Tuesday, July 26, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje awa mgeni rasmi siku ya Taifa la Misri

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akitoa hotuba kama mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Taifa la Misri yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katika hotuba yake Mhe. Dkt. Kolimba alisifu ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Misri na kuahidi kuendelea kuuimarisha kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa mataifa haya.

Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini wakimsikiliza Mhe. Dkt. Kolimba (hayupo kwenye picha) kwenye maadhimisho ya siku ya Taifa la Misri
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Suzan Kolimba akitakiana afya njema na Balozi wa Misri nchini, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf wakati wa maadhimisho ya Taifa la Misri yaliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya wageni waalikwa akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Balozi Simba Yahya (wa tatu kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (wa pili kushoto), Msaidizi wa Naibu Waziri, Bw. Adam Isara (kushoto)  na Maafisa wa Ubalozi wa Misri (k
Sehemu ya Wageni waalikwa


   

Balozi wa Misri nchini pamoja na mkewe wakimkaribisha Rais Mstaafu, Mhe. Ali Hassan Mwinyi kwenye maadhimisho ya Taifa la Misri
Meza kuu wakifurahia burudani kutoka kwa mtumbuizaji ambaye ni raia wa Misri anayeishi hapa nchini
Picha ya pamoja
Maafisa wa Ubalozi wa Misri wakiagana na Mhe. Mwinyi
Mhe. Dkt. Susan akiagana na Balozi wa Misri mara baada ya maadhimisho ya Taifa hilo
Balozi Yahya na Balozi Shelukindo wakiwa na mmoja wa wageni waalikwa
Picha ya pamoja

Friday, July 22, 2016

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje akutana na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa China nchini


Msemaji na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa China nchini,  Bw. Zhang Biao alipomtembelea leo katika Ofisi za Wizara.  Katika mazungumzo yao walizungumzia namna ya kuendelea kushirikiana hususan katika   kuhakikisha Sera za Mambo ya Nje za Tanzania na China zinajulikana kitaifa na kimataifa kwa kuimarisha tasnia ya Mawasiliano kwa Umma.
Maafisa wa Ubalozi wa China nchini waliofatana na Bw. Zhang Biao wakifuatilia mazungumzo. Kutoka kushoto ni  Bi. Sun Lihua na Mkurugenzi wa Diplomasia na Habari Bw. Xu Jingchun.
Picha ya pamoja.

Thursday, July 21, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Iran nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Iran nchini Mhe. Mehdi Agha Jafari alipomtembelea leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika Mazungumzo yao Mhe. Waziri alimweleza  Balozi huyo kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano na Iran  hususan katika kuhakikisha Diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo inaimarika kwa manufaa ya mataifa hayo. 
Mhe. Balozi Mehdi Agha Jafari akizungumza ambapo alieleza kuwa Serikali ya Iran itazidi kushirikiana na Tanzania katika sekta za Elimu, Biashara, Afya na Kilimo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdallah Kilima (kushoto) pamoja na Msaidizi wa Waziri, Bw. Adolf Mchemwa wakifuatilia kwa makini mazungumzo.
Mhe. Balozi Mehdi Agha Jafari akimkabidhi ujumbe maalum Mhe. Waziri Mahiga 
Mazungumzo yakiendelea

Ubalozi wa Kuwait nchini wakabidhi vitendea kazi kwa Chuo cha Diplomasia


Balozi wa Kuwait nchini, Mhe. Jasem Al-Najem akimkabidhi vitendea kazi zikiwemo Kompyuta kwa Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia (CFR), Dkt. Bernard Achiula. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi za Chuo hicho zilizopo eneo la Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi(wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Mhe. Balozi Abdallah Kilima wakiwa pamoja na Mhe. Jasem Al-Najem na Dkt. Achiula ambao waliiwakilisha Wizara katika makabidhiano hayo.
Balozi Mwinyi akiongea na Mhe. Jasem Al-Najem ambapo katika mazungumzo yao walizungumzia namna ya kuimarisha uhusiano uliodumu kwa muada mrefu baina ya mataifa ya Tanzania na Kuwait na alimshukuru kwa kukisaidia chuo hicho ambacho kipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kumwomba kupanua wigo katika sekta ya Elimu ikiwemo kuwa na program za mafunzo na kubadilishana uzoefu baina y anchi hizi mbili.
Balozi Abdallah Kilima (kushoto) akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Balozi Nasem Al-Najem na kueleza namna ambavyo Wizara imejidhatiti katika kuhakikisha inasimamia masuala yote ya Kidiplomasia na ushirikiano.
Mkurugenzi wa Taaluma katika Chuo cha Diplomasia, Dkt. Wetengere Kitojo akifafanua jambo wakati ujumbe huo ulipotembelea Maktaba ya Chuo. Wa pili kutoka kulia ni Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mhe. Balozi Jasem Al-Najem akiendelea kutembelea madarasa na huduma nyingine za wanafunzi katika chuo hicho.
Mhe. Balozi akisalimiana na Wanafunzi wa waliokuwa wakifundishwa somo la lugha ya Kiarabu
Balozi Mwinyi akifafanua jambo kwa Mhe. Al-Najem wakati wakitembelea maeneo ya Chuo hicho.
Dkt.Achiula akikabidhi zawadi ya kinyago kwa Mhe. Balozi Al-Najem ambapo pia alitumia fursa hiyo kumshukuru kwa msaada alioukabidhi kwa Chuo hicho.
Mhe. Balozi Al-Najem akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Diplomasia.

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Balozi wa China nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Dkt. Lu Youqing alipofika Wizarani kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China. Katika mazungumzo yao walijadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano hususan katika masuala ya kukuza uchumi  kupitia viwanda na uwekezaji na kuendelea kukamilisha miradi mbalimbali ya pamoja ikiwemo ule wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Mkoani Pwani.
Sehemu ya Ujumbe kutoka Ubalozi wa China.
Balozi nae akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Katibu Mkuu, Dkt. Mlima
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Christopher Mramba (kushoto) pamoja na Bw. Humphrey Shangarai, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Mlima na Balozi Lu (hawapo pichani)

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Balozi wa China nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Dkt. Lu Youqing alipofika Wizarani kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China. Katika mazungumzo yao walijadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano hususan katika masuala ya kukuza uchumi  kupitia viwanda na uwekezaji na kuendelea kukamilisha miradi mbalimbali ya pamoja ikiwemo ule wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Mkoani Pwani.
Sehemu ya Ujumbe kutoka Ubalozi wa China.
Balozi nae akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Katibu Mkuu, Dkt. Mlima
Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Christopher Mramba (kushoto) pamoja na Bw. Humphrey Shangarai, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Mlima na Balozi Lu (hawapo pichani)

KATIBU MKUU AKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA SHIRIKA LA TRADEMARK EAST AFRIKA

Mkurugenzi wa Shirika la TradeMark East Afrika (TMEA) Bw. John Ulanga (kushoto) akizungumza na Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (kulia) alipotembelea Wizarani leo. Bw. John Ulanga amechukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika hilo Dkt. Josaphat Kweka baada ya kumaliza mkataba wake wa kulitumikia shirika. Katika mazungumzo hayo Mkurugenzi mpya wa shikirika la TradeMark East Afrika Bw. John Ulanga  aliahidi kudumisha na kukuza ushirikiano na serikali katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo Nchini.
Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (wa pili kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi mpya wa Shirika la TradeMark East Afrika Bw. John Ulanga (kushoto). Wengine ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. Osward Kyamani (kulia) na Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule (wapili kulia)
Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la TradeMark East Afrika wakiendelea na mazungumzo. Tokea kushoto ni Afisa Uchumi kutoka Wizarani na Mratibu wa maratibu wa mradi wa TMEA  Bi. Joyce (wakwanza kushoto) Kimei na Afisa kutoka TMEA Bi. Monika Hangi (wapili kushoto)
Mkurugenzi wa TMEA Bw. John Ulanga akielezea jambo kwa Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima

Wednesday, July 20, 2016

Waziri Mahiga asaini Mkataba wa Uenyeji wa Benki ya Afrika Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bi. Vivienne Yeda wakisaini Mkataba wa Uenyeji (Host Agreement) wa Ofisi za  Benki hiyo nchini. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki tarehe 20 Julai, 2016.
Waziri Mahiga na Bi. Yeda wakibadilishana Mkataba mara baada ya kuusaini.
Dkt. Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Bi. Yeda, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Baraka Luvanda  (kulia) na Mkuu wa Biashara wa EADB hapa nchini Bi. Juliana Sweke (kushoto).


Picha na Reginald Philip 

Waziri Mahiga asaini Mkataba wa uenyeji wa Benki ya EADB

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) amesaini Mkataba wa uenyeji (Host Agreement) wa Ofisi za Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB) na Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo Bi. Vivienne Yeda. Mkataba huo umesainiwa leo katika Ofisi za Wizara  kwa lengo la kurasimisha kisheria Ofisi za Benki hiyo zilizopo nchini.

Aidha, uwekaji saini wa mkataba huo ni utekelezaji wa agizo la Mkutano wa Wakuu wa Nchi  Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  uliofanyika tarehe 2 Machi, 2016  Mjini Arusha -Tanzania. Mkutano huo pamoja na mambo mengine uliazimia kuanzishwa kwa Ofisi za Benki hiyo katika Makao Makuu ya kila nchi Mwanachama ili kuwezesha utekelezaji madhubuti wa shughuli za Benki hiyo. 

Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki ni Taasisi ya Fedha iliyoanzishwa mwaka 1967 chini ya iliyokuwa  Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa lengo la kutoa misaada ya kifedha na misaada mingine  ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

EADB ilianzishwa wakati iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa na wanachama watatu ambao ni Tanzania, Kenya na Uganda.  Rwanda ilijiunga na Benki hiyo  mwaka 2007 na kufanya nchi wananchama waliojiunga kufikia wanne.

Kwa upande wa Tanzania, EADB imeisaidia kutoa mikopo mbalimbali katika miradi ya maendeleo kupitia Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB). Pia, katika kulipa kipaumbele suala la Afya, Benki hiyo  imeweka mpango wa kusaidia afya ya uzazi kwa akinamama hususan,  katika maeneo ya vijijini.

Miradi mingine inayofadhiliwa na EADB hapa nchini ni pamoja na miradi ya Umeme hasa kwa maeneo ya vijijini, na miradi ya maji na usafi wa mazingira.

Akiongea katika hafla hiyo,  Mhe. Waziri Mahiga aliahidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu katika kuhakikisha uendeshaji wa Benki hiyo unafanikiwa. “Karibuni sana na pale inapotokea  mmekwama katika jambo lolote linalohitaji usaidizi wa Serikali au ushauri tupo tayari kutoa ushirikiano” alisema Waziri Mahiga.

Waziri Mahiga azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mkutano wa AU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema leo mchana kuhusu Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika uliomalizika hivi karibuni nchini Rwanda. Katika mkutano huo Mhe. Waziri alielezea mambo mbalimbali yaliyojadiliwa katika Mkutano huo ikiwemo suala zima la Haki za Wanawake katika kufanya maamuzi, kupata nafasi za Uongozi na kushirikishwa kwenye utatuzi wa migogoro mbalimbali Barani Afrika. Kaulimbiu ya mkutano huo ilihusu "Haki za binadamu hususan za Wanawake".  Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizarani, Bi. Mindi Kasiga.
Dkt. Mahiga akionyesha kwa waandishi wa habari Hati yake ya Kusafiria (passport) aliyopatiwa wakati wa mkutano wa AU. Hati hiyo imeanzishwa na Umoja wa Afrika kwa lengo la kuimarisha umoja na kurahisisha mawasiliano. Kulia  ni Bi. Kasiga.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri Mahiga kwenye mkutano uliowakutanisha naye.


Picha na Reginald Philip

Tuesday, July 19, 2016

Taasisi ya Aga Khan kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi ya maendeleo

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa masuala ya Kidiplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani alipotembelea Wizarani kwa ajili ya kujitambulisha na kueleza nia ya Taasisi hiyo ya kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika miradi ya maendeleo hususan katika sekta ya elimu na afya.
Sehemu ya wageni walioambatana na Balozi Lalani (hayupo pichani). Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Aga Khan nchini, Bw. Amin Kurji nao wakisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Muombwa na Balozi Lalani (hawapo pichani).
Balozi Lalani naye akizungumza na Balozi Mwinyi  alipotembelea Wizarani.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Ramla Khamis (kushoto), pamoja na Afisa Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Hellen Mgeta wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Mwinyi akiagana na  Balozi Lalani na Bw. Kurji  mara baada ya kumaliza mazungumzo.