iliyowasilishwa kwake na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dkt. Peter Kisenge pamoja na kutembelea chumba cha upasuaji mdogo na mkubwa wa moyo na chumba cha wagonjwa mahututi wa moyo. 

JKCI imejengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China kuanzia mwaka 2006 na kukamilika mwaka 2014 kwa ajili ya kutoa matibabu ya moyo nchini.

Taasisi ya JKCI inashirikiana na Taasisi za afya za China katika maeneo ya kubadilishana ujuzi na utaalam, utafiti, vifaa tiba na huduma za upasuaji wa moyo.


Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China na Mjumbe wa Kamati Kuu ya 20 ya Chama cha Kikomunisti cha China, Mhe. Liu Gouzhong akipokelewa na Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Godwin Mollel baada ya kuwasili katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete-JKCI tarehe 22 Januari 2024 jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China na Mjumbe wa Kamati Kuu ya 20 ya Chama cha Kikomunisti cha China, Mhe. Liu Gouzhong (wa pili kushoto) akisikiliza taarifa ya utendaji kazi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete-JKCI (wa pili kulia), Dkt. Peter Kisenge alipotembelea taasisi hiyo tarehe 22 Januari 2024 jijini Dar es Salaam. 


Mhe. Liu akieleza jambo wakati wa ziara hiyo.

Ziara ikiendelea.

Picha ya pamoja, Mhe. Liu (wa tano kutoka kulia), Mhe. Dkt. Mollel (wa sita kutoka kulia), Dkt. Kisenge na ujumbe kutoka Serikali ya China na  wafanyakazi wa Taasisi ya JKCI


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.