Friday, October 25, 2019

WAZIRI KABUDI ASHIRIKI MAADHIMISHO YA 74 YA SIKU UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini alipowasili katika uwanja wa Nyerere Square jijini Dodoma kushiriki maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa amesimama sehemu maalumu wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa unapigwa kwenye sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa mbele ya parede maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akikagua parede maalumu liliondaliwa kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja Mataifa 
Sehemu ya hadhara iliyojitokeza katika uwanja wa Nyerere Square kushuhudia sherehe za maadhimisho 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (katikati) akifuatalia matukio yaliyokuwa yakiendelea wakati wa maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, akipokea zawadi kutoka Ofisi za Umoja wa Mataifa nchini iliyowasilishwa na Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi, kwenye sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika jijini Dodoma 
Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi Wafanyakazi wa Ofisi za Umoja wa Mataifa nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia  hadhira iliojitokeza kwenye maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Taifa iliyofanyika jijini Dodoma katika uwanja wa Nyerere Square

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia  hadhira iliojitokeza (hawapo pichani) kwenye amaadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Taifa iliyofanyika jijini Dodoma katika uwanja wa Nyerere Square


WAKATI HUO HUO MHE. PROF. KABUDI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA  BW. MICHAEL DUNFORD KAIMU MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa na Bw.Michael Dunford Kaimu Katibu Makazi wa Umoja wa
Mataifa nchini, walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma. Wengine ni Bw. Deusdedit Kaganda Kaimu Mkurugenzi wa Ushikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Bi.Glory Ngaiza Afisa Mambo ya Nje.
Waziri Mhe. Prof. Kabudi akilelezea jambo wakati wa mazungumzo na Bw. Michael Dunford Kaimu Katibu Makazi wa Umoja wa Mataifa nchini. Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuendelea kudumisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Umoja wa Mataifa


VILEVILE WAZIRI MHE. PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisisitiza jambo alipokutana wakati wa mazunguzo na Mkuu wa Shirika la Wahamiaji nchini Dr. Qasim Sufi walipokutana kwa mazungumzo katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuendelea kudumisha ushiririkiano kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kutoa huduma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akimsikiliza Mkuu wa Shirika la Wahamiaji nchini Dr. Qasim Sufi walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma

Wednesday, October 23, 2019

MAADHIMISHO YA SIKU YA UMOJA WA MATAIFA KUFANYIKA KESHO, DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza na wanahabari  (hawapo pichani) kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma.

Katika mkutano huo Dkt. Mnyepe amewajulisha waandishi wa habari kuhusu kufanyika kwa maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa tarehe 24 Oktoba, 2019
jijini Dodoma kwenye uwanja wa Nyerere square.  

Dkt. Mnyepe amebainisha kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho hayo, yatakayofanyika kuanzia saa 2.30 asubuhi hadi 5.00 asubuhi.

Maadhimisho ya mwaka huu yataongozwa na kauli mbiu isemayo "Wanawake na Wasichana kuwa Kipaumbele katika kufikia Malengo ya Dunia. Kauli mbiu hii inalenga kusisitiza uwajibikaji na ushirikishwaji wa Wanawake katika kufikia malengo ya dunia.

Aidha, Katibu Mkuu Dkt. Mnyepe amebainisha kuwa Tanzania itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuheshimu na kusimamia misingi ya kulinda na kutetea maslahi ya Wanawake na Wasichana ikiwemo kuwashirikisha katika mipango ya maendeleo ya kijamii na uchumi.

Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Mataifa hufanyika kila mwaka tarehe 24 Oktoba. Maadhimisho ya mwaka huu ambayo yatapambwa na shamrashamra kutoka vikundi mbalimbali vya sanaa, yanatarajiwa kuhudhuriwa na Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali, Wawakilishi kutoka ofisi za Umoja wa Mataifa nchini, vijana, asasi za kiraia na wadau wengine mbalimbali.
Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano uliofanyika ofisi za Wizara ya Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.   
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (katikati) Bw. Deusdedit Kaganda Kaimu Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini wakisikiliza maswali kutoka kwa Wanahabari (hawapo pichani).
Picha ya pamoja baada ya mkutano na waandishi wa habari

Saturday, October 19, 2019

PROF. KABUDI AKUTANA NA BALOZI MTEULE WA EU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazugumzo na Balozi  Mteule wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fanti katika ofisi ndogo za Wizarajijini Dar es Salaam.

Balozi Mteule wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fantiakifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na Balozi Mteule wa Rwanda nchini, Meja Jenerali Karamba Charles jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Itifiki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Wilbert Ibuge akimkaribisha Balozi Mteule wa Rwanda nchini, Meja Jenerali Karamba Charles katika ofisi ndogo za Wizarajijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokea nakala ya hati ya utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fanti. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokea nakala ya hati ya utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Rwanda nchini, Meja Jenerali Karamba Charles. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Wilbert Ibuge.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika picha ya pamoja na Balozi mteule wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fanti na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Wilbert Ibuge, pamoja Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mona Mahecha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika picha ya pamoja na Balozi mteule wa Rwanda nchini, Meja Jenerali Karamba Charles. Kulia ni Mkuu wa Itifiki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Wilbert Ibuge.

Prof. Kabudi akutana, kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fanti.
Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam ambapo Waziri Kabudi amemueleza Balozi Fanti kuwa Uhusiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya ni wa Muda mrefu tangu mwaka 1975 ambao hadi sasa Tanzania imekuwa na mahusiano imara na umoja huo.
"Ushirikiano wa Tanzania na Umoja wa Ulaya umelenga kupunguza umasikini, kukuza maendeleo endelevu, na kusaidia ujumuishaji wa Tanzania katika uchumi wa dunia, mpango kazi wa ushirikiano huu unaundwa na nguzo kuu tatu ambazo ni maendeleo ya uchumi, biashara na uwekezaji pamoja na mazungumzo ya kisiasa. Msaada wa Umoja wa Ulaya umeweza kushughulikia changamoto mbalimbali katika ajenda za maendeleo ya kitaifa" Alisema Prof. Kabudi
 Waziri Kabudi ameongeza kuwa, kulingana na takwimu za mwaka 2017, Umoja wa Ulaya unaonekana ndiye mshirika mkubwa zaidi wa biashara ya bidhaa kwa Tanzania baada ya India, kwa asilimia 13.1. Bidhaa zinazoingizwa kutoka Umoja wa Ulaya ni pamoja na mashine, vifaa, bidhaa za kemikali na vifaa vya usafirishaji.  
 Prof. Kabudi amegusia pia mazungumzo ya kisiasa na kueleza kuwa ni nguzo muhimu ya uhusiano wa Tanzania na Umoja wa Ulaya. Mazungumzo ya kisiasa yanalenga kuongeza uwazi na umoja ili kukuza uelewa wa pamoja katika vyama vya siasa.
 Balozi mteule wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Balozi Manfredo Fanti amesema kuwa Umoja huo upo tayari kusaidia Tanzania na kuhakikisha kuwa sera za nchi zinasonga mbele ili kuiwezesha Tanzania kuwa na  maendeleo endelevu na kusaidia malengo ya nchi. 
"Pia tupo tayari kuhakikisha kuwa uwekezaji na biashara unaofanywa kati ya Umoja wa Ulaya pamoja na Tanzania unakuwa wa manufaa kwa pande zote lengo likiwa ni kukuza sekta ya biashara hapa Tanzania" Balozi Fanti
Katika tukio jingine Waziri wa Mamno ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule  wa Rwanda hapa nchini, Meja Jenerali Karamba Charles ambaye ameelezea uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Rwanda ni wa kiwango cha juu na kuongeza kuwa jukumu lake kubwa kwa sasa ni kuongeza kiwango cha biashara na uswekezaji kati ya Nchi hizo mbili.
Meja Jenerali Karamba Charles ameyasema hayo wakati akikabidhi nakala za hati ya utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) kuchukua nafasi ya  aliyekuwa Balozi wa Rwanda Nchini Tanzania Balozi Eugene Kayihura ambaye amemaliza muda wake.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar Es Salaam,Tanzania

Friday, October 18, 2019

KUAPISHWA RASMI KWA MFALME MPYA WA JAPAN

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUAPISHWA RASMI KWA MFALME MPYA WA JAPAN   

Dodoma, 19 Oktoba 2019
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt. (Mst) George Mkuchika (Mb.) atahudhuria sherehe za kuapishwa na kutambulishwa kwenye Jumuiya ya Kimataifa kwa Mfalme Naruhito wa Japan zitakazofanyika jijini Tokyo tarehe 22 Oktoba 2019.

Mhe. Mkuchika anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambaye aliakwa katika sherehe hizo na Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Shinzo Abe.

Kwa mujibu wa katiba na sheria za Kifalme za Japan, Mfalme Naruhito amerithi kiti cha Baba yake, Mfalme Akihito ambaye alitangaza kujiuzulu rasmi nafasi yake tarehe 30 Aprili 2019 kutokana na umri wake kuwa mkubwa sanjari na kusumbuliwa na matatizo ya kiafya. Mfalme Naruhito alichukua madaraka hayo tarehe 1 Mei 2019.

Mhe. Mkuchika na ujumbe wake wanatarajia kuondoka nchini tarehe 19 Oktoba 2019 na kurejea tarehe 24 Oktoba 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Thursday, October 17, 2019

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA 18 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NCHI ZA AFRIKA NA NORDIC KUANZIA TAREHE 7-8 NOVEMBA 2019




17 Oktoba, 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA 18 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NCHI ZA AFRIKA NA NORDIC KUANZIA TAREHE 7-8 NOVEMBA 2019

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Nordic (Norway, Denmark, Finland, Sweden na Iceland) unaotarajiwa kufanyika tarehe 08 Novemba 2019 kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.Hii ni mara ya kwanza kwa mkutano huu kufanyika hapa nchini tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000.
Mkutano huu unatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki takribani 250 ambao kati yao thelathini na nne (34) ni Mawaziri wa Mambo ya Nje akiwemo Mhe. Prof. Palamagamba J.A.M. Kabudi (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kadhalika, Mabalozi wa nchi shiriki za Afrika katika nchi za Nordic, Mabalozi wa nchi za Nordic hapa nchini, watendaji kutoka Wizara za Mambo ya Nje za nchi shiriki, wawakilishi wa taasisi za biashara na uwekezaji na Wafanyabiashara za hapa nchini wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huu.
Lengo la kuanzishwa kwa mkutano huu, ambao kwa mara ya kwanza ulifanyika mwaka 2000, ilikuwa ni kutoa nafasi kwa nchi za Nordic na nchi chache za Afrika marafiki zao wa karibu, kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya pande hizo mbili, kuainisha vipaumbele katika ushirikiano huo na kuweka mikakati ya pamoja ya kutekeleza vipaumbele hivyo. Nchi za Afrika na Nordic zimekuwa zikipokezana uenyeji wa mikutano hii kila mwaka. Mwaka 2017, mkutano huu ulifanyika Abuja, Nigeria na mwaka 2018 ulifanyika Copenhagen, Denmark na mwaka huu, utafanyika Tanzania.
Kwa mwaka huu, mkutano huu utajadili namna ya kuimarisha mahusiano yenye tija kwa maendeleo ya nchi washiriki hususan namna ya kukuza ushirikiano kwenye sekta ya biashara na uwekezaji kwa maendeleo endelevu. Aidha, ushirikiano kwenye masuala ya ulinzi na usalama unatarajiwa kupewa kipaumbele kwenye mkutano huu ikizingatiwa kuwa utekelezaji wa shughuli za maendeleo unategemea uwepo wa amani na usalama. 
Tanzania ni nchi ya kipaumbele kwa nchi za Nordic. Ushirikiano kati ya Tanzania na nchi za Nordic ulianza hata kabla ya uhuru wa Tanganyika ambapo wamisionari kutoka nchi hizo walikuja kufanya kazi hapa nchini kwenye sekta za afya na elimu. Katika sekta ya elimu, nchi hizo zilianzisha Kituo cha Kilimo cha Uyole na Kituo cha Elimu cha Kibaha kupitia Mradi wa Nordic-Tanganyika Project. Ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na nchi za Nordic ulichangiwa kwa kiwango kikubwa na falsafa zilizokuwa zinafanana kuhusu maendeleo ya watu, ukombozi wa Afrika, urafiki miongoni mwa viongozi wetu na nafasi ya kimkakati ya Tanzania katika Bara la Afrika. 
Hadi sasa, Tanzania ni nchi pekee iliyopokea msaada mkubwa kifedha kutoka katika nchi za Nordic. Kuanzia mwaka 2013 hadi 2019, Tanzania imepokea takribani shilingi za kitanzania bilioni 900 kutoka kwa nchi za Nordic. Nchi hizo zimekuwa zikisaidia sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo: elimu; afya; miundombinu; nishati; TEHAMA; utafiti; ukusanyaji wa kodi; bajeti; misitu; usawa wa jinsia; hali ya hewa; na ukuzaji wa sekta ya biashara. Kufuatia ushirikiano huu wa kihistoria kati ya Tanzania na nchi za Nordic, nchi hizo ziliiomba Serikali ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa mwaka huu na Serikali kuridhia kwa minajili ya kuendelea kuboresha ushirikiano kati ya pande hizi mbili kwa manufaa ya pande zote.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam.

Job Announcement at the United Nations Environment Programme

PRESS RELEASE

Job Announcement at the
United Nations Environment Programme
  • Dodoma, 17th October 2019. 

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the United Nations Environment Programme (UNEP) inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Chief Scientist available at the Science Division.

Application details can be found on the https://www.unenvironment.org/work-with-us

Closing date for application is 24th October 2019.

Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,

Wednesday, October 16, 2019

Balozi Kairuki awasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Vietnam

Balozi wa Tanzania nchini China ambaye anawakilisha pia Jamhuri ya Watu wa Vietnam, Mhe. Mbelwa Kairuki akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Vietnam, Mhe. Nguyen Phu Trong katika Ikulu ya Vietnam leo jijini Hannoi
Balozi wa Tanzania nchini China ambaye anawakilisha pia Jamhuri ya Watu wa Vietnam, Mhe. Mbelwa Kairuki akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Jamhuri ya Watu wa Vietnam, Mhe. Nguyen Phu Trong katika Ikulu ya Vietnam leo jijini Hannoi.

Tuesday, October 15, 2019

PROF KABUDI KATIKA KONGAMANO LA MIAKA 20 BILA NYERERE - UDSM

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), akitoa hotuba yake wakati akifungua kongamano la miaka 20 bila Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julias Nyerere katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Katika Kongamano hilo, Waziri Kabudi amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.  
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally (kushoto) Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Makinda pamoja na viongozi wengine wa Serikali na wastaafu wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), katika kongamano la miaka 20 bila Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julias Nyerere katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam


Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), katika kongamano la miaka 20 bila Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julias Nyerere katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Monday, October 14, 2019

Wanafunzi Uganda Wafanya Mdahalo kuhusu Mwalimu Nyerere

Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz P. Mlima (katikati), Mwambata Jeshi, Brig. Gen. Stephen Mkumbo na Afisa anayesimamia masuala ya Utawala Ubalozini wakiwa katika hafla ya Kumbukizi ya Miaka 20 ya Siku ya Mwalimu Nyerere iliyofanyika kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Uganda tarehe 13 Oktoba 2019. Hafla hiyo ilifanyika kwa kufanya mdahalo kuhusu maisha ya Mwalimu Nyerere ambapo wanafunzi mbalimbali kutoka Tanzania wanaosoma elimu ya juu nchini Uganda walishiriki mdahalo huo.
Wanafunzi walioshiriki wakifuatilia kwa makini hoja zilizokuwa zinawasilishwa katika mdahalo huo kuhusu maisha ya Mwalimu Nyerere.
Sanjari na Mdahalo huo, uongozi mpya wa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma vyuo vikuu nchini Uganda walitumia hafla hiyo kuapishwa rasmi kushika madaraka waliyochaguliwa.
Balozi Mlima akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma nchini Uganda.
Uongozi wa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma nchini Uganda wakiwa katika picha ya pamoja.




Sunday, October 13, 2019

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAKABIDHIWA JENGO JIPYA NA CHINA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke,wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya  la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masharii lililojengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Watu China na kukabidhiwa Serikaali ya Tanzania. Tukio hilo limefanyika jijini Dar es Salaam. 

Naibu katibu Mkuu, Mizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi na Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke wakisaini mkataba wa makabidhiano ya jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Anayeshuhudia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb).

Balozi wa China Nchini, Balozi Wang Ke akishikana mkono na Naibu katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi mara baada ya kubadilishana nyaraka walizosaini za kukabidhiana Jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililojengwa kwa msaada wa Jamhuri ya Watu wa China Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke akisoma hotuba yake wakati wa makabidhiano ya jengo jipya  la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaliyofanyika jijini Dar es salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), akisoma hotuba yake wakati wa makabidhiano ya jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaliyofanyika jijini Dar es salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Balozi wa China nchini nchini Tanzania Wang Ke na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje mara baada ya kukabidhiana jengo jipya la wizara hiyo.


Jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo jijini Dar Es Salaam  lililojengwa kwa msaada wa Jamhuri ya Watu wa China kwa jailli ya matumizi ya Ofisi za Wizara hiyo.

Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki wamalizika Jijini Arusha.

12 Oktoba 2019, Arusha.
Mkutano wa 30 wa Baraza la kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango umemalizika tarehe 12 Oktoba 2019 kwenye Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jijini Arusha - Tanzania. Mkutano huu wa siku sita (06) umefanyika katika Ngazi zifuatazo:
  1. Mkutano katika Ngazi ya Maafisa Waandamizi tarehe 7 na 8 Oktoba, 2019;
  2. Mkutano katika Ngazi ya Makatibu Wakuu tarehe 9 na 10 Oktoba 2019 na
  3. Mkutano katika Ngazi ya Mawaziri tarehe 11 na 12 Oktoba 2019.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu umeongozwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb) akisaidiana na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent L. Bashungwa (Mb); Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Balozi Dkt. Augustine P. Mahiga (Mb); Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaju (Mb); Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mary Mwanjelwa pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano  Tanzania.

Mkutano huu umetoa maamuzi na maelekezo mbalimbali ya kisera na kimkakati kwa Nchi Wanachama pamoja na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu Utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya mikutano ya Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyopita pamoja na mkutano wa 10 hadi 28 wa Baraza la kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango; Utekelezaji wa Soko la pamoja la Afrika Mashariki; Utekeleaji wa maagizo katika taarifa ya mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (2000 – 2017); Vipaumbele vya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwaka 2020/21; Maelekezo kuhusiana na mikutano ya Wakuu wa taasisi za masuala ya Uhamiaji na Kazi za Jumuiya, na maagizo ya hadidu za rejea za maandalizi ya mkakati wa mpango wa sita wa maendeleo ya Afrika Mashariki (2021/22).

Aidha, mkutano huu ulitoa mapendekezo katika taarifa ya hali ya ulipaji wa michango ya Nchi Wanachama katika Jumuiya; Taarifa ya uhamasishaji katika masuala ya rasilimali za jumuiya ya Afrika Mashariki na mikakati ya ushirikiano; Taarifa ya Tume ya Ukaguzi ya Jumuiya kwa mwaka 2017/18; Taarifa ya maendeleo ya makubaliano ya maeneo huru ya biashara katika utatu wa COMESA-EAC-SADC;Taarifa ya maendeleo ya makubaliano kuhusu eneo huru la kibiashara barani Afrika (AFCFTA); Taarifa ya maendeleo ya masuala ya kisiasa, na Kalenda ya majukumu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 2019.

Vilevile, wajumbe wa mkutano wamejadili kuhusiana na maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 2000, baada ya kuvunjika kwa jumuiya ya awali iliyoundwa mwaka 1967 na kuvunjika mwaka 1977.

Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki umemalizika tarehe 12 Oktoba 2019 Jijini Arusha, Tanzania.
Pichani ni viongozi wa ujumbe kutoka Nchi Wanachama katika ngazi ya Mawaziri wakisaini maamuzi na mapendekezo waliyoyatoa katika mkutano wa 30 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango.
Kutoka kulia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb); Waziri anayeshughulikia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mshariki, Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa kutoka Rwanda, Mhe. Balozi Olivier J.P Nduhungiuhe; Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki na Maendeleo ya Kikanda kutoka Kenya, Mhe. Ken M. Obura; Waziri Ofisi ya Rais anayeshughulikia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Burundi, Mhe. Isabelle Ndahayo; Waziri wa Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Uganda, Mhe. Rt. Dkt. Kirunda Kivejinja; pamoja na Waziri wa Biashara, Viwanda na masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Sudan Kusini, Mhe. Paul Mayom Akec kutoka.

Mawaziri wa Serikali ya Tanzania walioshiriki katika mkutano wa 30 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango wakiwa katika kikao cha ndani cha maandalizi pamoja na maafisa wengine waandamizi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hawapo pichani).

Pichani; Kutoka kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent L. Bashungwa (Mb); Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Balozi Dkt. Augustine P. Mahiga (Mb); Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mary Mwanjelwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaju (Mb). 

Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen P. Mbundi akijadili jambo pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya MiundombinuMhandisi Steven D. M. Mlote (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia sekta za uzalishaji na jamii, Mhe. Christophe Bazivamo (kushoto). 

Saturday, October 12, 2019

Watalii kutoka Israel wawasili nchini kwa ziara ya siku nane.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bi. Devotha Mdachi akiwakaribisha watalii kutoka nchini Israel mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kwa ndege ya shirika la El Al Israel, leo tarehe 12 Oktoba 2019.
Watalii wapatao 920 wameendelea kuwasili nchini katika makundi tofauti ambapo Watalii wanaowasili kupitia uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro wanatarajiwa kufika 720 na Watalii 200 kwa wale waliokwishawasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar. 

Sehemu ya Watalii kutoka nchini Israel wakipata huduma mara baada ya kuwasili ndani ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro.
Wakiwa nchini watalii hao watatembelea hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Manyara pamoja na Zanzibar ili kuweza kujionea vivutio mbalimbali na kujifunza mambo mbalimbali ya mila na utamaduni wa kitanzania.

Sehemu nyingine ya Watalii kutoka nchini Israel wakipata huduma mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro.
Kikundi cha ngoma cha Wamasai kikitumbuiza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro ikiwa ni ishara ya kuwalaki wageni hao.