Monday, July 22, 2013

Rais Kikwete aongoza Watanzania kuaga miili ya Askari 7 waliouawa nchini Sudan; Waziri Membe pia ahudhuria


Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiweka saini kitabu cha maombolezi leo, mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisaini kitabu cha maombolezi mara baada ya kuwasili uwanjani hapo. 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezi.
 Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitafakari kwa kina tukio la mauaji wa Askari wa Tanzania lililotokea katika jimbo la Darfur nchini Sudan. Wengine katika picha ni Mhe. Shamsi Vuai Nahodha (Mb) (wa pili kushoto), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi (wa tatu kushoto) Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na Luteni Jenerali Samwel Ndomba (wa nne kushoto), Mnadhimu Mkuu wa Majeshi nchini.

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), (wa pili kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, naye alishiriki katika kuaga miili ya Askari 7 waliouawa nchini Sudan hivi karibuni. 

Mh. Waziri Membe akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Abdulrahman Kinana. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said Meck Sadiki.

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania, Mhe. Rais Kikwete akizungumza kwa masikitiko wakati wa kuaga miili ya Askari saba wa kulinda amani waliouawa na waasi katika jimbo la Darfur, nchini Sudan hivi karibuni.  Rais Kikwete amevitaka vikosi vya ulinzi nchini kutokata tamaa kutokana na maafa hayo bali wazidishe moyo na kuendelea kulitumikia kwa ufasaha Taifa lao. 

Miili ya Askari wa kulinda amani wa Tanzania waliouawa katika jimbo la Darfur nchini Sudan, ikiwasili kwenye Viwanja vya Diamond Jubilee tayari kwa kuagwa na wananchi, ndugu, jamaa na marafiki.

Simanzi na majonzi viliwatala kwa familia za Marehemu.

Mhe. Rais Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za mwisho kwa miili ya Marehemu.

Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal akitoa heshima zake za mwisho kwa Marehemu.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kulia) na Mke wa Makamu wa Rais wa pili wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (katikati), pamoja na Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro wakiwa kwenye majonzi mazito mara baada ya kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu hao.

Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Jenerali Davis Mwamunyange akitoa saluti za heshima za mwisho kwa Marehemu hao.

Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini Tanzania,  Bw. Phillipe Poinso akitoa heshima za mwisho kwa Askari wa Tanzania wa kulinda amani waliouawa jimbo la Darfur nchini Sudan hivi karibuni.  Bw. Poinso alikuwa akimwakilisha Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou.

Umati wa Wanajeshi na Wananchi waliokusanyika katika uwanja wa Diamond Jubilee leo kuaga miili ya Askari hao saba.


Picha zote na maelezo kwa hisani ya Zainul Mzige wa www.dewjiblog.com


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.