Tuesday, June 9, 2015

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Balozi Linda Thomas - Greenfield alipotembelea Wizarani na kufanya mazungumzo yaliyojikita katika kukuza mahusiano kati ya Tanzania na Marekani katika Sekta mbalimbali.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress pamoja na ujumbe ulioambatana na Mhe. Thomas - Greenfield nao wakifuatilia mazungumzo.
Balozi Linda akitoa ufafanuzi wa jambo huku Balozi Mulamula akimsikiliza kwa makini. 
Balozi Mulamula (katikati) akimsikiliza Mhe. Linda alipokuwa akizungumza naye kulia ni Afisa Mambo ya Nje Bwa. Lucas Mayenga. 
Mazungumzo yakiendelea
 Balozi Liberatta Mulamula akimlaki kwa furaha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Balozi Linda Thomas - Greenfield wakati alipowasili na kufanya mazungumzo yaliyojikita katika kukuza mahusiano kati ya Tanzania na Marekani katika Sekta mbalimbali.


Picha na Reginald Philip.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.