Saturday, January 13, 2024

TANZANIA, RWANDA ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO UENDELEZAJI WA SEKTA YA MAZIWA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa na Jamhuri ya Rwanda.

Hati hiyo imesainiwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi - Tanzania, Mhe. Abdallah Ulega, (Mb.) na Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar. 

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Ulega alisema Tanzania kwa kushirikiana na Rwanda wakifanya jitihada za pamoja za kuzalisha maziwa ya kutosha na kuyasindika wananchi watapata ajira za kutosha, kuwapatia wananchi lishe pamoja na kupunguza maradhi.

“Tukifanikiwa kuwa na uzalishaji mzuri wa maziwa tutaweza kuongeza uchumi wetu, na kuifanya biashara ya maziwa kuwa kubwa zaidi,” alisema Waziri Ulega.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe alisema amefarijika na hatua hiyo iliyofikiwa kwani waliisubiri muda mrefu na ni imani yake kuwa tija kubwa itapatikana katika sekta ya maziwa kupitia ushirikiano huo.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe. 

Viongozi wengine ni Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Maj. Gen. Ramson Godwin Mwaisaka, Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Hererimana Fatou pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Bodi ya Maziwa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi - Tanzania, Mhe. Abdallah Ulega, (Mb.) akizungumza wakati wa hafla ya kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa na Jamhuri ya Rwanda. Kushoto ni Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar. Wengine pichani ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.). 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi - Tanzania, Mhe. Abdallah Ulega, (Mb.) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe wakisaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa kati ya Tanzania na Rwanda tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar

Waziri wa Mifugo na Uvuvi - Tanzania, Mhe. Abdallah Ulega, (Mb.) akimpongeza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe baada ya kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa kati ya Tanzania na Rwanda tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akizungumza wakati wa Hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa kati ya Tanzania na Rwanda tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar

Viongozi wakiwa katika picha ya pamoja ya kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa kati ya Tanzania na Rwanda tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar

Viongozi na badhi ya watumishi wakiwa katika picha ya pamoja ya kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika uendelezaji wa Sekta ya Maziwa kati ya Tanzania na Rwanda tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akizungumza na Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe. Jen. (Rtd.) James Kabarebe tarehe 12 Januari 2024, Visiwani Zanzibar


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.