Monday, February 23, 2015

Rais Kikwete amkabidhi Mtukufu Aga Khan Hati ya Utambulisho wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Kiongozi wa Madhehebu ya Ismailia Duniani, Mtukufu Karim Aga Khan alipowasili Ikulu, Mtukufu Aga Khan amefanya mazungumzo na Mhe. Rais na kukabidhiwa Hati ya Chuo Kikuu cha Aga Khan (Aga Khan University) kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mtukufu Aga Khan
Mhe. Rais Kikwete pamoja na Mtukufu Aga Khan wakifurahia jambo wakati wa mazungumzo yao.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Shukuru Kawambwa (Mb.) akizungumza na kumkaribisha Mhe. Rais Kikwete kwa ajili ya kumkabidhi Mtukufu Aga Khan Hati ya Utambulisho wa Chuo Kikuu cha Aga Khan nchini.
Wajumbe walioambatana na Mtukufu Aga Khan wakifuatilia mazungumzo hayo kwa makini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akimkabidhi Mtukufu Aga Khani Hati ya Chuo Kikuu cha Aga Khan nchini.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo kati ya  Mhe. Rais Kikwete, Mtukufu Aga Khan  na Waandishi wa Habari (hawapo pichani). Wa kwanza mstari wa pili ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga.
Mtukufu Aga Khani akizungumza wakati wa  mkutano kati yao na waandishi habari (hawapo pichani) huku Rais Jakaya Kikwete akimsikiliza
Mkutano na Waandishi wa Habari ukiendelea
Picha ya pamoja baada ya Mkutano


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.