Friday, February 7, 2020

MKUTANO WA 7 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI WA MAZINGIRA NA USIMAMIZI WA MALIASILI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAFIKIA TAMATI JIJINI DODOMA

Meza Kuu ikifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa Mkutano wa Saba (7) wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Dodoma. Mkutano huu uliofanyika kwa kipindi cha siku 5 (tarehe 3-7 Februari, 2020) umefanyika katika ngazi tatu nazo ni; ngazi ya wataalamu, ngazi ya Makatibu Wakuu na ngazi ya Mawaziri. 
Mawaziri kutoka nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakisaini taarifa kwenye Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Dodoma, Ijumaa tarehe 7 Februari, 2020
Mawaziri kutoka nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakisaini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada kusaini taarifa ya Mkutano 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu wakijadili jambo kwenye Mkutano wa 7 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Dodoma.  
Mawaziri walioiwakilisha Tanzania wakishikishana jambo kwenye Mkutano wa 7 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.