Tuesday, June 9, 2015

Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Ujumbe wa EU hapa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Kiongozi wa Ujumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) hapa nchini, Balozi Filberto Cerian Sebregondi alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Jumuiya  hiyo na Tanzania na pia kujitambulisha kwa Balozi Mulamula ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje. 
Maafisa Mambo ya Nje Waandamizi wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Sebregondi (hawapo pichani).
Balozi wa Uingereza hapa nchini Mhe. Diana Melrose kwa pamoja na Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe Adam Koeler na Maaafisa wengine  kutoka nchi za EU  wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Sebregondi.
Balozi Mulamula na Balozi  Sebregondi wakimsikiliza Balozi Melrose akifafanua jambo
Kikao kikiendelea

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.