Friday, February 20, 2015

Waziri Membe ampokea Mtukufu Karim Aga khan

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akimpokea Mwanzilishi wa Taasisi ya Maendeleo ya Aga khan Duniani,  Mtukufu Karim Aga Khan mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mtukufu Aga Khan yupo nchini kwa ziara binafsi ya siku nne, ambapo pia atatumia fursa hiyo kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya taasisi hiyo hapa nchini.


 


Mtukufu Aga Khan akisalimiana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Nchini  Dkt. Shukuru Kawambwa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
 
Mtukufu Aga Khan akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Mindi Kasiga mara baada ya kupokelewa kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam Ijumaa tarehe 20.02.2015
Mtukufu Aga Khan akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje Hassan Mwamweta baada ya kuwasili jijini Dar es salaam kwa ziara ya siku nne nchini Tanzania. 
Waziri Membe akizungumza jambo na Mtukufu Aga Khan mara baada ya sherehe fupi ya mapokezi baada ya kuwasili nchini.  


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.