Thursday, July 11, 2013

Mkuu wa Majeshi afungua Mkutano wa Wakuu wa Vyombo vya Usalama wa Asasi ya SADC


Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Generali Devis Mwamunyange akifungua rasmi Mkutano wa Makatibu Wakuu na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 10 Julai, 2013.  Mkutano  huo ni maandalizi ya mkutano wa Mawaziri wa Asasi hiyo utakaofanyika tarehe 13 Julai, 2013.

Baadhi ya Wajumbe kutoka nchi wanachama wa SADC wakimsikiliza Generali Mwamunyange (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano  huo.

Wajumbe wengine wakati wa mkutano huo.

Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya Usalama nchini Namibia, Bw. Ben Likando na Bw. Tom Moyane, Kamishina wa Magereza wa Afrika Kusini wakati wa ufunguzi wa mkutano wa asasi hiyo. Tanzania ni Mweneyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC  wakati  Namibia ni  Makamu Mwenyekiti wa Asasi hiyo na Afrika Kusini ilikuwa Mwenyekiti kabla ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.