Wednesday, January 24, 2024

MAKAMU WA RAIS WA CUBA ATEMBELEA KIWANDA CHA VIUADUDU CHA KIBAHA

Makamu  Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa amesema Serikali ya Cuba itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha  kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha  mkoani Pwani ili kiendelee kuhudumia Watanzania na nchi nyingine za Afrika.


Mhe. Mesa ametoa kauli hiyo leo tarehe 24 Januari 2024 alipotembelea Kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu nchini kuanzia tarehe 23 hadi 25 Januari 2024.


Amesema nchi yake itaendelea kutoa msaada wa kitaalam kwa mamlaka za Tanzania ili kukiwezesha kiwanda hicho kuzalisha bidhaa tofautitouti mbali na viuadudu vya malaria,  zikiwemo mbolea, viuatilifu na bidhaa nyingine za kilimo


Pia amesema kiwanda hicho kitaendelea kuwa mfano wa ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya Tanzania na Cuba katika sekta mbalimbali ikiwemo ya afya.


“Nimepata bahati ya kukitembelea kiwanda hiki kwa mara ya pili sasa, mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2016 wakati kinakamilishwa. Napongeza hatua iliyofikiwa kwenye uzalishaji” amesema Mhe. Mesa.



Amesema kiwanda hicho kinatakiwa kutunzwa kwani ni chanzo cha ajira kwa watanzania lakini pia kinakuza uchumi wa Tanzania pamoja na kuimarisha afya za watanzania.


Awali akizungumza kumkaribisha Mhe. Mesa katika kiwanda hicho, Mkuu wa Mkoa wa Pwani , Mhe. Abubakar Kunenge amesema kuwa anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhamasisha uwekezaji wa viwanda kwenye mkoa huo na kuwakaribisha wawekezaji zaidi kutoka Cuba kuja kuwekeza.


Miongoni mwa Viongozi wengine walioshiriki ziara ya Mhe. Mesa kwenye kiwanda hicho ni Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki, Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Humphrey Polepole na Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe. Yordenis Despaigne Vera. 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akimpokea Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Mesa mara baada ya kuwasili katika kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani. Mhe. Mesa yupo nchini kwa ziara ya siku tatu kuanzia tarehe 23 hadi 25 Januari 2024
Mhe. Mesa akiwa amepokelewa na Mhe. Dkt. Kijaji mara baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Mhe. Dkt. Kijaji akitoa taarifa fupi kwa Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Mesa baada ya kuwasili kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Mhe. Meda akizungumza alipokitembelea kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani. Kiwanda hicho kimejengwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Cuba

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge akizungumza wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Mesa alipotembelea kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani.
Meza kuu
Waziri wa maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki akifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Mesa alipotembelea kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani.


Viongozi na wageni waalikwa kutoka Mkoa wa Pwani walioshiriki ziara ya Makamu wa Rais wa Cuba alipotembelea kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Mkutano ukiendelea

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.