Friday, June 19, 2015

Banda la Wizara ya Mambo ya Nje lazidi kung'ara kwenye maonesho ya Utumishi wa Umma

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Mkumbwa Ally akizungumzia ushiriki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye maonyesho ya ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam
Afisa Mwandamizi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mashaka Chikoli akielezea utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje  na mafanikio ya Wizara  kwa  Mtayarishaji wa Vipindi vya Televisheni, Bw. Paschal Mayala.
Mkufunzi wa Chuo cha Diplomasia, Bw. Ali Masabo akielezea Kozi mbalimbali zinazotolewa na Chuo hicho ikiwemo kozi mpya ya Shahada ya Mahusiano ya Kimataifa na Diplomasia wakati akihojiwa na Bw. Mayala
Afisa kutoka Taasisi iliyo chini ya Wizara  ya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC)  Bw. Rodney T. Mbuya naye akielezea ushiriki wa Taaisisi hiyo katika maonyesho ya Utumishi wa Umma
Mmoja wa Wananchi akisoma na kutazama picha za Mawaziri wa Mambo ya Nje tangu uhuru hadi sasa katika kitabu kilichomvutia kilichokuwa kinatolewa katika banda la maonyesho la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatiafa
Bw. Mayala akimhoji mwananchi aliyemkuta akisoma Kitabu cha Sera ya Mambo ya Nje na kuimwagia sifa Wizara ya Mambo ya Nje kwa juhudi zake katika kutekeleza Sera hiyo.  Wanaoshuhudia ni Bw. Khatibu Makenga, Afisa Mambo ya Nje na Rodney Mbuya  wa AICC. 
Wananchi wakiendela kupata maelezo juu ya majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na jinsi gani Wizara inatekeleza Diplomasia ya Uchumi 
Maafisa wakiwa akitika picha ya pamoja katika banda lao


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.