Sunday, October 30, 2011

Closing CHOGM Press Conference Official Photos

Commonwealth Heads of Government Meeting, Perth 2011

CHOGM 2011- The Prime Minister of Trinidad and Tobago The Honourable Kamla Persad Bissessar, The Prime Minister and Minister of Foreign Affairs for Samoa The Honourable Tuilaepa Lupesoliai Sailele Malieliegaoi, The Commonwealth Secretary-General His Excellency Kamalesh Sharma, The Australian Prime Minister Julia Gillard, The President of The United Republic of Tanzania His Excellency Jakaya Kikwete, The President of Maldives His Excellency Mohamed Nasheed at CHOGM 30 October 2011.
Photograph by John Donegan/CHOGM.
CHOGM 2011-Concluding Press Conference-The President of Tanzania His Excellency Mr Jakaya Kikwete at a press conferece at the conclusion of The CHOGM 2011 meeting in Perth.
Photograph by Mike Bowers/CHOGM




CHOGM 2011-Concluding Press Conference-FROM LEFT-The Prime Minister of Australia Julia Gillard, The President of Tanzania His Excellency Mr Jakaya Kikwete and The President of The Maldives His Excellency Mr Mohamed Nasheed at a press conference at the conclusion of The CHOGM 2011 meeting in Perth.
Photograph by Mike Bowers/CHOGM



Saturday, October 29, 2011

Waziri Membe akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada Mhe. John Baird baada ya mazungumzo yao tarehe 29-10-2011
 
“Serikali ya Tanzania imedhamiria kutatua tatizo la ajira kwa vijana kwa kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika nyanja ya elimu ya mafunzo ya ufundi”.

Hayo yamebainishwa leo na Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa alipofanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. John Baird mjini Perth, Australia pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Madola (CHOGM).
Katika mazungumzo hayo, Waziri Membe alisisitiza umuhimu wa Tanzania na Canada kushirikiana katika kuendeleza Sekta ya Elimu ya Ufundi nchini Tanzania ili kusaidia kutatua tatizo la ajira kwa vijana.
Waziri Membe alisema Wizara yake ina dhamana ya kushughulikia masuala ya ushirikiano na mataifa mbalimbali duniani kwenye sekta tofauti ili kuleta maendeleo kwa Watanzania. Sekta ya Elimu ya Ufundi imepewa kipaumbele katika mahusiano hayo, ili kuwajengea vijana wengi zaidi nchini Tanzania uwezo wa kujiajiri baada ya kupata elimu ya ufundi.
Kwa kutambua hatua kubwa iliyopigwa na Canada katika sekta ya elimu ya ufundi, Waziri Membe aliiomba Serikali ya Canada kuisaidia Serikali ya Tanzania kujenga uwezo wa taasisi za elimu ya ufundi nchini Tanzania  ili kukuza ujuzi na hatimaye uwezo wa vijana kujiajiri na kuajiriwa.
Kwa upande wake, Waziri Baird alipongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kupiga vita umasiki na aliahidi kuwa Serikali ya Canada itakuwa tayari kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Elimu ya Ufundi.
Pia alielezea uzoefu wa Canada kwenye sekta hiyo ambapo wahitimu wa vyuo vya Elimu ya Ufundi wamefanikiwa kupata ajira kwa urahisi zaidi kuliko wahitimu wa Elimu ya Juu.
Katika Mkutano huo mawaziri hao pia walizungumzia umuhimu wa  kudumisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Canada na Tanzania katika nyanja mbalimbali za ushirikiano na masuala ya kimataifa. 
Mhe. Baird aliishukuru Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika Tume ya Kimataifa inayoshughulikia masuala ya afya ya wakina mama wajawazito na watoto iliyoundwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  ikiongozwa na wenyeviti wenza Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe. Steven Harper, Waziri Mkuu wa Canada.
Mawaziri hao pia walijadili  masuala ya ushirikiano katika ulinzi wa amani na suala la ugaidi katika bahari ya hindi.
 

Friday, October 28, 2011

Speech - Her Majesty the Queen at the CHOGM 2011 Opening Ceremony

Rais Kikwete ahudhuria Ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Madola Leo

Jina la Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete likitangazwa kabla hajaingia ukumbuni.

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akitembea kwenye jukwaa kuu kuelekea sehemu ya kukaa pamoja na wakuu wengine wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola.

Wanakwaya wa kikundi cha wanafunzi wakiimba wimbo wa Taifa wa Australia kabla ya ufungunguzi kuanza.

Sehemu ya burudani zilizopamba shughuli nzima ya ufunguzi

Rais Kikwete (aliyeketi mstari wa katikati wa tatu kutoka kulia) akifuatilia salamu za kiasili zilizotolewa na wananchi wa Australia wenye asili ya "aborigine" kutoka Kusini Magharibi mwa nchi hii kwenye Jamii ya Wanoongar.

Burudani za asili zilipendezesha sherehe za ufunguzi huo.

Wednesday, October 26, 2011

Tanzanian President in Perth, Australia For CHOGM

Mkuu wa Jumuiya ya Watanzania waishio Mjini Perth Asimwe Kabunga akimsikiliza Rais wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha Rais Kikwete aliyewasili Mjini Perth kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa  Jumuiya ya Madola.

By Ichikaeli Maro

President Jakaya Kikwete of Tanzania has arrived in this Western Australia capital to join leaders of the member states of the Commonwealth for the Commonwealth Heads of State and Government Meeting (CHOGM) beginning on Friday.

The president is accompanied by Minister for Foreign Affairs and International Co-operation Bernard Membe, Minister of State at the President's Office responsible for Good Governance, Mr Mathias Chikawe and Zanzibar's Minister of State at the Second Vice-President's Office Mohamed Aboud.

The official opening of the summit on Friday is expected to be attended by 54 Heads of State and Government of Commonwealth members. Queen Elizabeth II, as the Head of the Commonwealth, will officially open the biennial summit.

Security has been intensified in Perth with major streets closed to traffic as delegates arrive here for the summit.

The Commonwealth Heads of Government Meeting takes place every two years to discuss issues pertaining to the Member States of the Commonwealth and agree on collective policies and initiatives.

The theme for this year's summit is 'Building national resilience, building global resilience at a time of global economic and political challenges". Among the issues to be discussed are international peace and security, democracy, good governance, sustainable development, debt management, education, the environment, gender equality, health, human rights, information and communication technology (ICT), law, multilateral trade issues, and small states and youth affairs.

The Commonwealth objectives are outlined in the 1971 Singapore Declaration which committed the Commonwealth to institute world peace, promoting representative democracy, individual liberty and free trade, pursuing equality and opposing racism as well as fighting poverty, ignorance and disease.

Further objectives are included in the 1979 Lusaka (Zambia) Declaration opposing discrimination on the basis of gender and the Langkawi (Malaysia) Declaration of 1989 emphasising environmental sustainability.

According to a programme issued here Tuesday by the CHOGM Organizing Committee, pre-summit activities have been taking place since Monday. They include the Commonwealth Business Forum in which participants will have opportunity to sign new business deals, make contacts and networking.

Other activities of the day included meetings of the Commonwealth and Small States Foreign Ministers, Commonwealth and Small Developing States Foreign Ministers.

Viongozi Jumuiya ya Madola Wapewa Changamoto

Na Anna Nkinda – Perth, Australia
Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia ya Madola wameombwa kuchukua hatua na kuwasaidia mamilioni ya wasichana wanaoozwa kilazima huku wakiwa na umri mdogo na hivyo kukosa haki zao za msingi.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya Habari vilivyohudhuria maandalizi ya mkutano wa Viongozi wa Nchi wanachama wa Jumuia ya Madola (CHOGM) unaotarajia kuanza tarehe 28 hadi 30 mjini Perth nchini Australia inasema kuwa hivi sasa kuna mamilioni ya wasichana wananyanyasika kijinsia kutokana na ndoa za utotoni.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa leo na Plan International na Royal Commonwealth Society inasema kuwa ndoa za lazima na za utotoni ni moja ya vikwazo vikubwa kwa wasichana katika elimu, afya ya uzazi, na uchumi wa mwanamke hivyo basi kuna ulazima kwa jumuia ya madola kuchukua hatua zaidi ili kuzuia wasichana wasilazimishwe kuolewa wakiwa bado au wakiwa tayari kuolewa.
“Jumuia ya madola inatetea haki za binadamu na kaulimbiu yake ya mwaka 2011 ni “Wanawake ni wakala wa mabadiliko” hivyo basi viongozi wa Jumuia hiyo wafanye haraka kuhakikisha kuwa yanapatikana mabadiliko makubwa kwa wanawake na si kubaki kama walivyo”, ilisema taarifa hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Plan Internationa nchini Australia Ian Wishart alisema kuwa ndoa za lazima na za utotoni zinamuweka msichana katika umaskini, kutokuwa na afya njema na ukosefu wa elimu.
“Hivi sasa katika Dunia takwimu zinaonyesha kwamba kuna wasichana milioni 10 wenye umri wa chini ya miaka 18 ambao wanaolewa kila mwaka hii inamaana kuwa kila msichana mmoja anaolewa kila baada ya sekunde tatu”, alisema Wishart.
Aliendelea kusema kuwa wasichana wanaoolewa mapema wanauzoefu wa ukatili wa kijinsia, wanadharauliwa na kulazimishwa kufanya mapenzi hii inawasababishia matatizo ya kijinsia na afya ya uzazi na zaidi wanakosa elimu na hivyo kuwa wajinga..
Wishart alisema, “Ndoa za utotoni na za kulazimishwa ni moja ya vitu vinavyozuia kufika malengo ya milinia ya kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto , upatikanaji wa elimu ya msingi kwa wote, kupunguza umaskini , usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake .
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Royal Commonwealth Society Peter Kellner alisema kuwa Jumuia ya madola iko makini kuhusiana na maendeleo ya wanawake na haki za binadamu, na ina mipango kazi ya kuhakikisha kuwa suala la ndoa za lazima na za utotoni linachukuliwa hatua za haraka na linapata ufumbuzi.
“Wanachama wote wa Jumuia ya Madola wamekubaliana kulinda haki za watoto na wanawake kwani nchi 12 kati ya 20 ambazo zilikuwa na kiwango kikubwa cha ndoa za lazima na za utotoni ni nchi za Jumuia ya madola”, alisema Kellner.
Mwenyekiti huyo aliendelea kusema kuwa mamilioni ya wasichana kila mwaka kupitia Jumuia ya madola wanapata nafasi ya kuondokana na matokeo ya ndoa za lazima na za utotoni hii si kwao tu bali katika familia zao, jamaa zao na jumuia ya madola.
Jumla ya viongozi wa nchi 53 ambao ni wanachama wa Jumuia ya Madola wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo ambao utafunguliwa na Malkia Elizabeth wa pili akiwemo Rais Jakaya Mrisho Kikwete .
Serikali nchini Tanzania kupitia wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ,Taasisi mbalimbali za Kiserikali na zisizo za Kiserikali zinafanyakazi ya kuelimisha jamii ili kuhakikisha kuwa tatizo la ndoa za lazima na za utotoni linamalizika.
Mwisho.

Mhe. Rais na Mama Kikwete wakutana na Jumuiya ya Watanzania waishio Perth Australia Leo



Rais Kikwete akihutubia Watanzania wanaoishi Perth Australia kwenye hafla fupi waliyomuandalia leo tarahe 26-10-2011





Rais Kikwete akipokea zawadi kutoka kwa Mwekahazina wa Jumuiya Maryam Powell iliyotolewa na Watanzania hao kwa Rais kama ishara ya kumbukumbu ya mkutano huo. Walimshukuru Rais Kikwete kwa kuwatembelea na kuahidi kuleta fursa mbalimbali haswa za uwekezaji ili kuendeleza uchumi.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bwana John Haule akisalimiana na Mahir Meghji, Mtanzania anayeishi Perth Australia. Ujumbe wa Watanzania uko Mjini Perth kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya Madola.

Balozi wa Tanzania Nchini Japan na Australia Mhe. Salome Sijaona akisalimiana na mwakilishi wa Jumuiya ya Watanzania waishio Australia.

Katibu wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Perth Australia Pendo Mwaiteleke (wa pili kulia) akiwakaribisha wageni kumsikiliza Rais Kikwete kwenye hafla fupi iliyoandaliwa na Jumuiya hiyo leo Mjini Perth Australia.

Baadhi ya Wabunge na Waziri walioongozana na msafara wa Mhe. Rais Kikwete kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya Madola

Baadhi ya Watanzania na marafiki wa Tanzania waliohudhuria hafla hiyo.

Wana habari walioongozana na msafara wa Rais Kikwete Anna Nkinda (maelezo) na Jaffar Haniu (TBC) nao hawakuwa nyuma kuhakikisha wanapata matukio yote muhimu ya hafla hiyo.

Mama Salma Kikwete akiwa na baadhi ya Watanzania waliohudhuria hafla hiyo.

















Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na Wanajumuiya kwenye picha ya pamoja na viongozi wao

Tuesday, September 13, 2011

Mhe. Haule akutana na Mjumbe Maalum kutoka Australia

(Picha na Mindi Kasiga Tarimo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa)


Maandalizi ya Mkutano wa
Jumuiya ya Madola yaanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule akiwa kwenye mazungumzo na Mjumbe Maalum kutoka Serikali ya Australia, Bw. Leslie Rowe leo tarehe 12 Septemba, 2011.

Bw. Rowe yuko nchini kwenye ziara ya kikazi ya siku tatu kama sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika mjini Perth, Australia mwishoni mwa mwezi ujao. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Dora Msechu.

Thursday, September 8, 2011

New Egyptian Amb. present copy of Credentials

H.E. Hossam Moharam, the newly appointed Ambassador of Egypt to Tanzania, presents a copy of his Credentials to Hon. Bernard K. Membe (MP), the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation. 

Mhe. Membe akutana na Mabalozi nchini


Mheshimiwa Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa leo Jumatano Septemba 7, 2011 amekutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini kwenye ukumbi wa Karimjee.

Katika mkutano huo, Waziri Membe amezungumzia tatizo la umeme nchini na kufafanua mikakati ya Serikali katika kukabiliana na tatizo hilo. Alisema Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeweka mkakati wa muda mfupi ambapo kwa kutumia umeme wa gesi, kutakuwa na ongezeko la megawati mia sita kati ya Disemba 2011 hadi Disemba 2012.

Kupitia mkutano huo, Mhe. Waziri Membe alieleza kwamba suala muhimu katika mgogoro wa Libya si Umoja wa Afrika au Tanzania kulitambua Baraza la Mpito la Libya (NTC) kama nchi za Magharibi zinavyotaka bali Baraza hilo kutambua na kutekeleza roadmap for peace iliyowekwa na Umoja wa Afrika mjini Malabo, Equitorial Guinea kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana nchini humo.

“Tanzania inawapenda sana watu wa Libya na taifa lao, tunataka kuona taifa hilo likishamiri na kurudi kwenye hali ya utulivu na amani ili wananchi wa Libya waendelee kujenga taifa lao” alisema Waziri Membe.

Kuhusu baa la njaa lililoikumba Somalia, Mhe. Waziri Membe aliwaambia mabalozi hao kuwa Serikali ya
Tanzania imetoa msaada wa chakula na misaada mingine ya kibinaadam kwenda nchini humo. Aliishukuru Serikali ya Afrika Kusini kwa kusaidia kusafirisha misaada hiyo kwa ndege hadi Mogadishu, Somalia.

Mwisho, Waziri Membe aliwaarifu mabalozi hao kuhusu nia ya Wizara yake ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika kwa kuwapeleka Mabalozi safari ya kuitambua Tanzania na vivutio vyake. Safari hiyo inayotarajiwa kufanywa mwanzoni mwa mwezi Oktoba, itaanzia Butiama, nyumbani kwa Baba wa Taifa, Hayati Julius Kambarage Nyerere na kuishia Zanzibar, nyumbani kwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Abeid Amani Karume.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Septemba 7, 2011

Monday, September 5, 2011

New Finnish Ambassador presents copy of Credentials to Hon. Membe

(Photo by Tagie Daisy Mwakawago of the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation)

New Finnish Ambassador presents
copy of her Credentials to Hon. Membe

The new Finnish Ambassador to Tanzania, H.E. Sinikka Antila said her country will continue bilateral relations with Tanzania in areas of business partnership, find solutions to the rise in cost of food prices, Northern Africa problems and climate changes which may result in famine crisis facing countries such as Somalia and Ethiopia. 
Madame Antila said this yesterday while presenting a copy of her Credentials to Hon. Bernard K. Membe (MP), the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation in his office.
For his part, Hon. Membe said his government is aware of the crisis of hunger facing African nations, such as Somalia, which has become a priority.  He explained that Somalia alone is facing 3.7 million people without shelter, food, clothing and that it is a first time South Somalia has faced two consecutive dried seasons in the period of 2009/2010 and 2010/2011. 
Hon. Membe also added that in every 10,000 people at least 2 adults and 4 children are dying in Somalia all because of famine resulting from climate changes.   Hon. Membe said Tanzania is the only neighborhood country with food and that it has already pledged 300 tons of maize to be sent to the affected country.  He also added that the public needs to be educated about how to preserve food in times of drought.
On the light note, Madame Antila shared her trip to Tanzania by train using Tanzania Zambia Railway Authority (TAZARA).   During her trip, she had an opportunity to see the beauty of Tanzania as the train crossed through the Selous National Park. 
Prior to her appointment here, Madame Antila was a previous ambassador to Zambia, Malawi and Zimbabwe.    


Hon. Membe in talks with the Nertherlands' Ambassador

The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard K. Membe (MP), had a courtesy call in his office with H.E. Dr. Ad Koekkoek, the Ambassador of the Kingdom of Netherlands in Tanzania. (Photo by Mindi Kasiga Tarimo of the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation) 

Monday, August 29, 2011

Hon. Membe summons the Libyan's Ambassador


The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Hon. Bernard K. Membe (MP) called the Libya`s Ambassador to Tanzania, H.E. Prof. Ahmed A. El Ash`hab to his  office after his Embassy raised the rebel National Transition Council (NTC) flag without prior consultations.  (Photo by Tagie Daisy Mwakawago of the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation)  

Wednesday, July 6, 2011

Rais Kikwete atembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje Sabasaba

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na taasisi zake, wakiwa kwenye picha ya pamoja na Rais Kikwete leo mchana alipotembelea banda lao lililopo ndani ya Banda Kuu la Jakaya Kikwete. Kutoka kushoto ni Tagie Mwakawago, Charles Faini, Mindi Kasiga, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Assah Mwambene, Andes Seiya na Cleophace Ntongani leo tarehe 6.07. 2011.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa leo tarehe 6.07.2011. Pembeni kwake ni mtoto wa Rais Rashid Kikwete ambaye anapenda kuwa mwanadiplomasia. Kulia ni Afisa Mawasiliano wa Wizara Mindi Kasiga.

Afisa Mambo ya Nje Charles Faini akifafanua umuhimu wa kuwa na mahusiano mazuri na nchi mbalimbali kwa wananchi waliokuwa wakimiminika kwa wingi kwenye banda la Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye viwanja vya sababasaba leo tarehe 6.07.2011.


Watoto wa Rais Kikwete wakiwa kwenye banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakitambua bendera za nchi mbalimbali zenye mahusiano ya kidiplomasia na Tanzania.

Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Kificho akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa leo tarehe 6.07.2011.

Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Katinda Kamando akijibu swali la mwananchi kuhusu sera moya ya mambo ya nje kwenye banda la Wizara hiyo leo tarehe 6.07.2011 kwenye maonesho ya sabasaba.