Sunday, July 5, 2020

DKT. NDUMBARO ATEMBELEA BANDA LA WIZARA SABASABA


Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, ametembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Wizara Dkt. Ndumbaro amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi ili kuiletea sifa Serikali na kuendelea kuimarisha mahusiano ya kimataifa.

"Kwa kuwa sisi tunafanya kazi ya kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Nje na kuhakikisha mahusiano ya kimataifa yanaimarika hatuna budi kufanya kazi kwa bidii na maarifa yetu yote, hili ni jukumu letu hivyo ni lazima tuhakikishe tunalitekeleza kwa ufanisi na ufasaha," Amesema Dkt. Ndumbaro

Akiwa katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Dkt. Ndumbaro ametembelea pia banda la Bunge, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Dodoma na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.


Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.




Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Ndumbaro, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea jijini Dar es Salaam.




Thursday, July 2, 2020

PROF. KABUDI ATETA NA MJUMBE MAALUM WA MAZIWA MAKUU



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Prof. Kabudi ateta na Mjumbe Maalum wa Maziwa Makuu

Dodoma, 2 Julai 2020
Tanzania inaamini katika umoja wa jumuiya ya kimataifa kwenye kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia ikiwemo mlipuko wa ugonjwa wa Corona.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) alipofanya mazungumzo kwa njia ya mtandao na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye eneo la Maziwa Makuu, Balozi Huang Xia.

Viongozi hao walitumia fursa hiyo kubadilishana mawazo katika masuala mbalimbali yanayotokea duniani, ikiwa ni pamoja na mikakati na mbinu bora za kukabiliana na janga la ugonjwa wa Corona na athari zake katika uchumi kwenye eneo la Maziwa Makuu.   

Balozi Huang alielezea hatua mbalimbali anazozichukua zikiwemo kuongea na taasisi za kimataifa za fedha na wadau wengine kwa ajili ya kuzihimiza kutoa misaada kwa nchi za Maziwa Makuu ili ziweze kukabiliana na janga la ugonjwa wa Corona na athari zake za kiuchumi na kijamii. Licha ya kukutana na taasisi hizo, Balozi Huang pia amefanya mashauriano na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Maziwa Makuu kuhusu janga la Corona. Kwenye mashauriano hayo Mawaziri wamesisitiza umuhimu wa kuandaa mkutano wa Mawaziri kwa njia ya mtandao ili kujadili, pamoja na mambo mengine mikakati ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona na hali ya usalama katika eneo la Maziwa Makuu.

Kwa upande wake, Prof. Kabudi aliunga mkono wazo la kuwa na mkutano wa Mawaziri wa nchi za Maziwa Makuu na kuelezea matumaini yake kuwa, mkutano huo utatoa mawazo mazuri yatakayosaidia ufumbuzi katika changamoto zinazoikabili dunia ukiwemo ugonjwa wa Corona.

Aidha, Prof. Kabudi alitoa maelezo kuhusu mikakati iliyochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kudhibiti ugonjwa wa Corona. Alisema moja ya mikakati hiyo ni tangazo la maombi ya siku tatu kwa nchi nzima lililotolewa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, maombi ambayo yaliyohusisha imani zote.  Tangazo hilo  lilionekana ni jambo geni kwa watu wengi duniani lakini kwa Tanzania, nchi yenye waislamu na wakristo takribani nusu kwa nusu, lilikuwa ni muhimu na uamuzi huo haukuifanya Tanzania kupuuza maelekezo mengine yanayotolewa na wataalam wa afya.   

Mazungumzo hayo yalihitimishwa kwa Mhe. Waziri kuahidi kuwa, Tanzania itashirikiana kwa karibu na ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika uamuzi wake wa kuandaa mkakati maalum wa kuzuia migogoro na kuimarisha amani na utulivu kwenye eneo la nchi za maziwa makuu.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akizungumza kwa njia ya mtandao na Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu, Mhe. Balozi Huang Xia kuhusu ushirikiano katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona na masuala ya amani na usalama katika ukanda huo. Mazungumzo hayo yalifanyika Prof. Kabudi akiwa jijini Dodoma huku Balozi Huang Xia akiwa jijini Nairobi, Kenya.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Prof. Kabudi ukifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Kabudi na Balozi Huang Xia (hawapo pichani). Kulia ni Bw. Magabilo Murobi, Katibu wa Waziri na Bw. Ali Ubwa, Afisa Mambo ya Nje.




Monday, June 29, 2020

VACANCY ANNOUNCEMENT



PRESS RELEASE


VACANCY ANNOUNCEMENT

Dodoma, 29 June 2020

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the Commonwealth Secretariat inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Assistant Research Officer-International Trade Policy Section.

Application details can be found through the Secretariat’s website, http://thecommonwealth.org/jobs. Closing date for application is Wednesday 8 July 2020.


“The Ministry encourages qualified Tanzanians to apply”.



Issued by;
Government Communication Unit


Friday, June 26, 2020

MKUTANO WA MAWAZIRI WA KAMATI YA SADC YA ASASI YA USHIRIKIANO WA SIASA, ULINZI NA USALAMA (TROIKA) WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM


Mkutano wa Mawaziri wa Kamati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama kwa ngazi ya Mawaziri umefanyika kwa njia ya Mtandao (Video Conferencing) na kujadili masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama.

Mkutano huo umefanyika chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara ya Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Sibusiso Busi Moyo na utakutanisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mambo ya Ndani, Ulinzi pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutoka nchi wanachama wa SADC. Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi.

Mkutano huo umehudhuriwa na nchi 16 wanachama wa SADC ambazo ni Angola, Afrika Kusini, Botswana, Comoro, DRC, Eswatini, Lesotho, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Zimbabwe na Mwenyekiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati), kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nchi George Simbachawene na mwisho kushoto ni Katibu  Mkuu Wizara ya Ulinzi, Dkt. Faraji Mnyepe wakifuatilia mkutano kwa njia ya video conference, Jijini Dar es salaam

Mawaziri pamoja na baadhi ya Makatibu Wakuu/Maafisa waandamizi kutoka Tanzania wakifuatilia mkutano kwa njia ya Video Conference, jijini Dar es Salaam

Mkutano ukiendelea  





IMF YAAHIDI KUIPATIA TANZANIA FEDHA ITAKAYOIHITAJI


Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeahidi kuipatia Tanzania fedha itakayoihitaji ili iweze kuendelea kukabiliana na athari zitokanazo na janga la Covid 19 kwa ajili ya kuimarisha uchumi wake.

Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi leo katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Pia Bw. Reinke ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua madhubuti inazozichukua katika kukabiliana na janga la Covid 19 ili kuepusha madhara ya kiuchumi na kijamii.

Mazungumzo hayo pia yamelenga miradi ya maendeleo, msamaha wa madeni kwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, ushirikiano baina ya IFM na Tanzania, biasara na utalii. 
  
Kwa upande wake, Prof. Kabudi ameishukuru (IMF) kwa msamaha wa madeni ambao umetolewa kwa Tanzania na nchi nyingine, fedha zitakazoziwezesha nchi hizo kuendelea kukabiliana na Covid 19.

"Tumeongelea mambo mbalimbali yanayohusu ushirikiano hasa katika kuimarisha uchumi wetu baada ya janga la covid 19, usirikiano kati ya Tanzania na IMF unafahamika na tumekubaliana baadhi ya mambo ambayo tutayafanyia kazi kwa kina ili tuweze kuimarisha uchumi wetu baada ya corona hasa katika sekta ya utalii, biashara na miundombinu," amesema Prof. Kabudi.

Katika hatua nyingine, Waziri Kabudi amekutana na kumuaga Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh ambaye amemaliza muda wake wa utumishi na amemtakia maisha mema na kumsihi kuendelea kuwa balozi mwema kwa Tanzania nchini Vietnam na duniani kwa ujumla.

"Kwa niaba ya Serikali napenda kukuhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Vietnam katika nyanja mbalimbali za kimataifa ikiwemo kuiunga mkono Vietnum katika kugombea nafasi mbalimbali katika Masirika ya KImataifa," Amesema Prof. Kabudi.

Nae Balozi Doanh ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikimpatia alipokuwa akitekeleza majukumu yake nchini wakati wote na kuahidi kuwa ushirikiano kati ya nchi hizo mbili utaendelea kuimarishwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akimuelezea jambo Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke leo katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam 


Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi leo katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akiongea na Balozi wa Vietnam  nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh ambaye amemaliza muda wake wa utumishi nchini Tanzania 


Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi  


Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi  



Thursday, June 25, 2020

PROF. KABUDI AKUTANA, KUMUAGA BALOZI WA IRELAND NCHINI TANZANIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, amekutana na kumuaga Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Paul Sherlock ambaye amemaliza muda wake wa utumishi na amemtakia maisha mema na kumwambia kuwa ni matarajio yake kuwa atakuwa balozi mwema kwa Tanzania nchini Ireland na kwingineko duniani.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, Prof. Kabudi amesema kuwa Ireland imekuwa na uhusiano mzuri wa kidiplomasia na Tanzania hasa katika kuunga mkono jitihada za kuimarisha sekta mbalimbali nchini ikiwemo miradi ya maendeleo, elimu, kilimo, afya pamoja na biashara na uwekezaji.

“Kupitia uhusiano imara kati ya Tanzania na Ireland hivi karibuni tulivyopatwa na janga la covid 19, Ireland imetoa msaada wa Euro milioni 1.5 ambapo baadhi ya fedha hizo zilipelekwa Shirika la Afya Duniani ofisi ya hapa Tanzania na Shirika la Chakula duniani ofisi ya hapa nchini kwa ajili ya kununua chakula lakini pia kwenda katika mfuko wa Benjamini Mkapa kwa ajili ya kuajiri wafanyakazi na kujenga vituo vya afya ili kutusaidia kupambana na Covid 19,” Amesema Prof. Kabudi.


Waziri Kabudi amemhakikishia Balozi Sherlock, kuwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Ireland utaendelea kuimarika hasa katika sekta ya uwekezaji na biashara, na kutoa wito kwa Serikali ya Ireland kuja kuwekeza hapa nchini katika sekta za kilimo, viwanda hasa vya nguo pamoja na ujenzi.  

Aidha, Balozi Sherlock ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikimpatia alipokuwa akitekeleza majukumu yake nchini na kuahidi kuwa ushirikiano uliopo utaendelezwa hasa ikizingatiwa kuwa nchi hizo mbili zimekuwa na uhusiano wa kidiplomasia kwa miaka 40.

" Natumaini kuwa serikali ya Ireland kupitia uhusiano wake na Tanzania itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania za kukabiliana na changamoto mbalimbali na kuhakikisha kuwa inasonga mbele kimaendeleo," amesema Balozi Sherlock.

Tanzania na Ireland zimetimiza miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia tangu Serikali ya Ireland ilipofungua ubalozi wake nchini Tanzania mwaka 1979.  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akiongea na Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Paul Sherlock wakati alipokuwa akimuaga katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Sherlock akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi akimkabidhi zawadi ya picha ya mlima Kilimanjaro Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Sherlock katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Sherlock akimuonesha moja ya picha katika kitabu alichompatia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi kama zawadi  



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi akimkabidi zawadi ya kitabu cha picha Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Sherlock  



MKUTANO WA MAWAZIRI WA KAMATI YA SADC YA ASASI YA USHIRIKIANO WA SIASA, ULINZI NA USALAMA KWA NGAZI YA MAKATIBU WAKUU WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM


Mkutano wa Mawaziri wa Kamati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama kwa ngazi ya Makatibu Wakuu/ Maafisa Waandamizi umefanyika Jijini Dar es Salaam kwa njia ya Mtandao (Video Conferencing).

Mhimili wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC unaongozwa na mfumo wa Utatu (Troika) ambapo kwa sasa Mwenyekiti ni Zimbabwe, mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu unaofanyika leo ni maandalizi ya mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 26 Juni 2020 chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara ya Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Sibusiso Busi Moyo na utakutanisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mambo ya Ndani, Ulinzi na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutoka nchi wanachama wa SADC.

Pamoja na mambo mengine mkutano umepokea na kujadili agenda zinazohusu masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Ukanda wa SADC.
Mkutano wa leo umehudhuriwa na nchi wanachama wa SADC ambazo ni Angola, Afrika Kusini, Botswana, DRC,  Eswatini, Lesotho, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Zambia, Zimbabwe na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC ni moja ya mihimili ya SADC inayosimamia masuala ya Usirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama katika Kanda. Mhimili huu unatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Mkataba wa uanzishwaji wa SADC wa mwaka 1992 na Itifaki ya Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC ya mwaka 2001.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (katikati), kushoto kwake ni Katibu  Mkuu Wizara ya Ulinzi, Dkt. Faraji Mnyepe , mwisho kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Christopher Kadio wakifuatilia mkutano  huo kwa njia ya video conference, Jijini Dar es salaam




Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na baadhi ya Maafisa waandamizi kutoka Tanzania wakifuatilia mkutano huo kwa njia ya Video Conference, jijini Dar es Salaam

                                  Mkutano ukiendelea

NAIBU WAZIRI DKT. NDUMBARO AFANYA ZIARA KATIKA MIPAKA YA NCHI ILIYOPO MKOANI RUVUMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) anaendelea na ziara ya siku sita (6) katika maeneo ya mipaka iliyopo mkoani Ruvuma. Mpaka sasa Dkt. Ndumbaro amefanya  ziara katika mpaka wa Wenje uliopo Wilayani Tunduru, Chiwindi uliopo Wilayani Nyasa na mpaka wa Magazini uliopo Wilayani Namtumbo Mkoa wa Ruvuma. Mipaka hii inaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbuji. 


Ziara hii ambayo inatokana na utekelezaji wa majukumu  ya Wizara, ikiwemo utekelezaji wa diplomasia ya uchumi ,kujenga, kulinda na kudumisha uhusiano wa kimataifa, inalenga kuwahimiza watendaji na Mamlaka mbalimbali za Mkoa na Wilaya za Mipakani kuhusu umuhimu wa wakudumisha, kulinda, na kuendeleza uhusiano mzuri baina ya Taifa letu na nchi tunazo pakana nazo ili kustawisha biashara baina yetu na nchi tunazopakana nazo. Kadhalika, ziara hii inalenga kuhimiza umuhimu wa kulinda mipaka ya nchi na kubaini changamoto zinazowakabili wakazi wa mipakani. 

Aidha, kwa upande wake Dkt. Ndumbaro amewataka watendaji na Wakuu wa Wilaya hizo, kuendelea kuwa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, vilele kutengeneza na kuanzisha masoko ya bidhaa mbalimbali maeneo ya karibu na mipakani kwa lengo la kuchagiza biashara, ajira na kuongeza mapato ya Serikali. "Wizara tumejipanga kutekeleza mkakati wa kuhakikisha kuwa tunashiriana kwa ukaribu na wadau wanaosaidia kutekeleza majukumu ya Wizara zikiwemo Mamlaka za Mikoa na Wilaya ambazo zipo mipakani" alisema Dkt. Ndumbaro

Wakati huo huo katika ziara hii Dkt. Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na kamati za ulinzi na usalama  katika Wilaya ya Namtumbo ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Sophia Mfaume, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Julius Mtatiro na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nayasa ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Isabela Chilumba. Wakuu wa Wilaya zote tatu pamoja Wakuu vya Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Wilaya hizo kwa nyakati tofauti waliambatana na Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro kuzuru maeneo ya Mipakani.

Wananchi wa Tunduru kwa upande wao wameishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki  kupitia Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro, kwa kuwatembelea na kusikiliza changamoto zinazowakabili. Baadhi ya changamoto walizozitaja ni pamoja na kutokuwepo kwa huduma ya kivuko cha uhakika, barabara (kiwango cha lami) ukosefu wa huduma ya  maji safi na salama ya uhakika na umeme. Hata hivyo Dkt. Ndumbaro ameeleza  hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa na Serikali  katika kuhakikisha kuwa changamoto hizo zinatatuliwa.


Aidha, Wananchi wa Chiwindi, Wilayani Nyasa  wamemwomba Dkt. Ndumbaro kufikisha salaam na shukrani zao kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kuleta maendeleo nchini, na hasa kwa kuzingatia mahitaji ya watu wa kipato cha chini. 

Dkt. Ndumbaro amezipongeza Mamlaka zilipo katika maeneo ya mipaka hiyo kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya ya kulinda mipaka, kudumisha mahusiano na nchi jirani na kwa kutekeleza kwa ufasaha dhana ya Diplomasia ya Uchumi licha ya changamoto zinazowakabili. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mhe. Sophia Mfaume, alipowasili Walayani hapo kwa lengo la kutembelea mpaka wa Magazini. Mpaka huu uliopo Wilayani humo unaiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisalimiana na Katibu Tawala Bw. Adeni Nchimbi alipowasili katika Ofisi ya Wilaya hiyo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisaini kitabu cha wageni alipowalisi Ofisi za Makao Makuu ya Wilaya ya Namtumbo.

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mhe. Sophia Mfaume akifungua Kikao kati ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb)
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisisitiza jambo alipokuwa akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Namtumbo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mamlaka mbalimbali wa Wilaya ya Namtumbo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akipolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru alipowasili katika Ofisi za Makao Makuu ya Wilaya hiyo. Akiwa Wilayani Tunduru Dkt. Ndumbaro ametembelea mpaka wa Wenje unaoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro akifungua Kikao kati ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb). 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akifafanua jambo alipokuwa akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru. Mpaka wa Wenje uliopo Wilayani humo unaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisikiliza risala kutoka kwa mwakilishi wa Wakazi wa Kijiji cha Wenje alipotembelea kijiji hicho kinachopakana na nchi jirani ya Msumbiji.  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Wenje kilichopo Wilayani Tunduru, Ruvuma.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Namtumbo. Mpaka wa Magazini uliopo Namtumbo unaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akinawa mikono kufuata kanuni na taratibu za kiafya, muhimu katika kujinga na maambukizi ya COVID-19 alipotembelea mpaka wa Wenje,Wilayani Tundu kama inavyoshauriwa na Wataalam wa Afya.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mhe. Isabela Chilumba alipotembelea Wilaya hiyo. Akiwa Wilayani Nyasa  Dkt. Ndumbaro ametembelea Mpaka wa Chiwindi unaoiunganisha Tanzania na jirani ya Msumbiji. 
Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mhe. Isabela Chiluba akifungua kikao kati ya Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, Serikali ya Kijiji, Polisi wa upande wa Msumbiji na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) kilifanyika mpakani Chiwindi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akivuka Mto unaoitenganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akizungumza na Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyasa, wawakilishi wa Serikali ya Kijiji na Polisi wa upande wa Msumbiji katika kikao kilichofanyika mpaka wa Chiwindi, Nyasa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyasa, wawakilishi wa Serikali ya Kijiji na Polisi wa upande wa Msumbiji walropo mpakani hapo.