Friday, June 19, 2015

Balozi Mulamula azungumza na Balozi wa Ufaransa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mhe. Malika Berak, alipokuja kujitambulisha na kumpongeza Balozi Mulamula kwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu. Pia walizungumzia masuala mbalimbali ya kimaendeleo na kukuza mahusiano ya kibiashara kati ya nchi hizi mbili
Katibu Mkuu Balozi Mulamula akimwonyesha Balozi Berak Kitabu kinachozungumzia maendeleo ya Mji wa Kilwa.
Afisa Mambo ya Nje, Bi. Felisita Rugambwa akinukuu mazungumzo  yaliyokuwa yakiendelea kati ya Balozi  Mulamula na Balozi Berak (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea.
Picha na Reginald Philip


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.