Tuesday, February 3, 2015

Rais wa Ujerumani awasili nchini kuanza ziara ya kitaifa


Rais wa Ujerumani, Mhe. Joachim Gauck pamoja na Mhe. Mama Schadt wakiteremka kwenye ndege mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku tano hapa nchini.
Mhe. Gauck akilakiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mohammed Gharib Bilal mara baada ya kuwasili nchini.
Mhe. Gauck na Mama Schadt wakipokea  maua kutoka kwa Watoto Elizabeth Jackson na Barqat Mvungi walioandaliwa kwa ajili ya mapokezi yake. 
Mhe. Gauck akiongozana na Mhe. Dkt. Bilal
Mhe. Gauck na Mama Schadt kwa pamoja na Mhe. Dkt. Bilal na Mkewe Mama Asha Bilal wakifurahia burudani ya ngoma wakati wa mapokezi yake.
Baadhi ya wakina mama wa Dar es Salaam waliofika kumpokea Rais Gauck wakipeperusha bendera ya Tanzania na Ujerumani kwa furaha 
Mhe. Rais Gauck akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine wakati wa mapokezi.
Mhe. Rais Gauck akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Philip Marmo wakati wa mapokezi yake.
Mhe. Gauck akifurahia jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Victoria Mwakasege aliyekuwepo uwanjani hapo kwa mapokezi. 
Rais Gauck akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Bw. Assah Mwambene


Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.