Friday, November 18, 2016

Waziri Mahiga asaini Mkataba na Serikali ya China


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China  nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Lu Youqing wakisaini Mkataba wa Makubaliano ya uwekwaji wa samani katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Tukio hili limefanyika mapema leo Wizarani Jijini Dar es Salaam


Mazungumzo yakiendelea kabla ya kusaini mkataba

Mhe. Waziri Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Dkt. Youqing walipokutana Wizarani Jijini Dar es Salaam

Thursday, November 17, 2016

WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA MABALOZI



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
 

Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 



            20 KIVUKONI FRONT,
            P.O. BOX 9000,
                  11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb), amepokea Nakala za Hati za Utambulisho za Waheshimiwa Mabalozi Wateule wa Nchi za Yemen na Saudi Arabia na baadaye kufanya mazungumzo na Waheshimiwa Mabalozi wa  Malawi na Japan leo ofisini kwake.

Wakati wa mazungumzo na Balozi Mteule wa Saudi Arabia, Mhe. Mohammed Mansour Al-Malik viongozi hao walisisitiza umuhimu wa Tanzania na Saudi Arabia kuimarisha uhusiano na ushirikiano hususan katika nyanja za biashara na uchumi. Dkt. Mahiga  alimweleza Balozi Mteule kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alifurahishwa na ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia, Mhe. Adel Al Jubair  aliyoifanya nchini mwezi Machi 2016. 

Wakati wa ziara hiyo, Rais Magufuli aliomba Serikali ya Saudi Arabia kupitia Mfuko wa Serikali (Saudi Fund) kufadhili ukamilishwaji wa miradi mbalimbali ya barabara hapa nchini. Ombi hilo liliafikiwa na ujumbe kutoka Saudi Arabia ulifanya ziara nchini hivi karibuni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Rais Magufuli pia alitumia fursa hiyo kumualika Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo  kutembelea Hifadhi za Taifa zilizopo hapa nchini. Mhe. Waziri alikubali isipokuwa alisema atakuja wakati mwingine na mwanae wa kiume ambaye anapenda sana kuona paka wakubwa akimaanisha wanyama wakubwa kama simba, chui, tembo na faru.

Kwa upande wake, Balozi Mteule wa Saudi Arabia aliahidi kusimamia utekelezaji wa yote yaliyoafikiwa wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi yake na masuala mengine yenye maslahi ya pande zote mbili.

Wakati wa mazungumzo na Balozi Mteule wa Yemen, Mhe.  Fikri Taleb Abubaker Al-Sakaf, wawili hao walisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili. Waziri Mahiga alitumia fursa hiyo pia kuwaalika wafanyabiashara wakubwa kutoka Yemen kuja kuwekeza Tanzania. Alisema kuna wafanyabiashara wengi wenye asili ya Yemen wamefanikiwa kibiashara hapa nchini.

Aliongeza kuwa historia inaonesha kwamba watu kutoka Yemen ndio walikuwa wa kwanza kufanya biashara za maduka ya bidhaa muhimu nchini ambao walikuwa na utaratibu wa kukopesha bidhaa na kulipa baadaye. Alisema watu hao kutoka Yemen pia ndio walikuwa na utaratibu wa kupeleka bidhaa hadi vijijini na kukopesha wateja wao ambao leo unatumiwa na wafanyabiashara wa Tanzania kwa jina maarufu wamachinga.

Kwa upande wake, Balozi Mteule wa Yemen aliahidi kuwa atafanya kila awezalo kushawishi makampuni makubwa kutoka Yemen kuja kuwekeza nchini. Alisema kama watu wa Yemen walikuwa wanafanya biashara ndogo ndogo huko nyuma hapa nchini, kuna haja sasa ya kupanua wigo na kuingia katika biashara kubwa.

Wakati wa mazungumzo na Balozi wa Malawi, Mhe. Hawa Ndilowe, wawili hao walisisitiza pia umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili. Aidha, Mhe. Ndilowe alimweleza Waziri Mahiga kuwa Malawi imejipanga kuandaa mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi (JPC) mwezi Desemba 2016. Alieleza mara ya mwisho kufanyika mkutano huo ilikuwa mwaka 2003 nchini Tanzania, hivyo kuna umuhimu wa kuitisha mkutano huo ili kutoa fursa kwa wadau kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano pamoja na kutafuta mbinu za kukabiliana na changamoto zinazotukabili.

Waziri Mahiga alikaribisha uamuzi huo kwa furaha kwa kusema kuwa wakati wa mkutano huo itakuwa fursa nzuri ya kufafanua masuala mbalimbali ambayo yamefanyiwa mabadikiko na Serikali ya Awamu ya Tano, hususan katika sekta ya usafirishaji katika Bandari ya Dar es Salaam, mifuno ya ulipaji kodi, uhamiaji na biashara za mipakani.

Aliendelea kueleza kuwa Tanzania na Malawi zinatakiwa kushirikiana katika masuala ya ulinzi na usalama, hususan katika kukabiliana na mauaji ya watu wenye ualbino ambayo yameikumba nchi zao.

Katika mazungumzo yake na Balozi wa Japan hapa nchini, Mhe. Masaharu Yoshida, Waziri Mahiga alipongeza ushirikiano uliopo kati ya nchi hizi mbili ambao umejikita katika kuimarisha sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu hapa nchini kwa ajili ya maendeleo.

Aidha, akitoa maoni yake kuhusu Mkutano wa Sita wa Kimataifa kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo kati ya Japan na Afrika (TICAD VI)  uliofanyika kwa  mara ya kwanza Afrika, Jijini Nairobi mwezi Agosti, 2016, Waziri Mahiga alisema mikutano hiyo ni jukwaa muhimu linalotoa fursa kwa nchi za Afrika na Japan kujadili maendeleo. Pia alipongeza agenda zilizojadiliwa kwenye mkutano wa TICAD VI ikiwemo kuhamasisha mageuzi ya kiuchumi kupitia uendelezaji wa viwanda; Kuboresha sekta ya Afya kwa maisha bora na kusaidia jitihada za kudumisha amani na utulivu katika jamii kwa ajili ya maendeleo ya Afrika.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 17 Novemba, 2016.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Yemen nchini Mhe.Fikri Taleb Abubaker Al Sakaf mara baada ya kuwasili Wizarani kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akionesha Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Yemeni nchi Tanzania Mhe.Fikri Taleb Abubaker Al Sakaf mara baada ya kukabidhiwa 

aziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa  Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Mohammed Bin Mansoor Al Malyk alipowasili Wizarani Jijini Dar es Salaam  kukabidhi Nakala za Hati za Utambulisho
Balozi Mteule wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Mohammed Bin Mansoor Al Malyk  akikabidhi Nakala za Hati za Utambulisho kwa Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga Wizarani Jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Hawa Ndolowe alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam
Mzungumzo yakiendelea, Kushoto ni Balozi Msaidizi wa Malawi nchini Tanzania Bw.Sai Kaphale na Kulia ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yalikuwa yakiendelea.



Wakiwa katika picha ya pamoja

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Masaharu Yoshida alipomtembelea kwa mazungumzo yaliyofanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam

Mazungumzo yakiendelea. Kushoto ni Maafisa kutoka Ubalozi wa Japan nchini Tanzania na kulia ni Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea

Tuesday, November 15, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Algeria nchini Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Algeria nchini Tanzania Mhe. Saad Belabed katika mazungumzo yaliyofanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifanunua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Algeria nchini Tanzania Mhe. Saad Belabed. Kulia ni Afisa wa Wizara akifuatilia mazungumzo

Waziri Mahiga azungumza na Wadau wa Maendeleo kutoka nchi za Nordic na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwenye Mkutano na Wadau wa Maendeleo kutoka nchi za Nordic uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Nchi za Nordic zinatoa mchango mkubwa katika shughuli mbalimbali za maendeleo nchini ikiwemo kilimo na miradi ya maji. Nordic inaundwa na Nchi tano ambazo ni Norway, Finland, Iceland,Sweden na Denmark. 

Mkutano ukiendelea

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Bw.Alvaro Rodrigues  akizungumza wakati wa mkutano

Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Norway Bi. Sive Cathrine Moe akizigumza wakati wa mkutano

Baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia Mkutano.

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano

Waziri Mahiga akutana na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland, Mhe. Kai Mykkanen alipomtembelea kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Wawili hao wamezungumzia masuala mbalimbali kuhusu masuala ya biashara, uwekezaji na maendeleo ya huduma za kijamii nchini. Mhe. Kai katika mazungumzo hayo ameahidi kupitia Wizara yake ataendelea kushirikiana na Tanzania katika kuongeza kasi ya ukuaji wa shughuli za maendeleo sambamba na kuendelea kushawishi sekta binafsi za Finland kuja kuwekeza nchini.

Mhe. Waziri, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland  Mhe. Kai Mykkanen

Mazungumzo yakiendelea

Mhe. Waziri, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza  Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland  Mhe. Kai Mykkanen walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

Monday, November 14, 2016

Waziri Mahiga apokea hati ya utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Ubalozi mdogo wa Oman Zanzibar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Konseli Mkuu wa Ubalozi mdogo wa Oman, Zanzibar Mhe. Ahmed Hamood Al Habs alipowasili Wizarani Jijini Dar es Salaam kabla ya kukabidhi hati ya utambulisho 

Mhe. Wiziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Ubalozi mdogo wa Oman, Zanzibar Mhe. Ahmed Hamood Al Habs
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na  Konseli Mkuu wa Ubalozi wa mdogo wa Oman Zanzibar Mhe. Ahmed Hamood Al Habs mara baada ya kukabidhi hati ya utambulisho

Mazungumzo yakiendelea 

Wakiwa katika picha ya pamoja

Friday, November 11, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Zambia nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi. Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Zambia nchini, Mhe. Judith Kapijimpanga alimpomtembelea leo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao wamejadili masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili. Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa ni kuhusu kuboresha na kuimarisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inayoziunganisha Tanzania na Zambia, na masuala ya mazingira hasa kwa upande wa Ziwa  Tanganyika. 
Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Zambia nchini Mhe.Kapijimpanga walipokutana kwa mazungumzo Wizarani
Mkutano ukiendelea
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo (wa pili kulia) akifuatilia mazungumzo. Wa kwanza kulia  ni Afisa wa Wizara.
Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo

Thursday, November 10, 2016

Kaimu Katibu Mkuu Mambo ya Nje akutana na Mhariri Mtendaji wa TSN

Kaimu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akiongoza kikao alipokutuna na ujumbe kutoka Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Wizarani jijini Dar es Salaam

Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim J. Yonazi (kulia) akifuatilia mazungumzo wengine ni Mkuu wa kitengo cha Utafiti wa Kampuni hiyo Bi.Ichikael Maro na Afisa Biashara wa Wizara, Bw. Amadeus Mzee
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo (kushoto), na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasilano Serikalini,  Bi. Robi Bwiru wakifuatilia mazungumzo. Wengine Maafisa kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

UMOJA WA MATAIFA WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA

Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena, umeishukuru Serikali ya Tanzania kwa kusaidia kwa hali na mali ujenzi na hatimaye kuelekea ukamilishwaji wa Majengo mapya ambayo yatatumika kwa shughuli za iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) ambayo ilihitimisha majukumu yake mwaka jana.

Shukrani hizo zimetolewa siku ya jumatano na Bw.Theodor Meron, ambaye ni Rais wa Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia na Utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka zote muhimu za zilizokuwa Mahakama za Kimataifa zilizoshughulikia mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda na Yugoslavia ya zamani ( IRMCT).

Bw. Theodor Meron alikuwa akiwasilisha Ripoti yake ya Nne kuhusu IRMCT mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa . Ripoti ambayo imeanisha maendeleo ya kipindi cha mpito kutoka ICTR na ICTY kwenda IRMCT kazi ambayo amesema inakwenda vizuri ingawa kumekuwapo na changamoto kadhaa.

“Wakati ninapowasilisha ripoti hii, nichukue fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa mchango mkubwa na ushirikiano ambao tumeupata kutoka serikali ya Tanzania, takribani wiki tatu zijazo majengo hayo yatazinduliwa rasmi baada ya kuwa yamekamilika”. Akasema Bw. Meroe

Baadhi ya changamoto hizo kwa upande wa iliyokuwa ICTR ni pamoja na kutokamatwa hadi sasa kwa watuhumiwa watatu ambao inaelezwa wapo mafichoni. Ni pili ni mahali pa kuwapeleka watu ambao ama wamekwisha maliza kutumikia vifungo vyao na kuachiwa huru. Watu hao wamekosa nchi ya kuwapokea na hadi sasa bado wanaendelea kuishi nchini Tanzania.

Na kwa sababu hiyo, Rais wa IRMCT ametoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kutoa ushirikiano wa kuwachukua watu hao ambao hawana mahali pa kwenda na kwa wale walioko mafichoni nchi ambazo wamejificha watoe ushirikiano kwa kuwafichua na kuwakamata ili hatimaye sheria iweze kuchukua mkondo wake

Kwa upande wake, Tanzania kupitia Mwakilishi wake katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, amesema Tanzania inakaribia kuhitimishwa kwa ujenzi wa makazi mapya ya iliyokuwa ICTR katika eneo la Lakilaki ndani ya wakati na kwa bajeti iliyopangwa.

“Kwa namna ya pekee tunampongeza Msajili wa Mahakama, Bw. John Hopkins kwa uongozi wake na ushirikiano wake ambao umewezesha kukamilisha hatua hii muhimu sana”. Alisisitiza Balozi.

Aidha kukamilika kwa majengo hayo na ambayo yapo katika ardhi ya Tanzania ni heshima na fahari kubwa na ya kipekee kwa Tanzania na wananchi wake kutokana na jukumu kubwa iliyobeba ya kuwa mwenyeji wa Mahakama ya Kimataifa ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda kwa niaba ya Jumuiya ya Kimataifa. 

Balozi Manongi pia amepongeza uratibu uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa kupitia Ofisi ya Mshauri wa Sheria, Ofisi ya Msajili na the Hegue ya kuhakikisha kwamba, pamekuwapo na utaratibu mzuri wa kurithishana kutoka ICTR kwenda IRMCT. Na kwamba kazi hiyo haikuwa nyepesi.

Akizungumzia kuhusu kazi za IRMCT, Balozi amesema, Tanzania ingependa kuona Taasisi za Kitaifa zinawezeshwa ili ziweze kushughulikia kwa ukamilifu, haki na usawa na kwa kuzingatia sheria za kimataifa kesi zinazopelekwa kwenye Taasisi hizo za kitaifa.Aidha akasema uzoefu ambao umepatikana kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na ICTR pamoja na ile ya ICTY ni vema ukatumika kama mfano katika Mahakama nyingine za Kimataifa.

Kwa upande wa mashahidi, Tanzania imesisita umuhimu wa mashahidi kulindwa na kuhakikishiwa usalama wao dhidi ya vitisho mara baada ya kutoa ushahidi.Kuhusu watu walioachiwa huru baada ya kukamilisha vifungo vyao na bado wapo nchini Tanzania. Tanzania imeungana na wazungumzaji wengine katika mkutano huo wa kutaka pawepo na majadiliano ya kina ya kuangalia namna gani ya kuwasaidia watu hao.

Vilevile Tanzania imetoa wito kwa nchi zile ambazo zinahisiwa kwamba zinawahifadhi watuhumiwa watatu ambao wapo mafichoni na wanatakiwa kufikishwa katika vyombo vya sheria kutoa ushirikiano ili hatimaye haki itendeke.Watuhumiwa ambao wametajwa kuwa walihusika kwa namna moja ama nyingine katika mauaji ya Kimbari nchini Rwanda na wapo mafichoni hadi sasa ni Augustin Bizimana, Felicien Kabuga na Proitas Mpiranya. 

Kwa mujibu wa Ripoti iliyowasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, watuhumiwa hao watakapopatikana kesi zao zitafanyika katika Mahakama hiyo mpya nchini Tanzania.Uamuzi kwa kuwa na matawi ya IRMCT huko Arusha na the Hague, Uholanzi unatokana na maamuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia azimio nambari 1966 la mwaka 2010.

Kupitia Azimio hilo Baraza la Usalama liliamua kwamba, baada ya kumalizika rasmi kwa ICTR ( 2015) na ICTY ( 2017) Tanzania ambayo ndiyo ilikuwa mwenyeji wa ICTR itapewa jukumuu la kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka zote muhimu za iliyokuwa ICTR ikiwa ni pamoja na kumalizia kesi zitakazokuwa zimebaki. Huku the Hague ikiwa na dhamana hiyo hiyo kwa kazi zilizokuwa za iliyokuwa ICTY.

Mahakama za Kimataifa za Rwanda na Yugoslavia ambazo zimefanya kazi kubwa ya kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa karibu wote waliohusika na matukio ya kutisha ya ukiukwaji wa haki za binadamu ziliazishwa mwaka 1990 na Umoja wa Mataifa.
Mwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya utendaji kazi wa IRMCT ambapo alimshukuru kwa namna ya pekee Msajili wa IRMCT Bw. John Hopkins kwa uongozi wake na ushirikiano ambao ameonyesha katika ujenzi wa majengo mapya huko Lakilaki lakini pia katika kusimamia kipindi cha mpito na makabidhiano kutoka ICTR kwenda IRMCT.
Rais wa IRMCT, Bw. Theodor Meron akiwasilisha mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hapo siku ya jumatano, Ripoti ya utendaji kazi wa Matawi ya Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia zinachokua nafasi ya iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) na Mauaji ya halaiki yaliyotokea katika iliyokuwa Yugoslavia ya zamani ( ICTY. Bw. Meron alitumia pia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa hali na mali katika ujenzi wa majengo yanayochokua nafasi ya ICTR majengo hayo yamejengwa katika eneo la Lakilaki Mkoani Arusha

Wednesday, November 9, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika kujadidili masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano zaidi baina ya Tanzania na China na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo Nchini.
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa China nchini Mhe. Dkt.Youqing


Mazungumzo yakiendelea

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akimsikiliza  Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Dkt. Youqing

Tuesday, November 8, 2016

Mwambata wa jeshi wa Jamhuri ya watu wa China nchini atembelea Wizara ya Mambo ya Nje



Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki akiwa pamoja na mwambata wa Jeshi wa Jamhuri ya watu wa China hapa nchini, Meja Jenerali He Xinchong alipomtembelea wizarani leo Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao waliongelea kuhusiana na Ziara ya Jenerali FAN Changlong Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni Kuu ya Jeshi la Jamhuri ya watu wa China, inayotarajiwa kufanyika  nchini kuanzia tarehe 19 hadi 21 Novemba, 2016.





Friday, November 4, 2016

Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Jeffrey Labovitz alipotembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji ametembelea nchini kwa mara ya kwanza toka shirika hilo lijiunge na Umoja wa Mataifa.  Mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili hali ya wakimbizi nchini, biashara haramu ya binadamu, hali ya wahamiaji haramu, na ushiriki wa watanzania wanaoishi ughaibuni katika kuchangia maendeleo ya nchi.
Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akimsiliza Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Labovitz



Mkutano ukiendelea

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Labovitz wakipeana mikono mara baada ya mazungumzo
Mkurugenzi wa Diaspora (Watanzania waishio ughaibuni) Balozi Anisa Mbega (kushoto) akiwa pamoja na maafisa wa Wizara wakifuatilia mazungumzo

Wakiwa katika picha ya pamoja