Monday, June 22, 2015

Katibu Mkuu Kiongozi atembelea Banda la Mambo ya Nje kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kwenye Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Habu Mkwizu.
Balozi Sefue akisaini Kitabu cha Wageni katika Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Balozi Sefue akisoma Kitabu cha Sera ya Mambo ya Nje huku akisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Yahya.
Katibu Mkuu Kiongozi,  Balozi Sefue (katikati), Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya (kushoto) wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Manejimenti ya Utumishi wa Umma,  Bw. Habu Mkwizu alipokuwa akiwaelezea jambo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Taasisi zake wakifurahia jambo na Naibu Katibu Mkuu mara baada ya Katibu Mkuu Kiongozi  kutembelea Banda la Mambo ya Nje.

Juu na Chini ni Balozi Yahya akihojiwa na Mwandishi wa Habari kutoka TBC kuhusu mafanikio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mkufunzi kutoka Chuo cha Diplomasia Bw. Ally Masabo naye akihojiwa na Mwandishi wa TBC
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Batholomeo Jungu akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliojitokeza kutembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje wakati wa Maonesho ya Utumishi wa Umma.  
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Glory Mboya akisaini Kitabu katika Banda la Maonyesho la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililopo katika maonyesho Utumishi wa Umma Jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya akitizama mfano wa Majengo yanayojengwa katika Banda la Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolijia.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa tatu kulia), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Simba Yahya (wa nne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Wizarani na Taasisi zake. 
Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Wizara na Taasisi zake.

Picha na Reginald Philip

Rais Kikwete aongea na Watanzania wanaoishi India

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Watanznia wanaoishi India katika Hotel ya Taj Palace jijini Delhi. Rais Kikwete aliwaeleza mambo ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya nne ikiwemo ujenzi wa miundombinu kama vile barabara, maji, umeme na uboreshaji wa bandari ya Dar es Salaam. Aidha, aliwambia mipango iliyopo ya kujenga bandari ya Bagamoyo na reli ya kati ya kisasa. Aliwaeleza pia hali ya kisiasa, hususan maandalizi ya uchguzi mkuu ambapo zoezi la kuchukua fomu za kuwania nafasi ya Rais linaendelea.

Baadhi ya Watanzania waliohudhuria mkutano wa Rais Kikwete

Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe (Mb) kulia na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) nao waliongozana na Rais Kikwete katika mkutano na Watanzania.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekzaji Tanzania (TIC), Bi. Juliet Kairuki akitoa ufafanuzi wa masuala ya uwekezaji kwa Watanzania wanaoishi India.

Dada wa Kitanzania ambaye kwa sasa ni mwanafunzi wa Shahada ya Uzamili ya masuala ya Teknolojia ya Kilimo nchini India akimuuliza swali Rais Kikwete. Dada huyo alitaka kujua Serikali imejipngaje kuhakikisha kuwa mazao yanayolimwa nchini Tanzania yanasindikwa kabla ya kusafirishwa nje ya nchi. Rais Kikwete alieleza kuwa katika awamu ya pili ya mpango wa maendeleo wa mwaka 2025 ambao unaanza kutekelezwa mwaka 2015/2016 unalenga maendeleo ya viwanda. 

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini India.
Rais Kikwete (kushoto) akiwa pamoja na Balozi wa Tanzania nchini India, Me. Mhandisi John Kijazi


Mama Salma Kikwete (katikati) akiwa na baadhi ya Watanzania wanawake wanaoishi India.

 

Saturday, June 20, 2015

Ifanyeni Tanzania kuwa chaguo la kwanza katika uwekezaji, Rais Kikwete


Rais wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa katika mazungumzo na Wakuu wa Makampuni makubwa ya India hawapo pichani. Aliwahimiza kuchangamkia fursa za uwekezaji nchini Tanzania. kushoto kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda (Mb) na kulia ni kiongozi wa Chama cha Wafanyabiashara nchini India. Mazungumzo hayo yakifanyika katika Hoteli ya Taj Palace jijini Delhi 

Wakuu wa Makampuni Makubwa ya India wakimsikiliza Rais Kikwete. Baadhi ya Makampuni hayo tayari yalishawekeza nchini Tanzania na Makampuni mengine yalionesha dhamira ya kuja kuwekeza.

Mkurugenzi Mkuu  wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bi. Juliet Kairuki akiteta jambo na Mhe. Rais kabla ya mazungumzo na Wakuu wa Makampuni ya India.

Kiongozi wa Chama cha Wafanyabiashara wa India akimkabidhi, Mhe. Rais zawadi.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda (Mb) kulia akizungumza jambo na mmoja wa Wakuu wa Makampuni ya India. Mwingine kushoto ni Waziri wa Maji, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (Mb). 

Afisa Dawati wa India katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Emmanuel Luangisa akisalimiana na mmoja wa viongozi wa TIC kabla ya kuanza mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Wakuu wa Makampuni.
Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Nathaniel Kaaya  naye akiwa katika kubadilishana mawazo na wawakiishi wa India

Mikutano ya Rais Kikwete na baadhi ya Wakuu wa Makampuni
 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, knlia akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya IFLS inayojishughulisha na uwekezaji katika miundombinu na huduma za kifedha. Rais aliiomba kampuni hiyo iangalie uwezekno wa kuja kuwekeza nchini Tanzania, hususan katika ujenzi wa barabara na miundombinu ya  maji kwa kutumia mfumo wa PPP. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa tatu kutoka kushoto akiwa katika mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Hospitali za Apollo aliyenyoosha mikono. Mtendaji huyo alieleza kuwa taratibu zipo katika hatua za mwisho ili hospitali hiyo ifungue zahanati ya kwanza nchini Tanzania katika miezi miwili ijayo.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa tatu kushoto akiwa katika mazungumzo na Mkurugeenzi Mwendeshaji na Mwenyekiti wa Shirika la Ndege la India. Mhe. Rais aliliomba shirika hilo lirudishe safari za kuja Tanzania jambo ambalo walikubaliana nalo.
Rais Kikwete akiwa pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya ICICI. Rais Kikwete aliiomba benki hiyo ije kuwekeza Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Posta. Benki ya ICICI ina mtaji unaozidi Dola bilioni 100 imesambaa nchi nzima ya India hadi vijijini.



Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mara ya kwanza na Watumishi wote wa Wizara


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Libarata Mulamula akizungumza katika kikao chake cha kwanza na Watumishi wote wa Wizara tangu alipoteuliwa na Rais hivi karibuni kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Mkutano huo ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini  Dar es Salaam tarehe 20 Juni, 2015. Pamoja na mambo mengine Balozi Mulamula aliwahimiza Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje kufanya kazi kwa bidii, kuwa  na utii, nidhamu pamoja na unyenyekevu ili kufikia malengo katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.
Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Watumishi wa  Wizara wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani)
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje  wakimsikiliza Balozi Mulamula (Hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya Watumishi wa Mambo ya Nje wakimsikiliza Balozi Mulamula


Juu na Chini ni baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika kikao na Balozi Mulamula

Baadhi ya Watumishi wakichangia hoja wakati wa mkutano kati yao na Katibu Mkuu, Balozi Mulamula ambaye hayupo pichani


Mkutano ukiendelea 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya nae akizungumza machache mbele ya Watumishi wakati wa mkutano huo 
Balozi Mulamula kwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya wakishangilia  kwa furaha  wakati walipokutana na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Watumishi wa Wizara wakiwashangilia Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakati wa mkutano pamoja nao.

Picha na Reginald Philip





Friday, June 19, 2015

Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Msumbiji nchini

Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Msumbiji nchini, Mhe. Vicente Veloso  alipofika Wizarani kwa ajili ya kuzungumza na  Balozi Mulamula kuhusu namna bora ya kuiamarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Msumbiji  na pia kumpongeza kwa kuteuliwa na Rais kuwa Katibu Mkuu.
Mkutano ukiendelea huku wajumbe kutoka pande zote mbili wakisikiliza kwa makini. Wa pili kulia ni Bi. Zuhura Bundala, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bi. Talha Mohammed (kulia), Afisa Mambo ya Nje.

India yaipa Tanzania mkopo wa Dola Mil. 268 kwa ajili ya mradi wa maji katika miji ya Tabora, Igunga, Sikonge na Nzega

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa ameshikilia cheti kwa pamoja na Mwenyekiti wa Makampuni ya Kamal, Bw. Gagan Gupta. Bw. Gupta ni mfanyabiashara kutoka India ambaye amewekeza nchini Tanzania alikabidhiwa cheti cha kutambua mchango wake katika kukuza uchumi wa Tanzania. Cheti hicho alikabidhiwa siku ya Alhamisi jijini Delhi.



Na Ally Kondo, Delhi

Serikari za Tanzania na India zimewekeana saini Hati za Makubaliano kwa ajili ya kushirikiana katika kuendeleza sekta za maji, utalii, usafiri na usalama wa bahari pamoja na Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki.  Uwekaji saini wa hati hizo umefanyika jijini Delhi siku ya Ijumaa na kushuhudiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi. Rais Kikwete yupo nchini India kwa ziara ya kitaifa ya siku nne aliyoianza tarehe 17 Juni 2015.

Kwa mujibu wa Makubaliano katika Sekta ya Maji, Serikali ya India itatoa mkopo wa masharti nafuu wa Dola za Marekani milioni 268.35 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya mradi wa maji katika miji ya Tabora, Igunga, Nzega na Sikonge pamoja na  vijiji vitakavyopitiwa na bomba kubwa la maji litakalojengwa kutoka Ziwa Victoria.

Mradi huo utakaojengwa kwa miaka miwili na nusu na kampuni kutoka India utaanza Mwaka ujao wa Fedha 2015/16 na unatokana na ahadi ya Rais Kikwete aliyoitoa kwa wananchi wa maeneo hayo wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Kujengwa kwa mradi huo, itakuwa faraja kubwa kwa watu wanaoishi maeneo hayo ambayo kwa Tanzania yanakabiliwa na ukame na kupata mvua chache kwa mwaka ukilinganisha na maeneo mengine ya nchi. Watu takribani milioni 1.5 watafaidika na mradi huo utakapokamilika.

Mradi huo utakapokamilika utawaondolea wananchi adha ya kutembea mwendo mrefu kwa ajili ya kutafuta maji na badala yake watatumia muda mwingi kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali. Aidha, utawapa fursa watoto wa kike kujishughulisha na masomo pamoja na kutoa huduma za maji katika zahanati, vituo vya afya na mashuleni.


Kwa upande wa Makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya utalii, inatarajiwa kuwa makubaliano hayo yatasaidia kuongeza idadi ya watalii kutoka India kuja Tanzania. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhandisi John Kijazi, India kila mwaka inatoa watalii milioni 128 kwenda nchi mbalimbali duniani, lakini kati ya hao ni watalii 27,000 tu, ndio wanakuja Tanzania.

Makubaliano yaliyosainiwa kwa ajili ya Chuo cha Takwimu, utakiondolea chuo hicho na uhaba wa wakufunzi na mzigo wa kugharamia wakufunzi kutoka India kwa kuwa, kuanzia sasa India itakuwa ikipeleka wakufunzi kwenye chuo hicho kwa  gharama zao.