Monday, March 10, 2014

Tanzania na Malawi zasaini Mkataba wa kuanzisha Kituo cha Pamoja cha Uhamiaji na Ushuru wa Forodha




Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum (Mb), kushoto na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Malawi, Mhe. Sosten Gwengwe wakisaini Mkataba wa kuanzisha Kituo cha Pamoja cha Uhamiaji na Ushuru wa Forodha katika mpaka wa Songwe - Kasumulu. Hafla ya uwekaji saini imefanyika katika Ofisi ya Wizara ya Biashara na Viwanda, Lilongwe, Malawi tarehe 10 Machi, 2014.




Mhe. Salum, kulia akitoa neno baada ya shughuli za kusaini Mkataba kukamilika. Anayemsikiliza ni Waziri wa Biashara na Viwanda wa Malawi, Mhe. Gwengwe.



Maafisa wa Tanzania na Malawi wakifanya maandalizi kabla ya Mawaziri kuwasili kwa ajili ya shughuli ya uwekaji saini Mkataba

Waziri wa Nchi wa Serikali ya Zanzibar anayeshughulikia Masuala ya Utawala Bora, Mhe. Mwinyi Haji Makame naye alishuhudia hafla ya uwekaji saini. hapa Mhe. Makame akisaini Kitabu cha wageni alipowasili katika ofisi za Wizara ya Biashara na Viwanda nchini Malawi.

 
Maneno aliyosema Waziri wa Fedha baada ya uwekaji saini
 
Na Ally Kondo. Lilongwe
Nchi za Afrika zimehimizwa kufanya biashara baina yao ili kujiletea maendeleo, badala ya kusubiri misaada isiyokuwa na uhakika kutoka nchi wahisani. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum (Mb) wakati wa hafla ya uwekaji saini Mkataba wa kuanzisha Kituo cha Pamoja cha Uhamiaji na Ushuru wa Forodha cha Songwe – Kasumulu kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Malawi.
 Uwekaji saini huo ulifanyika Lilongwe, Malawi siku ya Jumatatu tarehe 10 Machi, 2014 ambapo Mhe Salum aliwela saini kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, wakati Waziri wa Biashara na Viwanda, Mhe.  Sosten Gwengwe aliweka saini kwa niaba ya Serikali ya Malawi.
Mhe. Salum alieleza kuwa kuanzishwa kwa kituo hicho, kutasaidia, sio tu kupunguza gharama za kufanya biashara kati ya Tanzania na Malawi bali pia kutaimarisha uhusiano baina ya watu wa nchi hizi mbili ambao kimsingi wana utamaduni unaofanana.
Mhe. Waziri aliwataka wataalamu wa pande zote mbili kuandaa mpango kazi wa kutekeleza Mkataba huo haraka iwezekanavyo ili wananchi na Serikali waone matunda yake badala ya kuishia katika makaratasi.
Alipoulizwa na wanahabari kutoa maoni kuhusu utekelezaji wa Mkataba huo, Mhe Wazri aliwahakikishia wananchi wa Malawi na Tanzania kwa ujumla kuwa kituo hicho kitafanya kazi kama ilivyokusudiwa na hakuna tishio lolote la kuvurugika kwa uhusiano kati ya nchi hizi mbili.
Kwa upande wake, Mhe. Gwengwe alifarijika na uanzishwaji wa kituo hicho, kwa kuwa kitarahisisha usafirishaji wa bidhaa kwa haraka kutoka Tanzania kuingia Malawi ambayo haina Bandari.
Uwekaji saini wa Mkataba huo umeenda sambamba na mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Mhe. Salum anaongoza ujumbe wa Tanzania. Mkutano huo ulioanza na vikao vya Makatibu Wakuu unatarajiwa kukamilika tarehe 11 Machi, 2014.
 
 

Saturday, March 8, 2014

Wanawake Mambo ya Nje washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani

Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wameungana na Wanawake wengine kote duniani katika kusheherekea Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Hawa Ghasia (Mb.). Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "CHOCHEA MABADILIKO KULETA USAWA WA KIJINSIA"
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa na nyuso za furaha wakati wa maadhimisho hayo.
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika maandamano.
 Mhe. Ghasia (wa tatu kutoka kushoto) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said Mecky Sadick pamoja na wageni waalikwa katika jukwaa wakiwashangilia Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani) walipokuwa wakipita mbele yao .
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakiwa wamejawa na furaha.
Wanawake  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika Picha ya Pamoja
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bibi Amisa Mwakawago akiwaongoza wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa kutoka uwanjani mara baada ya maadhimisho.
Picha na Reginald Kisaka


Thursday, March 6, 2014

Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai atembelewa na Balozi Mdogo wa Ethiopia

Mhe. Mjenga akimkaribisha ofisini kwake Balozi Mdogo wa Ethiopia Mhe. Yibeltal Alemu.
Wakiwa katika mazungumzo, walipata fursa ya kuzungumzia njia muafaka na mbalimbali za kufanya kazi kwa karibu ili kuhakikisha wanavutia utalii na uwekezaji katika nchi zao hasa kwa kuwavutia wawekezaji wakubwa waliopo Dubai
Mhe. Mjenga alimuomba Mhe. Yibeltal kubadilishana uzoefu wa Ethiopia katika kuvutia wawekezaji kutoka Dubai katika sekta ya kilimo. Pia aliomba Maafisa wa Biashara kutoka Balozi zote mbili wakutane ili kubadilishana uzoefu huo ili Tanzania nayo iweze kuchukua mkondo huo kuwavutia wawejezaji kwenye kilimo.


 


Wednesday, March 5, 2014

Mhe. Rais Kikwete akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufaransa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Biashara za Kimataifa wa Ufaransa, Mhe. Nicole Bricq mara baada ya Waziri huyo kuwasili Ikulu. Mhe. Bricq ameitembelea Tanzania kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchini hizi mbili.
Mhe. Rais Kikwete katika mazungumzo na Mhe.Bricq
Mhe. Rais Kikwete akimsikiliza Mhe.Bricq wakati wa mazungumzo yao.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu pamoja na Wajumbe wengine wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais Kikwete pamoja na Waziri wa Biashara za Kimataifa wa Ufaransa (hawapo pichani).
Balozi wa Ufaransa (katikati) nchini Tanzania pamoja na Ujumbe uliofuatana na Mhe. Bricq wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais Kikwete na Mgeni wake Mhe. Bricq hawapo pichani.
Mhe. Bricq akimkabidhi Mhe. Rais Kikwete ujumbe aliokuja nao.
Mhe. Rais Kikwete akiongozana na Mhe. Bricq mara baada ya mazungumzo
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Bricq, na wajumbe wengine.

Picha na Reginald Kisaka



Tuesday, March 4, 2014

PRESS RELEASE


PRESS RELEASE

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolence message to H.E. Xi Jinping, President of the People’s Republic of China following a terrorist attack that killed 28 people and injuring more than 130 others. 
The message reads as follows;
“H.E. Xi JINPING,
President of the People´s Republic of China,
BEIJING.

Your Excellency and Dear Friend,
I have received with great shock and sadness, the devastating news on the terrorist attack that occurred on the 1st March, 2014, at the square and ticket hall of the Railway Station of Kunming, Capital of China´s South West Yunnan Province, killing at least 28 civilians and injuring more than 130 others.
In this tragic moment and ordeal, I wish, on behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, to convey our deepest condolences to Your Excellency, and through you, to the Government and People of China, especially the family of the victims who have lost their loved ones and who have been severely injured by the attacks.
My government strongly condemns the attacks and calls for the perpetrator to be brought to justice to face the crimes committed.
During this period of mourning, we share with you, your pain over this irreparable loss and pray to the Almighty God to comfort the bereaved families and grant the People of China courage and fortitude to carry on with their daily lives.
May God the Almighty rest the souls of the deceased in eternal peace.
Please accept your Excellency and Dear Friend, the assurances of my highest consideration”.

ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM
4TH MARCH, 2014

Monday, March 3, 2014

Mhe. Membe ashuhudia mpambano kati ya Yanga na Al Ahly ya Misri

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akifuatilia kwa makini pambano la mpira wa miguu kati ya Timu ya Yanga ya Tanzania na Al Ahly ya Misri (hawapo pichani) lilifanyika katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Mhe. Membe alikuwa mgeni rasmi wakati wa pambano hilo ambapo Timu ya Yanga ilijipatia ushindi wa goli 1-0.
Mhe. Membe aliposhindwa kujizuia kusimama wakati Timu ya Yanga (hawapo pichani) ikielekea kufunga goli. Pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said Mecky Sadick.
Mhe. Membe kwa pamoja na Mhe. Mecky Sadick wakifurahia goli pekee lililofungwa na Timu ya Yanga  dhidi ya Al Ahly ya Misri.

Tanzania na Sweden zakubaliana kuimarisha ushirikiano


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Mhe. Tanja Rasmusson, Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Kimataifa wa Sweden alipofika Wizarani leo. Mhe. Rasmusson yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Katika mazungumzo yao waligusia masuala ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara, uwekezaji, elimu, haki za binadamu na vita dhidi ya rushwa.
Mhe. Rasmusson akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Wizarani.
Bw. Haule akizungumza na Mhe. Rasmusson
Mhe. Rasmusson akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule
Wajumbe waliofuatana na Mhe. Rasmusson wakifuatilia mazungumzo kati ya Bw. Haule na Mhe. Rasmusson (hawapo pichani). Wa kwanza kulia ni Balozi wa Sweden hapa nchini, Mhe. Lennarth Hjelmaker.
Wajumbe wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo. Kushoto ni Bibi Victoria Mwakasege, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Lucas Mayenga, Afisa Mambo ya Nje.
Mhe. Rasmusson akifurahia jambo kwa pamoja na Bw. Haule na Balozi Hjelmaker.
Bw. Haule akimsindikiza Mhe. Rasmusson mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Bw. Haule akiagana na Mhe. Rasmusson.

Thursday, February 27, 2014

Matukio mbalimbali ya ziara ya Mhe. Membe nchini China


...Mhe. Membe alipokutana na Makamu wa Rais wa China mjini Beijing
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao alipokutana nae kwa mazungumzo kwenye Jumba la Mikutano la Kitaifa la China maarufu kama People's Great Hall mjini Beijing, China. Mhe. Membe yupo nchini humo kwa ziara ya kikazi ya siku tano kuanzia tarehe 24 hadi 28 Februari, 2014.
Mhe. Membe na Mhe. Yuanchao wakiendelea na mazungumzo.
Mhe. Membe akiagana na Mhe. Yuanchao mara baada ya mazungumzo yao.


....Mhe. Membe alipokutana na Makamu Waziri wa Usalama wa Raia wa China



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Wang Hanning, Makamu Waziri wa Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China alipokutana nae mjini Beijing wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Membe nchini China tarehe 26 Februari, 2014.
Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo na Mhe. Hanning huku Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Abdulrahman Shimbo (kulia kwa Mhe. Membe) na wajumbe waliofuatana na Mhe. Hanning wakisikiliza.

.....Mhe. Membe alipokutana na Makamu Waziri wa Biashara wa China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Mhe. Li Jinzao, Makamu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China kabla ya kufanya mazungumzo rasmi na Waziri huyo wakati wa ziara yake nchini China.
Mhe. Membe (kulia) na Ujumbe wake wakiwa kwenye mkutano wa pamoja na Mhe. Jinzao (kushoto) na ujumbe wake.



Tuesday, February 25, 2014

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo rasmi na Waziri wa Mambo ya Nje wa China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)  akipokelewa na mwenyeji wake Mhe. wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa China mara baada ya kuwasili kwenye  Wizara ya Mambo ya Nje ya China.  
Mhe. Membe na Mhe. Wang Yi katika picha ya pamoja.
Mhe. Membe akiongozana na Mhe. Wang Yi mara baada ya kupokelewa.
Mhe. Membe akisalimiana na aliyewahi kuwa Balozi wa China nchini Tanzania miaka kadhaa iliyopita.Anayeshuhudia pembeni ni Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.







Mhe. Membe awasili nchini China kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Makamu Mkurugenzi wa masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Bi. Sun Baohong mara baada ya Mhe. Membe kuwasili nchini humo kwa ziara ya kikazi ya siku tano.
Mhe. Membe akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ubalozi wa Tanzania nchini China. Kulia ni Mhe. Lt. Jen. (Mstaafu) Abdulrahaman Shimbo, Balozi wa Tanzania nchini China.
Mhe. Membe katika mazungumzo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki. 

Na Mwandishi Wetu, Beijing, China

MHE. BERNARD K. MEMBE (MB.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa amewasili nchini China tarehe 24 Februari 2014 nchini China kwa ziara ya siku tano, na kulakiwa na Bi. Sun Baohong, Makamu Mkurugenzi wa Masuala ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje China. 

Baada ya kuwasili Mhe. Membe alipokea taarifa ya maendeleo ya shuguli za ubalozi kutoka kwa Lt. Jen. (Mstaafu) Abdulrahaman Shimbo, Balozi wa Tanzania hapa China ambapo pia iligusia maeneo ambayo Mhe. Waziri atayatembelea yaani Shenzhen na Guangzhou.  Baadaye Mhe. Membe na ujumbe wake walipata chakula cha usiku na kufanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi Beijing China kuhusu ziara yake na masuala mengine yahusuyo Tanzania. 

Katika salamu zake kwa Watanzania hao ambao walijumuika na wafanyakazi wa Ubalozi na Familia zao, Mhe. Membe alieleza baadhi ya mambo yaliomleta kwenye ziara hii ikiwa ni pamoja na maandalizi ya ziara ya Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete nchini hapa kufuatia mualiko wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. 

Mhe. Membe alielezea pia nia yake na Wizara anayoiongoza ya kukuza na kuendeleza Diplomasia ya Michezo na kusema anaamini Serikali ya China itaridhia ombi la Tanzania la kufundisha wanamichezo thelathini wa Kitanzania kwenye michezo mbalimbali kabla ya Mashindano ya Nchi za Jumuiya ya Madola katikati ya mwaka huu.

Mwishoni Mhe. Membe aliwaelezea Watanzania hao mchakato unaoendelea Tanzania wa kupitia Katiba na hoja kuu ya Wizara ya Mambo ya Nje inayowagusa Watanzania wengi waishio ughaibuni ya Uraia wa Nchi Mbili.

Kesho Mhe. Membe na Ujumbe wake wanatazamia kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa China, Mawaziri wa Mambo ya Nje,  Biashara na Naibu Waziri wa Usalama kabla ya kuendelea na ziara yake kwneye Jimbo la Shenzhen na Guangzhou.

Kwenye ziara hii, Mhe. Membe ameongozana na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Nakuala Senzia Mkurugenzi  Kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania, Bi. Mindi Kasiga Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na maafisa waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje.


Meya wa Mji wa Vallejo wa Marekani awasili nchini

Meya wa Mji wa Vallejo nchini Marekani, Mhe. Osby Davis (kushoto) akisalimiana na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mhe. Didas Masaburi mara baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi. Mji wa Vallejo una uhusiano wa udada na Mji wa Bagamoyo
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu akisalimiana na mmoja wa wajumbe waliofuatana na Meya Davis kutoka Vallejo nchini Marekani.
Meya Davis na ujumbe wake wakimsikiliza Balozi Msechu wakati  akifafanua jambo kwao huku Mhe. Masaburi nae akisikiliza.
Mhe. Masaburi akiwapatia maelezo Mhe. Davis na ujumbe wake.

Sunday, February 23, 2014

MHE. MEMBE ZIARANI NCHINI CHINA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) atafanya ziara ya kikazi ya siku tano katika Jamhuri ya Watu wa China kuanzia tarehe 24 hadi 28 Februari, 2014. Ziara ya Mhe. Membe inakuja kufuatia mwaliko kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Wang Yi.

Mhe. Membe anafanya ziara hiyo nchini China kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kirafiki uliopo kati ya Tanzania na China. Wakati wa ziara hiyo, Mhe. Membe atafuatana na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Ziara hii pia ni muendelezo wa maeneo ya utekelezaji baada ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping aliyoifanya hapa nchini tarehe 24 na 25 Machi, 2013 na baadaye ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda nchini China mwezi Oktoba, 2013.

Akiwa nchini China, Mhe. Membe atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Mhe. Wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa China tarehe 25 Februari 2014. Siku hiyo hiyo Mhe. Membe atamtembelea Makamu wa Rais wa China, Mhe. Li Yuanchao kwa lengo la kumsalimia na baadaye atafanya mazungumzo rasmi na Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Gao Hucheng.

Aidha, tarehe 26 Februari, 2014 Mhe. Membe atatembelea Makao Makuu ya Kampuni ya Poly Technologies yaliyopo katika mji wa Shenzhen na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa  na Kampuni hiyo kabla ya kutembelea Makao Makuu ya Kampuni ya China Merchant Holdings International ambako atapokea taarifa ya maandalizi ya kuanza kwa mradi wa Ujenzi wa Bandari katika eneo la Mbegani huko Bagamoyo.

Mhe. Membe pia atapata fursa ya kutembelea Kampuni ya HUAWEI ili kujionea shughuli mbalimbali. Kampuni ya HUAWEI ina Mkataba na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya hapa nchini kuhusu Elimu kwa Njia ya Mtandao (e-Education) kwa Shule za Sekondari.

Vile vile tarehe 27 Februari, 2014, Mhe. Membe atautembelea Mji maarufu wa biashara wa Guangzhou na kukutana na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi mjini hapo. Mhe. Membe atatoa taarifa kuhusu hali ya uchumi, siasa na masuala ya jamii yalivyo hapa nchini kwa sasa pamoja na  kutoa taarifa ya maendeleo ya Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba.

Waziri Membe pia atatembelea Eneo la Viwanda la Huadu tarehe 28 Februari, 2014 kabla ya kurejea nchini tarehe 1 Machi, 2014.

IMETOLEWA NA: KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM.

24 FEBRUARI, 2014