Wednesday, June 17, 2015

Katibu Mkuu Balozi Mulamula apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Qatar nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akipokea Nakala ya Hati za Utambulisho kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kutoka kwa Balozi Mteule wa Qatar nchini Tanzania,  Mhe. Abdullah Jassim Mohamed Al Maadadi leo tarehe 17 Juni 2015.
Balozi Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi Al Maadadi mara baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati (wa kwanza kulia) Bw. Elibariki Maleko na Afisa Mambo ya Nje Bwa. Batholomeo Jungu wakisikiliza kwa makini mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Balozi Mulamula na Balozi Mteule Mhe. Al Maadadi (hawapo pichani). 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.