Sunday, February 16, 2020

NAIBU WAZIRI DKT.NDUMBARO AHITIMISHA ZIARA YAKE KATIKA ENEO LA USHOROBA WA MTWARA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amehitimisha ziara yake katika Mikoa  inayopitiwa na mradi wa maendeleo wa kuboresha miundombinu ya Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (Mtwara Corridor). Mradi huu unahusisha ujenzi wa bandari ya Mtwara (ambao unaendelea kwa kasi), ujenzi wa barabara katika kiwango cha lami kuanzia Bandari ya Mtwara hadi bandari ya Mbamba Bay iliyopo Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma sambamba na ujenzi wa bandari hiyo.

Lengo la ziara hii ilikuwa ni kuangalia hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa miundombinu ya bandari na barabara katika ushoroba huo, kufanya mazunguzmzo na viongozi wa Serikali za Mikoa na Wilaya, ambapo Mheshimiwa Ndumbaro alitumia nafasi hiyo kuhimiza Mamlaka za Mikoa na Wilaya, kulinda na kuboresha uhusinao wa kidipolomasia na nchi tunazopakana nazo katika ukanda huo ili kujenga mazingira rafiki ya kibiashara, wakati huu ambao Serikali ya Awamu ya Tano imeboresha miundombinu inayowezesha kuzifikia nchi hizo kiurahisi zaidi.

Ujenzi wa miundombinu katika Ukanda wa Kusini mwa Nchi unachochea ukuaji wa biashara katika ukanda huo kwa kurahishisha usafirishaji na mawasiliano na kuzifikia kiurahisi Nchi jirani za Malawi, Kaskazini mwa Msumbiji na Zambia.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ndumbaro aliambatana na Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali, ambaye amefurahishwa na kuridhishwa na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga mazingira rafiki ya kibiashara na nchi jirani kwa kuboresha miundombinu inayoziwezesha nchi hizo kunufaika na huduma za bandari nchini kiurahisi na kwa gharama nafuu. 

Kadhalika, nia ya Mhe. Munthali Balozi wa Malawi nchini, katika ziara hiyo ilikuwa ni kuangalia kwa namna gani wafanyabiashara kutoka nchini kwake watanufaika na uboreshwaji wa miundombinu ya ushoroba wa Mtwara katika kusafirisha bidhaa zao kwa muda mfupi na gharama nafuu. 

Aidha, kwa nyakati tofauti Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mndeme na Mkuu wa Wilaya Nyasa Mhe. Isabela Chilluba wameelezea utayari wao wa kuratibu na kusimamia shughuli na fursa za biashara zinazotokana na maboresho ya miundombinu katika ukanda huo.

Ziara hii ni mwendelezo wa jitihada zinazofanywa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa  kushirikiana na Mamlaka mbalimbali za ndani katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kukuza biashara na kuvutia uwekezaji nchini.   

Ujenzi wa barabara ya Mtwara hadi bandari ya Mbamba Bay kwa kiwango cha lami unafikia ukingoni, mkandarasi anaendelea na ujenzi wa sehemu iliyosalia (Mbinga hadi Mbamba bay) ambapo anataraijia kukabidhi barabara hiyo Septemba, 2020.

Ujenzi wa miundombinu katika ushoroba wa Mtwara umeleta mapinduzi makubwa ya maendeleo ya uchumi na kijamii katika Mikoa ya Kusini mwa Tanzania sambamba na kuliongezea Taifa mapato.  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa (kulia) wakiwa kwenye mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa akielezea jambo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kwa kutumia kielelezo cha ramani, walipokuna kwa mazungunzumzo wakati wa ziara ya Dkt.Ndumbaro katika ushoroba wa Matwara. 
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa (kulia) na Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali (kushoto) wakiwa katika mazungumzo walipokutana wakati wa ziara ya Mhe. Dkt. Ndumbaro katika Mkoa huo
Kutoka kulia ni Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Bw. Alfayo Kidata Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, na Mhe. Evod Mmanda Mkuu wa Wilaya ya Mtwara wakiwa katika picha ya pamoja.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  akisalimiana na Wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara alipotembelea Ofisi za Bandari hiyo wakati wa ziara yake mkoani humo.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza na wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara (hawapo pichani). Aliwahimiza kujituma na kuongeza ubunifu ili kuongeza  ufanisi na tija wa bandari hiyo ambayo ukarabati wa kuiboresha unaendelea.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na Watendaji wa Bandari ya Mtwara na Viongozi wa Mkoa alipotembelea eneo la bandari ya Mtwara
Kutoka kushoto; Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Christina Mndeme Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, na Mhe.Glad Munthali Chembe Balozi wa Malawi nchini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. 
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Mhe. Isabela Chilluba Mkuu wa Wilaya ya Nyasa alipowasili wilayani humo kwa ziara ya siku moja
 Mkuu wa Wilaya Nyasa Mhe. Isabela Chilluba akitoka maelezo kwa Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  na Ujumbe wake katika moja ya fukwe na eneo la bandari ya Mbamba Bay iliyopo katika Ziwa Nyasa. 
Picha ya pamoja 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.