Thursday, February 26, 2015

Naibu Waziri Mambo ya Nje amuaga Balozi wa Japan

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akisalimiana na Balozi wa Japani anayemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Masaki Okada wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam leo.
  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akibadilishana mawazo na Mhe.Masaki Okada, Balozi wa Japani anayemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Katikati ni mke wa Balozi Mama Okada.
  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akisoma hotuba wakati wa hafla hiyo.
 Mheshimiwa Naibu Waziri akiendelea na hotuba huku wageni waalikwa wakimsikiliza.
 Balozi wa Japani anayemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Masaki Okada na Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati wakiwa wamenyanyua glasi zao juu kabla ya kugongeana glasi kwa ajili ya kutakiana heri na afya njema.
 Wageni waalikwa nao wakifanya ishara ya kutakiana heri katika hafla hiyo.
 Balozi wa Japani anayemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Masaki Okada akitoa shukrani zake kwa ushirikiano mzuri alioupata akiwa nchini Tanzania.
 Naibu Waziri Mhe.Mahadhi Juma Maalim (kulia), Balozi Mbelwa Kairuki (katikati), Mkuu wa Idara ya Asia na Australasia na Bibi Rosemary Jairo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora wakimsikiliza Balozi Masaki Okada kwa makini  katika hafla hiyo
 Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na wageni waalikwa wakimsikiliza Balozi Okada kwa makini.
  Bw. Adam Issara, Msaidizi wa Naibu Waziri (kulia) Bi.Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali (katikati) na Mke wa Balozi Mama Okada wakifuatilia kwa makini shukrani za Mhe. Balozi Okada.
  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) akimkabidhi zawadi Mhe. Balozi Okada katika hafla hiyo.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.