Thursday, June 16, 2016
Dkt. Possi asisitiza umuhimu wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu
Wednesday, June 15, 2016
Naibu Waziri Dkt. Possi ashiriki Mkutano wa Tisa wa nchi Wanachama wa Mkataba wa watu wenye Ulemavu
Katibu Mkuu Mambo ya Nje ashiriki Warsha ya Makatibu Wakuu
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz P. Mlima ( wa nne kutoka kulia
waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki Balozi Liberat Mfumukeko (wa nne kutoka kushoto), Makatibu Wakuu
kutoka Wizara zinazosimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na
wataalam kutoka Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Warsha (Retreat) ya Makatibu Wakuu inayoendelea
Mjini Moshi.
|
Monday, June 13, 2016
KATIBU MKUU AKIWA KWENYE SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO MAALUM YA JKT
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt Aziz P. Mlima akikagua gwaride liliondaliwa wakati wa sherehe za kufunga mafunzo maalum ya JKT kwaajili ya watumishi 30 walioajiriwa hivi karibuni. |
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo maalum ya JKT akitoa salaam maalum ya kijeshi kwa Katibu Mkuu Dkt. Aziz P. Mlima |
Katibu Mkuu Dkt Aziz P. Mlima akimpongeza mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri zaidi wakati wa mafunzo maalum ya JKT |
Waziri Mahiga amuaga rasmi Balozi wa Italia hapa nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb), akimkabidhi zawadi Balozi wa Italia aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini, Mhe. Luigi Scotto, katika hafla maalumu ya kumuaga iliyofanyika tarehe 10-06-2016, kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine
Mahiga (Mb), akimkabidhi zawadi Balozi wa Vatcan na mwakilishi wa Papa hapa nchini, Balozi Francisco Montecillo Padilla. Balozi Francisco alipewa zawadi hiyo kwenye hafla maalumu ya kumuaga Balozi wa Italia hapa nchini, iliyofanyika tarehe 10-06-2016, katika hoteli ya Serena jijini Dar es
Salaam.
Waziri Mahiga akifurahia jambo na Balozi Padilla na Balozi Scotto, mara tu baada ya kuwapa zawadi.
Saturday, June 11, 2016
Friday, June 10, 2016
Waziri Mahiga ashiriki maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari ya nchini Rwanda dhidi ya Watutsi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiongea na wageni waalikwa (hawapo pichani) katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994, maadhimisho hayo yaliandaliwa na Ubalozi wa Rwanda nchini Tanzania na kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake alitoa wito kwa mataifa yote kuweka mbele suala la amani ili kuepuka kupoteza maisha ya wananchi wasio na hatia ambao ni nguvu kazi ya Taifa katika kujiletea maendeleo. |
Naibu Waziri Kigwangalla ashiriki Mkutano wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla ( Mb) akizungumza kwa niaba ya
serikali kuhusu mafanikio na changamoto ambazo serikali imekuwa
ikikabiliana nazo dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI katika Mkutano wa ngazi ya juu wa
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI unaoendelea Umoja wa
Mataifa New York-Marekani. |
Waziri Mahiga ampokea Mjumbe Maalum kutoka Eritrea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Eritrea, Mhe. Isaias Afwerki kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Ujumbe huo uliwasilishwa na Mjumbe Maalum ambaye pia ni Balozi wa Eritrea nchini mwenye makazi Nairobi, Kenya, Mhe. Beyene Russom Habtai. |
Subscribe to:
Posts (Atom)