Monday, June 22, 2015

Katibu Mkuu Kiongozi atembelea Banda la Mambo ya Nje kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kwenye Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Habu Mkwizu.
Balozi Sefue akisaini Kitabu cha Wageni katika Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Balozi Sefue akisoma Kitabu cha Sera ya Mambo ya Nje huku akisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Yahya.
Katibu Mkuu Kiongozi,  Balozi Sefue (katikati), Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya (kushoto) wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Manejimenti ya Utumishi wa Umma,  Bw. Habu Mkwizu alipokuwa akiwaelezea jambo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Taasisi zake wakifurahia jambo na Naibu Katibu Mkuu mara baada ya Katibu Mkuu Kiongozi  kutembelea Banda la Mambo ya Nje.

Juu na Chini ni Balozi Yahya akihojiwa na Mwandishi wa Habari kutoka TBC kuhusu mafanikio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mkufunzi kutoka Chuo cha Diplomasia Bw. Ally Masabo naye akihojiwa na Mwandishi wa TBC
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Batholomeo Jungu akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliojitokeza kutembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje wakati wa Maonesho ya Utumishi wa Umma.  
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Glory Mboya akisaini Kitabu katika Banda la Maonyesho la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililopo katika maonyesho Utumishi wa Umma Jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya akitizama mfano wa Majengo yanayojengwa katika Banda la Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolijia.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa tatu kulia), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Simba Yahya (wa nne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Wizarani na Taasisi zake. 
Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Wizara na Taasisi zake.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.