Sunday, July 28, 2013

Wizara yazungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mkumbwa Ally (mwenye suti) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya Wizara katika kutekeleza  Diplomasia ya Uchumi. Wengine katika picha ni Balozi Simba Yahya (kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Mbelwa Kairuki (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia pamoja na Bibi. Zamaradi Kawawa, Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo na Mratibu wa Mkutano huo.
 
Bibi Kawawa akizungumza kabla ya kumkaribisha Bw. Mkumbwa kuzungumza na Waandishi wa Habari.

Waandishi kutoka Vyombo mbalimbali vya Habari wakimsikiliza Bw. Mkumbwa (hayupo pichani) alipozungumza nao juu ya utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.
Balozi Yahya (kushoto) akijibu moja ya swali lililoulizwa na Waandishi wa Habari.

Balozi Kairuki (kulia) akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya hoja zilizotolewa naWaandishi wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.