Wednesday, July 10, 2013

Hafla ya Chakula cha Jioni yafanyika kwa heshima ya Waziri wa Mambo ya Nje wa India

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimkaribisha katika hafla ya Chakula cha Jioni Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Preneet Kaur (mwenye nguo ya pinki walioketi) na ujumbe wake ambao walikuwa nchini kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na India uliofanyika tarehe 08 na 09 Julai, 2013.

Wajumbe kutoka Tanzania na India wakati wa hafla hiyo.

Mhe. Membe akimkabidhi Mhe. Kaur zawadi ya kinyago. Kulia ni Bw. Omar Mjenga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia.

Mhe. Kaur akisikiliza maelezo kuhusu zawadi hizo za vinyago alizokabidhiwa na Mhe. Membe.

Tuesday, July 9, 2013

Mhe. Rais Kikwete akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa India

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Preneet Kaur alipofika kwa ajili  ya mazungumzo rasmi. Mhe. Kaur yupo nchini  kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.

Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Mhe. Kaur kabla ya kuanza mazungumzo.

Mhe. Kaur akifafanua jambo Mhe. Rais Kikwete wakati wa mazungumzo yao.

Mhe. Rais Kikwete akimsindikiza Mhe. Kaur mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Mhe. Rais Kikwete akiagana na Mhe. Kaur mara baada ya mazungumzo yao. Kushoto kwa Mhe. Rais ni Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (kulia) akisisitiza jambo huku Bw. Cliford Tandari (katikati), Naibu Katibu Mkuu, Tume ya Mipango na Bw. Omar Mjenga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wakimsikiliza kwa makini walipokuwa eneo la Ikulu wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Waziri wa Mambo ya Nje wa India.

Monday, July 8, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



220px-Coat of arms of Tanzania.svg f1f71



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kikao cha 15 cha Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (The SADC Ministerial Committee of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation), kitafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam tarehe 10-13 Julai, 2013.

Kikao hicho kinachohusisha sekta ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kitatanguliwa na kikao cha Makatibu Wakuu na Maofisa Waandamizi tarehe 10 na 11 Julai, 2013 na kitahudhuriwa na Nchi zote wanachama wa SADC isipokuwa Madagascar, ambayo imesimamishwa uanachama.

Mawaziri watakutana tarehe 13 Julai, 2013, chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Mheshimiwa Bernard Kamilius Membe (Mb).

Pamoja na mambo mengine, Kikao hicho kitajadili hali ya kisiasa Kusini mwa Afrika, uimarishaji wa Demokrasia, Utekelezaji wa  Mpango Mkakati wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, Mikataba ya ushirikiano katika Nyanja za Ulinzi na Usalama pamoja na Ushirikiano baina ya SADC na Umoja wa Ulaya (EU).

Washiriki wa vikao vya Maofisa Waandamizi wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam tarehe 9 Julai, 2013 wakati Mawaziri watawasili tarehe 12 Julai, 2013.  

Kikao hicho cha Mawaziri kitafuatiwa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi, utakaofanyika Lilongwe, Malawi, tarehe 17-18, Agosti, 2013, ambao utahitimisha Uenyekiti wa Tanzania wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama, ulioanza tangu Agosti, 2012.  Mwenyekiti anayefuata wa Asasi hiyo atakuwa Namibia wakati Uwenyekiti wa SADC utachukuliwa na Malawi.

Nchi Wanachama wa SADC ni Angola, Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Sheli Sheli, Afrika Kusini, Swaziland, Tanzania, Zambia na Zimbabwe.


IMETOLEWA NA:


WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM

8 JULAI,  2013


Mhe. Membe afungua Mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission-JPC) kati ya Tanzania na India unaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro kuanzia tarehe 08 hadi 09 2013. Mkutano huo unaowashirikisha Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini na India utajadili pamoja na mambo mengine masuala ya ushirikiano katika sekta za Uchumi, Ufundi, Sayansi na Teknolojia, Elimu, Afya, Utalii, Kilimo na Nishati na Madini.

Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi huo.

Wadau wengine wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

Wadau kutoka India.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya India, Mhe. Preneet Kaur akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

Wadau wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Kaur (hayupo pichani)

Wadau zaidi.

Meza kuu kabla ya ufunguzi.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza machache kabla ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo. Anayeonekana pembeni ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini India.

Wajumbe wa Sekretarieti wakati wa mkutano huo.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur walioketi, katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Omar Mjenga (kulia) akiwa na Mjumbe kutoka India wakati wa Mkutano huo.


Picha na Reginald Philip na Olga Chitanda.




Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo rasmi na Waziri wa Mambo ya Nje wa India

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati) akiwa katika mazungumzo rasmi na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Bibi Preneet Kaur (hayupo pichani) kabla ya ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission-JPC) kati ya Tanzania na India unaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro kuanzia tarehe 8-9 Julai, 2013. Wengine katika picha ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (kulia).
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya India, Mhe. Bibi Preneet Kaur akiwa na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo rasmi kabla ya kuanza kwa mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.

Mhe. Kaur akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake rasmi na Mhe. Membe (hayupo pichani). Kulia kwa Mhe. Kaur ni Balozi wa India hapa nchini Mhe. Debnath Shaw.

Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Kaur (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo rasmi kuhusu kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na India.Kulia kwa Mhe.Membe ni Balozi Gamaha, Bw. Omar Mjenga, Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Asia na Australasia na Bw. Thobias Makoba, Msaidizi wa Waziri.Kushoto kwa Mhe. Membe ni Mhe. Balozi Kijazi na Bw.Clifford Tandari, Naibu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango.
Mazungumzo yakiendelea.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakielekea kwenye ufunguzi rasmi wa mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati nchi hizi mbili.

Saturday, July 6, 2013

Tanzania/Japan meet for their Annual Consultation meeting on Economic Cooperation


Dr. Philip Mpango, Executive Secretary of the President's Office Planning Commission gives his opening remarks during the meeting between Tanzania and Japan on economic cooperation of the two countries held yesterday at Hyatt Regency (Kilimanjaro) Hotel in Dar es Salaam.  Also in the photo is Ambassador Rajabu Gamaha (2nd right), Deputy Permanent Secretary of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.  

The Tanzania/Japan annual consultation meeting on economic cooperation is in session.  The two countries have been cooperating in various sectors that include water and sanitation, agriculture, roads projects, education and energy sectors as part and parcel of incorporating and implementing the Fifth Tokyo International Conference on Africa Development (TICAD V) declarations held a month ago in Yokohama City, Japan.  It is in that spirit that these projects are entwined with the Tanzania Development Vision of 2025, as continued efforts to revitalize the economic growth of the country.

Deputy Permanent Secretary Ambassador Rajabu Gamaha introduces himself during the meeting.  Also in attendance is Ambassador Salome Sijaona of the United Republic of Tanzania in Japan.

The meeting was also participated by Ambassador Mbelwa Kairuki (2nd left), Director of the Department of Asia and Australasia in the Ministry of Foreign Affairs, Mr. Kambona (3rd left), Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs and Mr. Clifford K. Tandari (4th left), Deputy Executive Secretary  - International Trade and Economic Relations in the President's Office Planning Commission. 

Also in attendance is Mr. Ottaro (right), Assistant Director of the Department of Policy and Planning in the Ministry of Foreign Affairs. 

Ms. Yoshiko Kijima, Director - Third Country Assistance Planning Division, International Cooperation Bureau, Ministry of Foreign Affairs in Japan and H.E. Ambassador Masaki Okada of Japan to the United Republic of Tanzania. 

Mr. Kambona and Ambassador Kairuki. 


Tanzania delegation that included H.E. Ambassador Salome Sijaona, Ambassador of the United Republic of Tanzania in Japan. 

Japanese delegation that was led by Ms. Yoshiko Kijima, Director - Third Country Assistance Planning Division, International Cooperation Bureau, Ministry of Foreign Affairs in Japan and also included Mr. Motoharu Watanabe, DIrector of Africa Division 2/Africa Department in Japan Itnernational CooperationH.E. Masaki Okada, Ambassador of Japan to the United Republic of Tanzania. 

Secretariat team that included Mr. Khatib Makenga (left seating), Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs and Mr. Senya R. Tuni (right), Senior Policy Analyst of the President's Office Planning Commission.


All photos by Tagie Daisy Mwakawago 



Post Dialogue Message by Joint Dialogue Convener Dr Mihaela Smith



Friday, July 5, 2013

The US President Delivers Remarks at Independence Day Celebration

President Kikwete congratulates US President Obama on the occasion of the National Day


Jakaya Kikwete - Doug Pitt Named Goodwill Ambassador Of Tanzania Hosted by President Kikwete
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Barack Obama, President of the United States of America on the occasion of the National Day of the United States of America.

The message reads as follows;

H.E. Barack Obama
President of the United States of America
Washington D.C.
USA

Your Excellency,

On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I wish to convey my sincere congratulations to you and through you to the Government and People of the United States of America on the occasion of your country’s 237thIndependence Day.

This year’s celebration of your independence day comes just after you have concluded ahistoric visit to Tanzania. We were touched by your presence amongst us, the memories of which we shall ever cherish.

I am confident that our two countries will continue to pursue our shared values and aspirations for the mutual benefit of our peoples.

I wish in this regard to reaffirm my commitment and desire to further strengthen our cordial and fraternal ties of friendship and cooperation.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for Your continued good health, peace and prosperity for the people of the United States of America”.


Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and 

International Co-operation, Dar es Salaam.

5th July, 2013



Wednesday, July 3, 2013

Matukio mbalimbali yaliyofanyika wakati wa Mkutano wa Wake wa Marais wa Afrika



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi Mkutano wa Wake wa Marais wa Afrika uliofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 2 na 3 Julai 2013. Mkutano huo unafadhiliwa na Taasisi ya George W. Bush, Jr.

Mke wa Rais, Mhe. Mama Salma Kikwete akitoa hotuba ya kuwakaribisha nchini Wake za Marais kutoka nchi za Afrika katika mkutano wao uliofanyika Jijini Dar es Salaam  tarehe  2 na 3 Julai, 2013. Pamoja na mambo mengine mkutano huo ulijadili masuala mbalimbali yanayoweza kuwainua wanawake Barani Afrika ikiwa ni pamoja na Elimu. Ujasiriamali na Afya Bora.

Mke wa Rais wa zamani wa Marekani, Mama Laura George W. Bush, Jr. akitoa neno la shukrani kama mfadhili wa mkutano huo.


Baadhi ya Wake wa Marais wakisikiliza hotuba ya Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani).

Wajumbe mbalimbali waliohudhuria mkutano huo wa Wake wa Marais
Mke wa Rais wa Marekani, Mhe. Mama Michelle Obama akichangia hoja na uzoefu wake kama mke wa rais  wakati wa Mkutano huo wa Wake wa Maraisi wa Afrika. Kushoto ni Mama Laura Bush akisikiliza.

Mama Obama akikumbatiana na Mama Laura George W. Bush, Jr. mara baada ya kuzungumza na Wake wa Marais.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dkt. Twalib Ngoma akiwakaribisha baadhi ya Wake wa Marais waliotembelea kuona shughuli zinazofanywa na Taasisi hiyo.

Baadhi ya Wake wa Marais wakimsikiliza Dkt. Ngoma alipozungumza nao.

Mke wa Rais wa Sierra Leone, Mhe. Mama Sia Nyama Koroma akimpa pole mmoja wa wagonjwa katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road

Dkt. Ngoma akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wake wa Marais na wagonjwa.
Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Rais Mstaafu George W. Bush, Jr. pamoja na Mama Salma Kikwete na Mama Laura George W. Bush, Jr. wakati wa Chakula cha Jioni kilichoandaliwa na Mama Salma kwa heshima ya Wake wa Marais.

Baadhi ya Wake wa Marais wa Afrika wakati wa chakula cha jioni

Mama Laura George W. Bush, Jr. akiwa na Mama Cherie Blair, Mke wa Waziri Mkuu mstaafu wa Uingereza.

Rais Mstaafu wa Marekani, Mhe. George W. Bush, Jr. akiteta jambo na Mhe. Rais Kikwete

Mhe. Rais George W. Bush, Jr. akitoa hotuba wakati wa chakula cha jioni

Wake wa Marais wakijadiliana jambo wakati wa  chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yao na Mama Salma Kikwete.

Brassband ikitumbuiza wakati wa chakula cha jioni
Afisa Mwandamizi katika Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Hellen Rwegasira akiwa na mmoja wa wajumbe wakati wa mkutano huo wa wake wa marais.


Picha na Reginald Philip na Olga Chitanda