Monday, August 7, 2017

Hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Bomba la Mafuta

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Bomba la Mafuta

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameitaja tarehe ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania kuwa ni siku ya maendeleo ya kweli kwa Tanzania na Uganda na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla.

Uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba hilo litakalokuwa na urefu wa kilomita 1445 litakalogharimu takribani Shilingi trilioni 8 za Tanzania ulifanywa na Rais Magufuli na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni katika eneo la Chongoleani mkoani Tanga siku ya Jumamosi tarehe 05 Agosti 2017 na kushuhudiwa na umati mkubwa wa watu wakiwemo viongozi wakuu wa Serikali na vyama vya siasa kutoka pande zote mbili.

Rais Magufuli alieleza kuwa hadi kufikia hatua ya uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa bomba hilo, vikwazo vingi vilijitokeza, hivyo anamshukuru Rais Museveni kwa kuipa kipaumbele Tanzania kwa kuwa bomba hilo lingeweza kupita mahali pengine ambako umbali ungekuwa mfupi kwa zaidi ya kilomita 500.

Aliendelea kueleza kuwa licha ya Tanzania kutoa vivutio vingi kwa Uganda ikwemo kusamehe baadhi ya kodi kama za ongezeko la thamani lakini ujenzi wa bomba hilo utakuwa na manufaa makubwa kwaTanzania katika kipindi cha ujenzi unaotarajiwa kuanza mwezi Januari 2018 na kukamilika mwaka 2020 na baada ya kukamilika kwa ujenzi huo.

"Tutapata mamilioni ya Dola yatakayotokana na ada ya usafirishaji ambayo ni Dola 12.5 kwa pipa moja na inakadiriwa kwa siku yatasafirishwa mapipa 216,000". Rais Magufuli alisema.

Manufaa mengine ni pamoja na ajira ambapo inakadiriwa watu kati ya elf 10 hadi 15 watapata ajira za kudumu bomba litakapokamilika na ajira za muda mfupi za watu zaidi ya elf 30 katika kipindi cha ujenzi.

Aidha, bomba litakuza biashara ya bidhaa mbalimbali ikiwemo saruji na vifaa vingine vitakavyotumika katika ujenzi wa bomba,  ujenzi wa nyumba za kupangisha na kuchochea ujenzi wa viwanda ambavyo malighafi zake zinatokana na mabaki yanayotokana na usafishaji wa mafuta kama vile viwanda vya mbolea. 

Vile vile, bomba linatarajiwa kupunguza gharama za uendeshaji katika sekta ya anga kutokana na unafuu wa mafuta na linakuja wakati mwafaka kwa kuwa Tanzania imeshaanza kulifufua shirika lake la ndege na Uganda ipo mbioni pia kulifufua shirika lake. Imeelezwa kuwa moja ya sababu ya Mashirika ya ndege ya nchi za Mashariki ya Kati kufanya vizuri kibiashara inatokana na unafuu wa mafuta ya ndege.

Mhe. Rais alitoa wito kwa wakandarasi watakaojenga bomba hilo kuharakisha  ujenzi ili uweze kukamilika kabla ya muda uliopangwa wa miaka mitatu.

"Kuna sababu gani ya kutumia muda wote huo wakati fedha zipo na wakandarasi wote mnatoka nchi kubwa zilizopiga hatua ya maendeleo, Tuoeni zabuni kwa wakandarasi wengini (sub contractors) ili ujenzi ukamilike kwa muda mfupi". Rais Magufuli alishauri. 

Wakandarasi watatu, wawili kutoka Ufaransa, Total na Cnooc na mwingine kutoka Uingereza, Tullow Oil kwa pamoja watajenga bomba hilo.

Mhe. Magufuli alibainisha kuwa Tanzania na Uganda zipo katika mazungumzo ili wataalamu wa Kiganda waliogundua mafuta hayo mwaka 2006 waje Tanzania kufanya utafiti kwenye maziwa ya Tanganyika na Eyasi ambayo yana viashiria vya kuwepo kwa mafuta.

Rais Magufuli alihitimisha hotuba yake kwa kumuhakikishia Mhe. Museveni kuwa Tanzania ni nchi iliyokamilika kiulinzi, hivyo Waganda wasiwe na wasi wasi kuhusu usalama wa bomba hilo ambalo litapita katika mikoa 8 ya Tanzania , wilaya 24 na vijiji 124.

Kwa upande wake, Rais Museveni aliishukuru Tanzania kwa kutoa vivutio vingi ili ujenzi wa bomba hilo uendelee kwani bila ya hivyo mafuta hayo hayatakuwa na faida ukizingatia bei ya mafuta katika soko la dunia imeshuka.

Alisema sababu kubwa ya bara la Afrika kuwa masikini hadi leo ni kutumia bidhaa isiyozalisha na kuzalisha bidhaa isiyotumia. 

Kwa mujibu ya takwimu alizotoa, nchi za Afrika Mashariki zinaagiza bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 33 na inauza bidhaa zenye thamani ya Dola milioni 13.8 tu kwa mwaka. Fedha hizo zinafaidisha nchi zilioendelea kuimarisha uchumi wao na kuziacha nchi za Afrika kubaki masikini.

Kutokana na hali hiyo, Rais Museveni alizisihi nchi za Afrika zibadilishe mfumo wa uchumi kwa kujenga viwanda na kuuziana bidhaa. Hivyo, ana matumaini makubwa  kuwa ujenzi wa bomba hilo litaongeza kipato kitakachotumika kuchochea mabadiliko ya kiuchumi ndani ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella aliwahakikishia Marais wawili kuwa mkoa umejipanga kutoa huduma stahiki kwa wageni wote watakaoingia mkoani humo kwa ajili ya ujenzi wa bomba hilo.

"Tumejipanga kuzalisha chakula cha kutosha na tumetenga maeneo ya kujenga nyumba za makazi, hivyo wawekezaji jitokezeni kuchukua maeneo hayo". Mkuu wa Mkoa alihimiza. Aliwasihi watu wa Tanga wasomeshe watoto wao ili waweze kuwa na vigezo vya kupata ajira zitakazotokana na ujenzi wa bomba hilo.

Alihitimisha kwa kumuomba Rais Magufuli asaidie kuimarisha bandari ya Tanga angalau iwe na kina cha mita 12 ili iweze kuhudumia meli zote zitakazotumika kubeba shehena za vifaa vya kujengea bomba la mafuta.


 -Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Tanga, 05 Agosti, 2017.

Viongozi Wakuu wa Serikali wakiwa katika mstari kwa ajili ya kuwapokea Waheshimiwa Marais wa Tanzania na Uganda kwenye viwanja vilivyofanyika hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga nchini Tanzania. Mwenye ushungi ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Madam Balozi Grace Martin, Mkuu wa Itifaki

Rais wa Jamhuri ya Muungno wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (kulia) akiwa kwenye Meza Kuu na Mgeni wake, Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni (katikati) na Makamu wa Rais, Mama Samia Hassan Suluhu.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella akitoa neno la ukaribisho kwa Marais wa Uganda na Tanzania na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta iliyofanyika katika eneo la Chongoleani mkoani Tanga tarehe 05 Agosti 2015.

Bw. Guy Mourice, Rais wa Kampuni ya Total na Msimamizi  wa ujenzi wa bomba hilo akitoa maelezo mafupi kuhusu ujenzi wa bomba hilo utaskavyotekelezwa.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Mhe. Abdulrahman Kinana akiwasalimia viongozi na wananchi waliofurika viwanjani hapo kushuhudia hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta.

AWaziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi.

Makamu wa Rais, Mhe. Samia Hassan Suluhu akiwasalimia wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Uganda akisoma hotuba yake kwenye hafla ya uwekasji wa jiwe las msingi la ujenzi wa bomba ls mafuta ghafi kutoka Uganda hadi Tanga.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisoma hotuba katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa bomba lamfuta kutoka Uganda hadi Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda akipeana Mkono na Bw. Ruge Mutahaba wa Cloud FM. Wawili hao walitakiwa  na Mhe. Rais Magufuli kumaliza tofauti zao.

Viongozi mbalimbali wakiwemo Waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wabunge walioshiriki hafla hiyo.

Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi.

Burdani ndani ya viwanja vya Chongoleani.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (kulia) na Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakiweka jiwe la Msingi kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania.

Waheshimiwa Marasi wakishikana mikono baada ya kuweka jiwe la msingi.

Thursday, August 3, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kifaru

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Dkt. Viktor Korcek, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kifaru ambaye pia ana nia ya kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania katika Jamhuri ya Czech.
Mazungumzo yakiendelea
Dkt. Korcek nae akimweleza jambo Dkt. Kolimba.
Picha ya pamoja


Monday, July 31, 2017

Waziri Mahiga akutana na Mchungaji Ongere

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akisalimiana na Mchungaji John Oscar Ongere ambaye alifika ofisini kwa Mhe. Waziri kujadili maandalizi ya Kongamano kubwa la uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini mwezi Novemba 2017..Kongamano hilo litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam litajumuiya wafanyabiashara wakubwa kutoka kote duniani na wa hapa nchini kujadiliana namna bora ya kutumia fursa lukuki za uwekezaji zilizopo hapa nchini.

Mchungaji Ongere akifanya maombi kwa ajili ya kuiombea nchi amani na utulivu ili iweze kukua kiuchumi
Picha ya pamoja
 Balozi wa Iran
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Mousa Farhang ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.  Mazungumzo yao pamoja na mambo mengine walijadili maandalizi ya sherehe za kumuapisha Rais Mteule wa Iran, Mhe. Hassan Rouhani zitakazofanyika Tehran tarehe 05 August 2017.

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo, Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi-Mrutu, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw Ayoub Mndeme na Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu.

Ujumbe aliofuatana nao Balozi wa Iran ukifuatilia mazungumzo.

Saturday, July 29, 2017

Balozi Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Uganda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Tumusiime Kabonero katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera, leo tarehe 29/07/2017. Waziri Mahiga yupo Mkoani Kagera kwaajili ya kuhudhuria Mkutano wa Ujirani mwema Kati ya Tanzania na Uganda. 
Waziri Mahiga akizungumza na Balozi Mteule Kabonero
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mej.Gen. Salum M. Kijuu ( wa pili kutoka kulia), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga ( wa kwanza kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Grace Mgavano (wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, nao walikuwepo kushuhudia tukio hilo
Balozi Mgavano akisalimiana na Balozi Mteule Kabonero
Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kupokea nakala za utambulisho za Balozi Mteule Mhe. Kabonero.

Friday, July 28, 2017

KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU CHA UJIRANI MWEMA BAINA YA TANZANIA NA UGANDA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Aziz Mlima akizungumza wakati akifungua mkutano wa ujirani mwema kati ya Tanzania na Uganda, ngazi ya Makatibu Wakuu. Mkutano huo unao jadili pia masuala ya mpaka umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa ELCT Mjini Bukoba, Mkoani Kagera.
Ujumbe kutoka nchi ya Uganda wakifuatilia kwa makini hotuba ya Dkt. Mlima (hayupo pichani),  alipokuwa akizungumza wakati wa ufunguzi.
Ujumbe wa upande wa Tanzania nao wakimsikiliza kwa makini Dkt. Mlima (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, wa kwanza kutoka kulia ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu (wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome, na wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi Dr. Florens Turuka
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda  Balozi Patrick Mugoya naye akizungumza kwenye ufunguzi  wa Mkutano huo kati ya Tanzania na Uganda kwa ngazi ya Makatibu wa Kuu.
Dkt. Mlima (katikati) akitoa miongozo ya kikao hicho, wa kwanza kulia ni Bw. Suleiman Salehe (kulia), Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na wa kwanza kushoto ni  Balozi Mugoya.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania ukisikiliza  kwa makini miongozo iliyokuwa inatolewa na Dkt. Mlima (hayupo pichani).
Sehemu ya Makatibu wa Kuu upande wa Uganda, nao wakisikiliza kwa makini miongozo iliyokuwa ikiendelea kutolewa na Dkt. Mlima (hayupo pichani), wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Uganda, na kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Mazingira Uganda.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera Naibu Kamishina Jeremiah M. Nkondo (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kagera Bw. Butenge  Christopher.


Tanzania kuimarisha mipaka yake na nchi jirani

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi (Mb.), katikati, anaongoza ujumbe wa Tanzania kwenye ziara ya kutembelea na kujifunza juu ya mipaka iliyopo kati ya Tanzania na Uganda. Watatu kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Isaack Kamwele, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba (wa tatu kutoka kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima (wa pili kutoka kulia), Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe Gerson John Mdemu (wa kwanza kulia) na wa kwanza kushoto ni Bw. Deogratias Nholope, wakitizama Mto Kagera ulipopita.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba akisalimiana na wanakijiji wanaoishi mpakani mwa Tanzania na Uganda, mara baada ya kuwasili kwenye eneo hilo na kujionea alama za mipaka.
Mhe. Lukuvi pamoja na ujumbe wa Manaibu Waziri wakisalimiana na wanakijiji wa pande zote mbili, ambapo wananchi hao walionekana kufurahishwa na ziara hiyo.
Mhe. Lukuvi pamoja na ujumbe alioambatana nao, wakiwemo wataalamu kutoka sekta mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja.
Mhe. Lukuvi akijadiliana jambo na Manaibu Waziri alioambatana nao kwenye ziara ya kujifunza na kujionea mipaka iliyopo kati ya Tanzania na Uganda. Wa pili kutoka kulia ni Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mhandisi Isaack Kamwelwe Naibu Waziri wa Maji (wa pili kutoka kulia), na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Jafo Selemani Said (wa kwanza kulia).
Ziara ikiendelea ambapo Ujumbe ulioongozwa na Mhe. Lukuvi alipata fursa ya kutembelea majengo yanayotumika kwenye kukagua mizigo na kukusanya ushuru wa forodha kati ya Tanzania na Uganda yanayopatikana eneo la Mtukula.
Picha ya pamoja ya ujumbe wa viongozi na wataalam wa Tanzania ulioongozwa na Waziri Lukuvi wakiwa kwenye moja ya alama iliyopo mpakani mwa Tanzania na Uganda.

Thursday, July 27, 2017

Balozi Mero amkaribisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Professa Mussa Assad New YMork

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Modest Mero akimkaribisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Professa Mussa Assad kwenye ofisi za uwakilishi Jijini New York Marekani hivi karibuni. 

http://www.mwananchi.co.tz/habari/CAG-awasilisha-ukaguzi-mashirika-ya-Umoja-wa-Mataifa/1597578-4034028-j2vri7/index.html

TAARIFA YA KIFO CHA BI. LOVENESS HERMAN, MTANZANIA MWENYE URAIA WA UBELGIJI

 
Mwenye picha katika kitambulisho hapo juu ni Bi. Loveness Herman (69), Mbelgiji mwenye asili ya Tanzania ambaye alifariki huko Liege, Ubelgiji tokea tarehe 18 Mei 2017. Marehemu Loveness Herman kabla ya kuhamia Ubelgiji na kuchukuwa uraia wa nchi hiyo katika miaka ya 1980 alikuwa akiishi Dar es Salaam. Tokea alipohamia Ubelgiji, Marehemu alikuwa akiishi peke yake na hakuwahi kupata mtoto. Kwa taarifa hii, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wake wa Brussels inawatafuta ndugu zake ili iwape taarifa kamili za msiba huo
Kwa maelezo zaidi  piga simu katika namba hii +3226406500 au barua pepe brussels@nje.go.tz.

                             

Kaimu Balozi wa Saudi Arabia atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini, Bw. Bandar Abdullah Alhazani ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Masuala yaliyojadiliwa katika mazungumzo hayo ni pamoja na uhusiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia ambao ulielezwa kuwa ni mzuri.

Waziri Mahiga akisoma barua aliyokabidhiwa na Kaimu Balozi ambayo ni mwaliko kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia ikimwalika kufanya ziara ya kikazi nchini humo katika muda utakaopangwa baadaye. Mhe. Mahiga anaalikwa nchini Saudi Arabia kufuatilia utekelezaji wa masuala yaliyoafikiwa wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia alipofanya ziara hapa nchini mwezi Machi 2016.

Mazungumzo yanaendelea



Wednesday, July 26, 2017

Tanzania calls for immediate solution on Diplomatic crisis in Gulf Countries


PRESS STATEMENT

Tanzania calls for immediate solution on Diplomatic crisis in Gulf Countries

The united Republic of Tanzania is supporting the initiatives taken by the Amir of Kuwait HH Sheikh Sabah Al-Jaber Al-Sabah’s mediation efforts to address the Gulf crisis and the exploration of possible solution methods.

The diplomatic crisis began in June 5th 2017 when Saudi Arabia, United Arab Emirates, Bahrain, and Egypt abruptly cut off diplomatic relations with Qatar by withdrawing ambassadors and imposing trade and travel bans.

Tanzania call for unity and stability of the Gulf region and it emphasis that a solution should be found within the framework of the Gulf Cooperation Council and in that regards, it joins and support the initiative of the State of Kuwait that called for the crisis to be resolved through peaceful negotiations.

We therefore, appeal to the Gulf Nations to quickly resolve their disputes in peaceful and diplomatic manner.


Issued by Government Communication Unit, Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation

26 July, 2017