Tuesday, July 9, 2013

Mhe. Rais Kikwete akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa India

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Preneet Kaur alipofika kwa ajili  ya mazungumzo rasmi. Mhe. Kaur yupo nchini  kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.

Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Mhe. Kaur kabla ya kuanza mazungumzo.

Mhe. Kaur akifafanua jambo Mhe. Rais Kikwete wakati wa mazungumzo yao.

Mhe. Rais Kikwete akimsindikiza Mhe. Kaur mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Mhe. Rais Kikwete akiagana na Mhe. Kaur mara baada ya mazungumzo yao. Kushoto kwa Mhe. Rais ni Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (kulia) akisisitiza jambo huku Bw. Cliford Tandari (katikati), Naibu Katibu Mkuu, Tume ya Mipango na Bw. Omar Mjenga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wakimsikiliza kwa makini walipokuwa eneo la Ikulu wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Waziri wa Mambo ya Nje wa India.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.