Thursday, February 26, 2015

Rais Kikwete ashiriki Dhifa ya Kitaifa wakati wa ziara yake nchini Zambia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Mstaafu wa kwanza wa Zambia, Mhe. Keneth Kaunda mara baada ya kuwasili katika Hoteli ya Taj  Pamodzi kwa ajili ya kushiriki Dhifa ya Kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima  yake  na Rais Edgar Lungu wa Zambia (mwenye tai ndogo nyeusi). Mhe. Rais Kikwete amefanya ziara ya siku mbili nchini Zambia kwa mwaliko wa Rais Lungu.
Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Rais Lungu pamoja na Wake zao Mama Salma Kikwete (mwenye kilemba chekundu) na Mama Esther Lungu (wa kwanza kulia) wakifuatilia sala iliyotolewa kabla ya kuanza kwa Dhifa hiyo. Wengine ni Rais Mstaafu wa Zambia, Mhe. Kaunda, Makamu wa Rais wa Zambia, Bibi Inonge Wina (watatu kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb)
Rais Lungu akitoa hotuba
Viongozi wakitakiana afya njema na kuimarisha ushirikiano 
Mhe. Kaunda, Mhe. Wina na Mhe. Membe wakitakiana afya njema
Rais Kikwete akitoa hotuba

Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya pamoja na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Charles Tizeba nao wakishiriki dhifa hiyo
Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Grace Mujuma (kushoto) akiwa na Balozi wa Zambia nchini Tanzania, Mhe. Judith Kapijimpanga wakati wa dhifa
Mkuu wa Moa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro akiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salva Rweyemamu na Bw. Togolani Mavura wakati wa dhifa.
Sehemu ya Wageni waalikwa
Wageni waalikwa
Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Kaunda wakitakiana afya njema
Sehemu ya ujumbe wa Tanzania
Ujumbe wa Tanzania


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.