Wednesday, February 19, 2020

UBELGIJI NA TANZANIA  ZAPANIA KUDUMISHA URAFIKI NA KUONGEZA USHIRIKIANO.
 Ubelgiji na Tanzania zimedhamiria kudumisha urafiki na kuongeza zaidi ushirikiano katika ubia wa maendeleo, uwekezaji, biashara, utalii na masuala mengine ya Kikanda na kimataifa. Hayo yalielezwa wakati wa mazungumzo baina ya Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mheshimiwa Jestas Abuok Nyamanga na  Mfalme wa Ubelgiji, Mtukufu Philippe  wakati Balozi Nyamanga akiwasilisha Hati zake za utambulisho kwa Mfalme huyo katika kasri yake jijini Brussels  tarehe 6 Februari 2020.
Wakati wa utambulisho huo, Balozi Nyamanga aliwasilisha salaam za Mheshimiwa Dkt John Pombe Joesph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mfalme huyo na kueleza jinsi Tanzania inavyoridhika na urafiki na ushirikiano mzuri uliodumu kwa miaka mingi baina ya nchi mbili na imedhamiria kuueleza ushirikiano huo na kupanua wigo wake.
Balozi Nyamanga katika mazungumzo hayo  amemweleza  Mfalme Philippe, juhudi za pekee zinazofanywa na serikali inayoongozwa na Rais Magufuli katika kuweka msingi wa uchumi wa viwanda;  kufungamanisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu; kuboresha mazingira wezeshi kwa uendeshaji wa biashara na uwekezaji; na kuimarisha usimamizi wa utekelezaji wa mipango mbalimbali  ya kitaifa, kikanda na kimataifa. 
Aidha, Balozi Nyamanga amemweleza Mfalme Philippe kuwa Tanzania imedhamiria kushirikiana na Ubelgiji hususan katika ubia wa maendeleo, biashara na uwekezaji wenye kuleta faida kwa pande zote.
 Kwa upande wake,   Mfalme huyo wa Ubelgiji ambaye kwa kuipenda Tanzania miaka ya nyuma  amewahi kuja Tanzania kwa mapumziko binafsi Zanzibar na kueleza kuwa Tanzania ni nchi muhimu kwa Ubelgiji na hivyo nchi yake itaendeleza ushirikiano zaidi na Tanzania katika kufanikisha mipango mbalimbali ya maendeleo nchini pamoja na kushirikiana katika masuala ya amani na usalama hususan kwa wa nchi za Maziwa Makuu na ajenda zingine zinazogusa maslahi ya nchi zetu mbili kimataifa. 
Ubelgiji ni miongoni mua Nchi zinazoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania ikiwa inashika nafasi ya kumi kati ya nchi zaikai ya 90 zilizowekeza nchini Tanzania. Aidha kutokana na ushirikiano mzuri uliopo Tanzania ni kati ya nchi 14 zinazoendelea duniani ambazo Ubelgiji imeingia nazo makubaliano maalum ya ushirikiano wa ubia wa maendeleo (Developmet Coop[eration Framework)


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.