Saturday, June 20, 2015

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mara ya kwanza na Watumishi wote wa Wizara


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Libarata Mulamula akizungumza katika kikao chake cha kwanza na Watumishi wote wa Wizara tangu alipoteuliwa na Rais hivi karibuni kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Mkutano huo ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini  Dar es Salaam tarehe 20 Juni, 2015. Pamoja na mambo mengine Balozi Mulamula aliwahimiza Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje kufanya kazi kwa bidii, kuwa  na utii, nidhamu pamoja na unyenyekevu ili kufikia malengo katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.
Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Watumishi wa  Wizara wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani)
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje  wakimsikiliza Balozi Mulamula (Hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya Watumishi wa Mambo ya Nje wakimsikiliza Balozi Mulamula


Juu na Chini ni baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika kikao na Balozi Mulamula

Baadhi ya Watumishi wakichangia hoja wakati wa mkutano kati yao na Katibu Mkuu, Balozi Mulamula ambaye hayupo pichani


Mkutano ukiendelea 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya nae akizungumza machache mbele ya Watumishi wakati wa mkutano huo 
Balozi Mulamula kwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya wakishangilia  kwa furaha  wakati walipokutana na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Watumishi wa Wizara wakiwashangilia Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakati wa mkutano pamoja nao.

Picha na Reginald Philip





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.