Saturday, June 20, 2015

Ifanyeni Tanzania kuwa chaguo la kwanza katika uwekezaji, Rais Kikwete


Rais wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa katika mazungumzo na Wakuu wa Makampuni makubwa ya India hawapo pichani. Aliwahimiza kuchangamkia fursa za uwekezaji nchini Tanzania. kushoto kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda (Mb) na kulia ni kiongozi wa Chama cha Wafanyabiashara nchini India. Mazungumzo hayo yakifanyika katika Hoteli ya Taj Palace jijini Delhi 

Wakuu wa Makampuni Makubwa ya India wakimsikiliza Rais Kikwete. Baadhi ya Makampuni hayo tayari yalishawekeza nchini Tanzania na Makampuni mengine yalionesha dhamira ya kuja kuwekeza.

Mkurugenzi Mkuu  wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bi. Juliet Kairuki akiteta jambo na Mhe. Rais kabla ya mazungumzo na Wakuu wa Makampuni ya India.

Kiongozi wa Chama cha Wafanyabiashara wa India akimkabidhi, Mhe. Rais zawadi.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda (Mb) kulia akizungumza jambo na mmoja wa Wakuu wa Makampuni ya India. Mwingine kushoto ni Waziri wa Maji, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (Mb). 

Afisa Dawati wa India katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Emmanuel Luangisa akisalimiana na mmoja wa viongozi wa TIC kabla ya kuanza mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Wakuu wa Makampuni.
Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Nathaniel Kaaya  naye akiwa katika kubadilishana mawazo na wawakiishi wa India

Mikutano ya Rais Kikwete na baadhi ya Wakuu wa Makampuni
 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, knlia akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya IFLS inayojishughulisha na uwekezaji katika miundombinu na huduma za kifedha. Rais aliiomba kampuni hiyo iangalie uwezekno wa kuja kuwekeza nchini Tanzania, hususan katika ujenzi wa barabara na miundombinu ya  maji kwa kutumia mfumo wa PPP. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa tatu kutoka kushoto akiwa katika mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Hospitali za Apollo aliyenyoosha mikono. Mtendaji huyo alieleza kuwa taratibu zipo katika hatua za mwisho ili hospitali hiyo ifungue zahanati ya kwanza nchini Tanzania katika miezi miwili ijayo.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa tatu kushoto akiwa katika mazungumzo na Mkurugeenzi Mwendeshaji na Mwenyekiti wa Shirika la Ndege la India. Mhe. Rais aliliomba shirika hilo lirudishe safari za kuja Tanzania jambo ambalo walikubaliana nalo.
Rais Kikwete akiwa pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya ICICI. Rais Kikwete aliiomba benki hiyo ije kuwekeza Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Posta. Benki ya ICICI ina mtaji unaozidi Dola bilioni 100 imesambaa nchi nzima ya India hadi vijijini.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.